Nafasi Ya Matangazo

December 07, 2012

Na Hamisi Mohamedi- Morogoro
Waziri wa mawasiliano nchini Prof.Makame Mbarawa amefungua kikao cha pili cha mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA kilichofanyika jijini Dar es salam.
 
Akizungumza katika ufunguzi huo Prof. Mbarawa amesema serikali imejipanga vyema katika kukabiliana na mabadiliko ya kutoka katika mfumo wa Analogy na kwenda Digital.

Prof. Mbarawa amewataka mawakala walioidhinishwa na mamlaka hiyo ya mawasiliano nchini TCRA wazingatie ubora wa matangazo kama inavyotarajiwa na wengi.
 
Pia kwaupande wa wamiliki wa nyombo vya habari Pro. Mbarawa amewataka wamiliki hao kujikita katika kutayarisha vipindi vya kuelimisha jamii hasa jamii ilioko vijijini ambayo ndio kundi kubwa la watanzania wapo huko.
 
Mkutano huo wa siku mbili ulikuwa na lengo lakuwakumbusha wamiliki wa vyombo vya habari na waandaaji wa vipindi waandae vipindi vya kuielimisha jamii
Posted by MROKI On Friday, December 07, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo