Nafasi Ya Matangazo

August 24, 2012

Wema Sepetu pia akizungumzia ujio wao ndani ya mji wa Moshi,kuwa wao kama Wasanii Nyota wa Filamu wamewasili mkoani humo kusaka vipaji vipya mbalimbali vya filamu,usahili huo unafanyika kwenye ukumbi wa Mr Price,ulioko mtaa wa Malindi.
Mmoja wa wasanii mahiri katika fani ya uigizaji hapa nchini,Wema Sepetu akifanya mahojiano mafupi na Millard Ayo wa Clouds FM mapema leo kwenye amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta ambalo linafanyika jioni ya leo mpaka lyamba ndani ya uwanja wa chuo cha Ushirika,ndani ya mji wa Moshi,ambapo katika tamasha hilo kiingilio kimepangwa kuwa ni nusu mnyama tu a.k.a 5,000/= kwa kila kichwa.
Mtangazaji wa Clouds FM,Millard Ayo akiwa Live mapema leo mtaa wa Malindi katika mpango mzima wa amsha amsha kwa wakazi wa Moshi kuhusiana na tamasha la Serengeti Fiesta 2012,ambapo pia katika tamasha hilo kutatolewa zawadi mbalimbali ikiwemo gari ndogo aina ya Vits kama uinavyo pichani ikinadiwa vilivyo.

Kama kawa amsha amsha ya tamasha la Serengeti Fiesta pia linatoa mafuta kwa daladala,pikipiki sambamba na bajaji lita 10 ama tano kutoka kampuni ya Gapco ambao pia ni sehemu ya wadhamini wa tamasha hilo kwa wakazi wa mji wa Moshi..
Msanii mwingine nyota katika tasnia ya filamu,Aunt Ezekiel akielezea ni namna gani tamasha la Serengeti Fiesta lilivyowambamba wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake,na pia ujio wao wa kuwatafuta wasanii wapya chipukizi katika tasnia hiyo ambayo wigo wake umekuwa ukitanuka na kukua siku hadi siku.
Wema Sepetu katika pozi na washabiki wake mapema mchana huu.
Mastaa wetu wa filamu hapa nchini,wametokelezeaje sasaaa.
Kiongozi wa msafara wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012,Mully B akiwa na mastaa wa filamu,Wema Sepetu na Aunt Ezekiel afu fulllll BBM kama kawa.
Millard Ayo akifanya mahojiano na Ray a.k.a Vincent Kigosi kuhusiana na ujio wao ndani ya  mji wa Moshi

Kutoka kushoto ni Mr Hatman,Steve Nyerere,Bonge pamoja na Millard Ayo katika shoo love ya pamoja.
Wema Sepetu akijiweka sawa.
Wakiwa katika mazungumzo yao ya hapa na pale.
Kila mmoja ana haki ya kupata habari na kuhabarishwa.

Pichani ni Gari aina ya Vits itakayotolewa jioni ya leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,kwa mshindi atakaejishindia kwenye droo itakayofanyika katika uwanja wa chuo cha ushirika,ambako tamasha hilo litarindima mpaka majogoo.
Jacob Steven a.k.a Steven akifafanua jambo mapema leo mtaa wa Malindi kuhusiana na suala zima la wasanii hao kulivamia jiji la Moshi
Posted by MROKI On Friday, August 24, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo