Nafasi Ya Matangazo

July 11, 2023

 
 
 
Na Mwandishi Wetu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji Bi. Mwantum Mgonja ameipongeza kampuni ya Mainstream Media Limited kwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika mkoa wa Kigoma.
 
Pongezi hizo zimetolewa mbaada yakampuni hiyo  kuanzisha kituo che redio cha Main Fm 91.7 ambayo kutoa habari na taarifa katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo yanayofanywa na serikali ndani ya mkoa wa Kigoma
 
Bi. Mwantum ameyasema hayo wakati wa mahojiano katika studio za Main Fm kwenye tukio la kuwasha kipaza sauti (mic) kwa mara ya kwanza.
 
Mkurugenzi huyo alisema serikali imetoa fedha  kwa ajili ya kujenga na kuboresha miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya manispaa ya Kigoma Ujiji katika sekta mbalimbali hususani afya na elimu   na  pia ni bahati na kusema redio hiyo itasaidia kutoa taarifa za aina hiyio kwa umma huku akishukuru kwa kupata fursa ya kukizindua.
 
Aidha mkurugenzi huyo pia alipata fursa ya kutoa ufafanuzi juu ya mambo mbali mbali ambapo alisema kuwa mfuko wa maendeleo ya vijana unafanyiwa marekebisho na kuwataka vijana wa Mkoa wa Kigoma kuendelee kusikiliza vyombo vya habari hususani Main fm 91.7 kwa ajili ya kujua fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya mkoa wa Kigoma ikiwemo mikopo nafuu inayotolewa na serikali kwa ajili ya kuwainua vijana kiuchumi.
 
Mwantum aliambatana na diwani viti maalum kata ya Mwanga Kusini,mtendaji wa kata ya Mwanga Kusini na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kilimahewa pamoja na wadau mbalimbali kutoka  ndani ya mkoa wa  Kigoma.
 
Zoezi hili ya Kuwasha Vipaaza sauti (Mic) kwa mara ya kwanza lilifanyika Tarehe 10 Julai 2023.
 
Mainstream Media Limited, pamoja na uwekezaji huo pia wametoa fursa za ajira kwa Watangazaji na wadau wa tasnia ya habari  kutoka maeneo mbali mbali duniani ili kuhakikisha kuwa kituo chao hicho kinafikisha ujumbe kwa urahisi na haraka zaidi kote duniani.
 
Zoezi la kuwasha Vipaaza sauti (Mic) lilienda sambamba na kuwaruhusu wasikilizaji wa redio hii duniani kote kuisikiliza kupitia kwenye tovuto ya Main FM (www.mainfm.co.tz)
 
Pia Meneja wa kituo Bw. Felician hulilo, alisema kuwa RMain FM imeanzia Kigoma lakini menejimenti yake imelenga kuipeleka katika mikoa yote ya Tanzania.

Posted by MROKI On Tuesday, July 11, 2023 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo