Nafasi Ya Matangazo

May 14, 2024

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia Viongozi mbalimbali, wadau wa Nishati pamoja na Washiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024. Rais Samia pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano huo wa Kimataifa ambao umewakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali Duniani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Wenyeviti Wenza, Waziri Mkuu wa Norway Mhe. Jonas Gahr Støre wa pili kutoka kulia, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina wa kwanza kulia pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kimataifa ya Nishati (IEA) Mhe. Dkt. Fatih Birol wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Wenyeviti Wenza, Waziri Mkuu wa Norway Mhe. Jonas Gahr Støre wa pili kutoka kulia, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina wa kwanza kulia wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024.
Viongozi, Wadau wa Nishati pamoja na Washiriki mbalimbali wakiwa kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024

Viongozi, Wadau wa Nishati pamoja na Washiriki mbalimbali wakiwa kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri Mkuu wa Norway Mhe. Jonas Gahr Støre kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Kimataifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Afrika uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO Jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 14 Mei, 2024.
****************
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema licha ya Afrika kuwa na idadi kubwa ya watu na raslimali zote muhimu, ni bara la chini kuwa na upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.
 
Zaidi ya Waafrika milioni 900 wanatumia nishati isiyo safi ya kupikia, jambo ambalo linachangia uharibifu wa mazingira, upotevu wa bioanuai na athari za kiafya.
 
Rais Samia amesema nishati safi ya kupikia ina maeneo matatu. La kwanza hasa maeneo ya vijijini ni uwezo mdogo kutokana na gharama kubwa na upatikanaji wake pia ni tabu.
 
La pili ni ulimwengu kwa jumla kutolipa suala hilo kipaumbele. Ufadhili mdogo na watu kutokujua fursa za kiuchumi zilizopo kwenye nishati safi ya kupikia inayorejesha nyuma harakati hizo.
 
Na pia kutokuwepo ushirikiano wa kuhakikisha nishati safi ya kupikia inapatikana kwa wote. Rais Samia amesistiza upatikanaji, gharama ndogo na suluhu zinazotekelezeka.
 
Rais Samia pia amesema kuongezeka kwa upatikanaji wa nishati safi ya kupikia itasaidia wanawake kupata fursa zaidi kushiriki shughuli nyingine za kiuchumi, kupunguza umaskini na usawa wa kijinsia.
 
Licha ya changamoto hizo, Tanzania ina dhamira ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia uliozinduliwa hivi karibuni uliokusudia kufikia 80% ya Watanzania wanaotumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.
 
Mkutano huu umehudhuriwa na zaidi ya watu 1000 wakiwemo Marais, Viongozi mbalimbali, Asasi za Kiraia, Watu mashuhuri wenye ushawishi kwenye masuala ya nishati safi na wengine wengi.
 
Malengo hasa ni kuhakikisha mbali na Afrika kupata uelewa lakini pia liwe jambo la Kimataifa ambapo pia itakuwa rahisi kuchangia ili kuweza kutekeleza azma hiyo.
 
Pia nia ni kuandaa sera madhubuti inayotekelezeka kwa ajili ya nishati safi ya kupikia na kuharakisha ushirikiano wa wadau katika suala hilo.
 
Inakadiriwa kuwa dola za kimarekani bilioni 4 zinahitajika kila mwaka ili kufanikisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa Waafrika wote ifikapo mwaka 2030.
 
Mkutano huu umeandaliwa nchini Ufaransa na Shirika la Nishati Duniani (IEA) ambapo Rais Samia Suluhu Hassan ndio Kinara wa Nishati Safi ya Kupikia Afrika.
Posted by MROKI On Tuesday, May 14, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo