September 28, 2008
Blog hii inamuombea kwa Mungu amjalie afya njema haraka na matibabu mema.
September 25, 2008
September 24, 2008
September 23, 2008
TAARIFA AMBAZO ZIMEIFIKIA BLOG HII HIVI PUNDE ZINASEMA MWANDISHI WA MAGAZETI YA UHURU NA MZALENDO RAMADHANI KINYONYA ALIYEKUWA AMELAZWA KWA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI AMEFARIKI DUNIA.
BLOG HII INAWAPA POLE NDUGU JAMAA NA MARAFIKI NA WANAHABARI WOTE KWA UJUMLA KUTOKANA NA MSIBA HUU MZITO.
MUNGU ALAZE ROHO YA MAREHEMU PEMA AMINA.
BLOG HII INAWAPA POLE NDUGU JAMAA NA MARAFIKI NA WANAHABARI WOTE KWA UJUMLA KUTOKANA NA MSIBA HUU MZITO.
MUNGU ALAZE ROHO YA MAREHEMU PEMA AMINA.
Mburudishe akupigiae kwa shilingi 27 tu kwa siku (Caller Tune Services)
Sasa Tigo imepunguza gharama za Mlio kwa Mpigagaji (Caller Tune) Hii ni huduma inayomruhusu mteja kuweka wimbo kwenye simu yake ili ampigiae aweze kuusikia midundo miziki kabambe badala ya mpigaji kusikia mlio wa "ring ring".
Namna ya kupata huduma hii.
1) Mteja anapaswa kupiga namba 15007 na kufuatisha maelekezo atakayopewa.
Punde atapata wimbo anaoutaka anatakiwa kufuata maelekjezo ya nini cha kufanya hapohapo ili kunakili wimbo huo kwenye simu yake.
Gharama ya (Caller Tune services) mlio kwa mpigaji ni shilingi 27 tu kwa siku.
TIGO EXPPRESS YOURSELF.
September 22, 2008
NB: Makampuni ya simu vi[pi mnasema mnasema mpo nchi nzima?
Asante Kamanda Irine Bwire kwa snape hii.
September 20, 2008
Baadhi ya wafanyakazi 8 wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) waliofikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kistu jijini Dar es Salaam jana kujibu tuhuma za kughushi vyeti wakijifunika nyuso zao kuwakwepa paparazi Septemba 20 wakati wakienda kupanda karandinga tayari kwa safari ya Mahabusu hadi Oktoba 6 shitaka lao litakapo anza kusikilizwa.
Wafanyakazi hao, ni Justina J Mungai, ambaye imeelezwa kuwa ni mtoto wa Joseph Mungai, ambaye amewahi kushika wizara tofauti ikiwemo ya elimu, Christina G Ntemi, Siamini Eddie Kombakono, Janeth John Mahenge, Beatha Constantine Massawe, Jacquiline David Juma, Philimina Philibert Mutagurwa na Amina Mohamed Mwinchumu.
September 17, 2008
Msendo atoka kifungoni akiwa na furaha.
*aiteua siku ya kutoka jela kuwa ya kuzaliwa
*aha hidi kuendelea kuandika maovu
*
Na Mroki Mroki Kibaha
MWANDISHI wa Habari Mwandamizi, Zephania Musendo aliyekuwa akitumikia kifungo cha miaka mitano jela ametoka gerezaji jana.
Musendo aliyeanza kutumikia kifungo chake Mei 17, mwaka 2005 katika gereza la Keko kwa kupatikana na hatia ya kuomba na kupokea rushwa aliachiwa saa 9:54 na kupokelewa na wanafamilia yake waliofika kumpokea katika gereza la Mahabusu Mkuza mkoani Pwani.
Musendo aliyelakiwa na watoto wake Richard na Victor, mke wake Pascalia pamoja na shemeji yake Elizabeth N’gabo aliiteua siku yake ya kutoka gerezani na kuwa siku yake ya kuzaliwa baada ya yeye kutokuifahamu rasmi tarehe yake ya kuzaliwa.
“Leo ni siku yangu ya kuzaliwa maana ninafurahi sana kuwa hutru na kutoka katika matatizo haya ambayo yamenikabili kwa kipindi kirefu, baba yangu hakujua nilizaliwa lini zaidi ya mwaka kuwa ni 1947,”
Wanafafamilia hao wanasema wanafurahi sana babayao kuwa huru na wanamshukuru Mungu kwa kutoka jela akiwa hai na mwenye afya njema tofauti na walivyodhania.
Akisimulia maisha yake ya miaka mitatu na miezi mitano aliyoishi katika magereza mawili ya Keko na Mkuza anasema ni maisha hatari yasiyozoeleka na mwanadamu wa kawaida.
“Jela hakufai maana kitendo cha kutengwa na jamii, familia yako, nyumba ndugu jamaa na marafiki na kufanya mambo yako kwa uhutru ni hatari sana,” alisema.
Anasema alipokaa katika gereza la Keko kwa muda wa mwezi mmoja mambo hayakuwa mazuri sana kutokana na afya yake kutokuwa nzuri nay eye kulazimika kutumikia kifungo sambamba na kazi ngumu.
Licha ya kuwa hakupata usumbufu wa mateso kutoka kwa wafungwa wenzakwe lakini alipata tabu mwanzoni kutoka kwa Askari Magereza kwa kutekeleza adhabu yake kwa upande wa kazi ngumu.
“Nilipata shida kutoka kwa askari maana walikuwa hawanielewi kuwa ninaumwa , wao walishikilia midhali nimehukumiwa kazi ngumu lazima nizifanye tu,” alisema.
Alisema wakati akiwa katika gereza la Mkuza mkoani Pwani wakifabnya kazi ya kubeba kifusi katika jingo la Mkuu wa Mkoa alianguka katika ngazi na kushindwa kuendelea na kazi lakini hakupelekwa Hospitali siku hiyo kupatiwa matibabu.
Alianza kupatiwa matibabu ya Kisukari pamoja na Presha katika Hospitali ya Tumbi na kuandikiwa na daktari awe anakula mayai, maziwa na mboga za majani lakini aliporudi gerezani hakupata vitu hivyo hadi pale familia yake ilipoamua kumuwekea bili ya maziwa kutoka katika Ng’ombe gerezani hapo.
Aliendelea na kazi nyepesi gerezani hadi pale alipochaguliwa kuwa Nyapara mkuu Aprili 2007 nafasi ambayo aliitumikia hadi alipotoka gerezani humo.
Baadhi ya Askari Jela walisema watamkumbuka Musendo kwa nidhamu, Busara na Uongozi mzuri alipokuwa Nyapara mkuu katika gereza hilo ambalo linawafungwa 78 na mahabusu 129.
Aidha Musendo anasema maisha yake yalibadilika pale alipochaguliwa kuwa Nyapara mkuu na wenzake kumkubali na kumheshimu kutokana na umri wake.
“Kazi zangu kubwa zilikuwa kusimamia chakula, magenge ya kazi, usafi wa gereza na uandaaji wa risala kwa wageni zihusuzo wafungwa… kuna wakati niliandika hata risala za mkuu wa Gereza”.
Akizungumzia juu ya tuhuma zilizo mtia hatiani Musendo anasema yeye kwa sasa anafurahi na kushukuru Mungu kuwa yupo huru lakini Kubwa zaidi anafurahia kuwa habarizilizokuwa zikiandikwa katika gazeti zilikuwa ni zakweli.
Juu ya kurejea katiika ulingo wa habari Musendo anasema hatoacha kuandika na kampuni yeyote atakayopata ataanza kazi yake ya uandishi na kulitumikia taifa.
MWANDISHI wa Habari Mwandamizi, Zephania Musendo aliyekuwa akitumikia kifungo cha miaka mitano jela ametoka gerezaji jana.
Musendo aliyeanza kutumikia kifungo chake Mei 17, mwaka 2005 katika gereza la Keko kwa kupatikana na hatia ya kuomba na kupokea rushwa aliachiwa saa 9:54 na kupokelewa na wanafamilia yake waliofika kumpokea katika gereza la Mahabusu Mkuza mkoani Pwani.
Musendo aliyelakiwa na watoto wake Richard na Victor, mke wake Pascalia pamoja na shemeji yake Elizabeth N’gabo aliiteua siku yake ya kutoka gerezani na kuwa siku yake ya kuzaliwa baada ya yeye kutokuifahamu rasmi tarehe yake ya kuzaliwa.
“Leo ni siku yangu ya kuzaliwa maana ninafurahi sana kuwa hutru na kutoka katika matatizo haya ambayo yamenikabili kwa kipindi kirefu, baba yangu hakujua nilizaliwa lini zaidi ya mwaka kuwa ni 1947,”
Wanafafamilia hao wanasema wanafurahi sana babayao kuwa huru na wanamshukuru Mungu kwa kutoka jela akiwa hai na mwenye afya njema tofauti na walivyodhania.
Akisimulia maisha yake ya miaka mitatu na miezi mitano aliyoishi katika magereza mawili ya Keko na Mkuza anasema ni maisha hatari yasiyozoeleka na mwanadamu wa kawaida.
“Jela hakufai maana kitendo cha kutengwa na jamii, familia yako, nyumba ndugu jamaa na marafiki na kufanya mambo yako kwa uhutru ni hatari sana,” alisema.
Anasema alipokaa katika gereza la Keko kwa muda wa mwezi mmoja mambo hayakuwa mazuri sana kutokana na afya yake kutokuwa nzuri nay eye kulazimika kutumikia kifungo sambamba na kazi ngumu.
Licha ya kuwa hakupata usumbufu wa mateso kutoka kwa wafungwa wenzakwe lakini alipata tabu mwanzoni kutoka kwa Askari Magereza kwa kutekeleza adhabu yake kwa upande wa kazi ngumu.
“Nilipata shida kutoka kwa askari maana walikuwa hawanielewi kuwa ninaumwa , wao walishikilia midhali nimehukumiwa kazi ngumu lazima nizifanye tu,” alisema.
Alisema wakati akiwa katika gereza la Mkuza mkoani Pwani wakifabnya kazi ya kubeba kifusi katika jingo la Mkuu wa Mkoa alianguka katika ngazi na kushindwa kuendelea na kazi lakini hakupelekwa Hospitali siku hiyo kupatiwa matibabu.
Alianza kupatiwa matibabu ya Kisukari pamoja na Presha katika Hospitali ya Tumbi na kuandikiwa na daktari awe anakula mayai, maziwa na mboga za majani lakini aliporudi gerezani hakupata vitu hivyo hadi pale familia yake ilipoamua kumuwekea bili ya maziwa kutoka katika Ng’ombe gerezani hapo.
Aliendelea na kazi nyepesi gerezani hadi pale alipochaguliwa kuwa Nyapara mkuu Aprili 2007 nafasi ambayo aliitumikia hadi alipotoka gerezani humo.
Baadhi ya Askari Jela walisema watamkumbuka Musendo kwa nidhamu, Busara na Uongozi mzuri alipokuwa Nyapara mkuu katika gereza hilo ambalo linawafungwa 78 na mahabusu 129.
Aidha Musendo anasema maisha yake yalibadilika pale alipochaguliwa kuwa Nyapara mkuu na wenzake kumkubali na kumheshimu kutokana na umri wake.
“Kazi zangu kubwa zilikuwa kusimamia chakula, magenge ya kazi, usafi wa gereza na uandaaji wa risala kwa wageni zihusuzo wafungwa… kuna wakati niliandika hata risala za mkuu wa Gereza”.
Akizungumzia juu ya tuhuma zilizo mtia hatiani Musendo anasema yeye kwa sasa anafurahi na kushukuru Mungu kuwa yupo huru lakini Kubwa zaidi anafurahia kuwa habarizilizokuwa zikiandikwa katika gazeti zilikuwa ni zakweli.
Juu ya kurejea katiika ulingo wa habari Musendo anasema hatoacha kuandika na kampuni yeyote atakayopata ataanza kazi yake ya uandishi na kulitumikia taifa.
NB:
Gazeti la HabariLeo ndio gazeti pekee lililopata picha za tukio hili pamoja na Habari. Usikose Makala yake toleo la Septemba 18 2008 katika HabariLeo. www.habarileo.co.tz
September 14, 2008
Habari ya kazi kaka zangu wapenzi, I hope tunaenda sawa na mwezi mtukufu wa ramadhani.
Mimi ni mjasirimali mwenzenu na sasa nimepania kuwakwamua wenzangu kiuchumi. Nimeandaa semina kubwa Millenium Tower 'Makumbusho' Semina hiyo inahusu jinsi ya kujikwamua kiuchumi na mtu kutoka katika umaskini. Lengo letu ni kusaidiana ili kujiinua, Mtaji tunao ni sisi wenyewe kuchukua hatua. Semina hiyo itakua J.5 saa 8 mchana na J.mosi saa 8 machana. Kutokana na blog yako kutembelewa na watu wengi wa rika mbali mbali naomba uniwekee katangazo kaka hata na wewe unakaribishwa. Hakuna kiingilio ni bureeeee....
Kwa watakaofika wasiliana na no. 0767 17 77 74
Mimi ni mjasirimali mwenzenu na sasa nimepania kuwakwamua wenzangu kiuchumi. Nimeandaa semina kubwa Millenium Tower 'Makumbusho' Semina hiyo inahusu jinsi ya kujikwamua kiuchumi na mtu kutoka katika umaskini. Lengo letu ni kusaidiana ili kujiinua, Mtaji tunao ni sisi wenyewe kuchukua hatua. Semina hiyo itakua J.5 saa 8 mchana na J.mosi saa 8 machana. Kutokana na blog yako kutembelewa na watu wengi wa rika mbali mbali naomba uniwekee katangazo kaka hata na wewe unakaribishwa. Hakuna kiingilio ni bureeeee....
Kwa watakaofika wasiliana na no. 0767 17 77 74
September 12, 2008
Wapigapicha za Habari wa tatu wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam leo wamenusurika kufa katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi wakiwa njiani kelekea Kilwa katika futari maalum iliyoandaliwa na kampuni ya Vodacom kupitia Voda Foundations. Wapigapicha hao ni Athumani Hamisi wa Daily News na Habarileo, Herry Makange wa DTV na Channel 10 pamoja na Anthony Siame wa New Habari Cooparation. Halizao zinaendelea vyema isipokuwa Athumani aliyepata majeraha kichwani tumboni na mkononi baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka mara tatu. Athumani kwa sasa yupo Hospitali ya taifa Muhimbili kwa matibabu na yupo wodi ya Dharula.
September 05, 2008
Subscribe to:
Posts (Atom)