Spika wa Bunge Dkt. Tulia Akson akizungumza katika mkutano wa hadhara alioufanya katika Kata ya Iyunga Jijini Mbeya leo Julai 14,2023
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amewataka Wananchi kupuuza hoja za baadhi ya watu wenye nia ovu wanaosema kwamba Serikali inampango wa kuuza Bandari ya Dar es Salaam huku wakijua fika kuwa ni mashirikiano ya kibiashara yanayofanywa na si vinginevyo.
Dkt. Tulia ameyasema hayo leo
tarehe 14, Julai 2023 wakati wa mkutano wa hadhara alioufanya katika Kata ya
Iyunga Jijini humo kwa lengo la kuwaelezea Wananchi baadhi ya ahadi
alizozitekeleza katika Jimbo hilo ikiwemo Kata hiyo pamoja na yale yaliyofanywa
na Serikali ya awamu ya sita.
Amewaeleza kuwa katika kipindi
chake cha Uongozi wa miaka miwili ndani ya Jimbo hilo kwa kushirikiana na
Serikali wameweza kufanikisha utatuzi wa changamoto mbalimbali ikiwemo kuwezesha
ujenzi wa barabara ya njia nne kutoka Inyala hadi Airport ambao utekelezaji
wake umeshaanza.
Kuhusu changamoto ya maji na
afya, Dkt. Tulia amewaeleza Wananchi hao kwamba Serikali imewezesha kupatikana
kwa ufumbuzi huo kupitia mradi wa mto Kiwila ambao utamaliza tatizo hilo kwa
Mkoa mzima wa Mbeya na kuhusu afya tayari Serikali imewezesha upatikanaji wa
vifaa tiba katika Hospitali zote ndani ya Jiji hilo.
“Niwaombe sana, watu hawa
wapuuzwe na niwahakikishie tupo salama na hakuna cha bandari wala nchi
inayouzwa na hata wakija hao wanaosema imeuzwa waambieni wawapatie mgao wa hayo
mauzo” Amesisitiza Dkt. Tulia.
0 comments:
Post a Comment