Nafasi Ya Matangazo

November 22, 2021

Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa akizindua  Mfumo wa maombi ya kazi kupitia simu za kiganjani uliofanyika katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Mhe.Mohamed Mchengelwa (wa katikati), Naibu Waziri ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (wa pili kushoto), Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora Dkt. Laurean Ndumbaro(wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bi.Sophia Kaduma (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bw. Samweli Tanguye wakifuatilia kwa umakini mfumo wa maombi ya kazi kupitia simu za kiganjani kwenye screan  za ukumbi.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi akitoa hotuba yake mbele ya Mgeni Rasmi kwa kuelezea namna ambavyo mfumo utafanya kazi na kuwasaidia waombaji fursa za ajira nchini.
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye ukumbi wa Tume ya Uchaguzi wakishuhudia uzinduzi wa " Ajira Portal Mobile App" jijini Dodoma
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira  Bw. Xavier Daudi ( wa kwanza kulia aliyekaa)  pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Waziri Mhe. Deogratius Ndejembi (wa pili kutoka kulia aliyekaa), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Laurean Ndumbaro ( wa pili kutoka kushoto aliyekaa) Mwenyekiti wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira Bi.Sophia Kaduma (wa kwanza kushoto aliyekaa) na Katibu  wa Sekretarieti ya Ajira  Bw. Xavier Daudi ( wa kwanza kulia aliyekaa)  pamoja na wawakilishi  kutoka Mradi wa Maendeleo PS3+ mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (wa tatu kutoka kulia aliyekaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na  Menejimenti ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma  mara baada ya kuzindua Ajira Portal Mobile App.
***********
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imezindua App ijulikanayo kama “Ajira Portal Mobile App” ambayo itakuwa na manufaa makubwa kwa waombaji fursa za ajira kupata taarifa za uwepo wa nafasi za kazi, taarifa za nichakato ya ajira kupitia simu zao za kiganjani.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira  katika Utumishi wa Umma Bw.Xavier Daudi amesema kuwa huduma hii itakuwa inapatikana kwenye Playstore za simu janja na waombaji wa fursa za ajira wataweza kujisajili, kuingia kwenye akaunti zao, kupakia taarifa za vyeti vyao na kuomba kazi kupitia mobile app hiyo.

Aidha,amesema kuwa uwepo wa huduma hii utaongeza wigo wa upashanaji wa habari na kuokoa fedha zilizokuwa zikipelekwa kwenye internet café na baadhi ya waombaji fursa za ajira. Pia amesema mfumo huu utasaidia upatikanaji wa taarifa za walioajiriwa ndani ya sekta ya umma kuwa rahisi zaidi, kuwaondolea usumbufu waombaji wa fursa za ajira kwa kutumia mfumo mmoja wa ajira na utapunguza siku za kuendesha usaili kutoka siku 42 za sasa hadi kufikia siku 38.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Mohamed Mchengelwa (Mb) amesema kuwa ili Sekretarieti  ya Ajira iweze kutekeleza kwa ufanishi  majukumu yake inahitaji ushirikiano na uwajibikaji wa mtu mmoja mmoja katika eneo lake ikiwemo waombaji wa fursa za ajira Serikalini, Waajiri wa Taasisi za Umma na wadau mbalimbali wa maendeleo.

“Nayasema mambo haya ili tuone suala la ajira katika Utumishi wa Umma ni suala la msingi  na muhimu linalotuwezesha kupata nguvu kazi yenye ubunifu,ujuzi na maadili mema ili kuiwezesha Serikali kutekeleza ipasavyo malengo yake inayojiwekea hususani kufikia Uchumi wa kati wa Juu” alikaririwa akisema.

Hata hivyo  Waziri Mchengelwa ameipongeza  Sekretarieti ya Ajira kwa ubunifu na maboresho ambayo imekuwa ikiyafanya kwa kutumia TEHAMA ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu  yao muhimu.

Waziri Mchengelwa alizindua” Ajira portal Mobile App “jijini Dodoma katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi hafla ambayo ilihudhuriwa na waombaji fursa za ajira katika Utumishi wa Umma, Wawakilishi kutoka  Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma  PS3, Wajumbe wa Bodi ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma pamoja na Menejimenti ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Posted by MROKI On Monday, November 22, 2021 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo