Nafasi Ya Matangazo

May 12, 2024



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) amewasili jijini Paris, Ufaransa na kupokelewa na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Ali Mwadini tarehe 12 Mei, 2024.

Mhe. Makamba anatarajia kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Nishati Safi ya Kupikia barani Afrika utakaofanyika tarehe 14 Mei, 2024 katika Makao Makuu ya UNESCO.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo utaongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye atakuwa Mwenyekiti Mwenza kufuatia mwaliko wa Taasisi ya Kimataifa ya Nishati (International Energy Agency). Aidha, Mhe. Rais anatarajia kuhutubia hafla ya ufunguzi ya Mkutano husika.

Wenyeviti wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kimataifa ya Nishati, Dkt. Fatih Birol; Waziri Mkuu wa Norway, Mhe. Jonas Gahr Støre na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Adesina.
Posted by MROKI On Sunday, May 12, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo