Nafasi Ya Matangazo

May 16, 2024

Baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Mei 15,2024 kuongeza siku tano kwa vijana wenye nia na sifa za kujiunga na Jeshi la Polisi ili kuendelea kuwasilisha maombi ya ajira idadi ya waombaji imeendelea kuwa kubwa hivyo baadhi ya waombaji kushindwa kutuma maombi.
 
Jeshi la Polisi linaendelea kufanya maboresho kwa kuandaa mazingira ya kuwezesha kupokea maombi zaidi ili kutoa fursa kwa waombaji wote kutuma maombi yao ndani ya muda uliopangwa.
 
Aidha, waombaji waendelee kutuma maombi kupitia https://ajira.tpf.go.tz/
badala ya kupitia kwenye tovuti ya Polisi www.polisi.go.tz.
 
Taarifa zaidi itatolewa baada ya wataalam kukamilisha kazi ya kuongeza mazingira ya kupokea maombi mengi zaidi kwa wakati mmoja.

Posted by MROKI On Thursday, May 16, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo