Nafasi Ya Matangazo

December 03, 2012

Shindano la Maisha Plus limefikia tamati huku mwana dada Bereniki Kimiro akiibuka mshindi na kujinyakulia Shilingi Milioni 20 za Kitanzania kibindoni.

Nafasi ya pili katika shindano hilo lililo waweka vijana katika kambini ni Venance Mushi amejishindia Tshs. Million 6 huku nafasi mshindi wa Tatu ni Justine Bayo, amejishindia Tshs. Million 4.

Mara baada ya kutangazwa mshindi,  Mshindi wa Maisha Plus 2012, Beneriki alimshuukuru Mungu kwa ushindi, na kusema kuwa ‘yeye si kitu kwa wenzake, hilo ni zali tu’..

Aidha amemshukuru baba yake mzazi kwa kumshauri kusali,a mewashukuru pia wapenzi watazamaji kwa kumpiga kura, ameahidi kuendeleza kile alichokianza kijijini na kuitendea haki nchi yake.. 

Bereniki amemshukuru babu wa Kijijini, Brother Masoud na Crew nzima ya Maisha Plus.. Amemshukuru pia mwanae Kelvin (6yrs) kwa kuvumilia kipindi chote bila kuongea na mama.

Amesema Mungu amejibu maombi yake kwani ukipiga goti, maombi yako yatajibiwa.


Posted by MROKI On Monday, December 03, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo