Nafasi Ya Matangazo

September 27, 2013

WATUHUMIWA watatu kati ya watano waliokuwa wakikabiliwa na  kesi ya  wizi wa fedha kwenye  Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wamehukumiwa kifungo jela baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwatia hatiani ambapo kati yao ni mke na mume.

Mke na mue hao ni Manase Makale aliyetupwa jela miaka 5 na mkewe Eddah Makale aliyetupa jela miezi 18 sawa na mwaka mmoja na nusu  Pamoja na Bahati  Mahenge, aliyehukumiwa kifungo cha Miaka 7 lupango.

Mbali na hukumu hiyo washitakiwa hao waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya wizi wa Sh1.86 bilioni za EPA, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kupitia Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex wametakiwa kulipa fedha kiasi cha Sh 1.5 Bilioni.

Washitakiwa wawili wameachiwa huru na Mahakama hiyo baada ya Mahakama kushindwa kuwatia hatiani. 
Posted by MROKI On Friday, September 27, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo