Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano inapenda kuutarifa umma kuwa kesho tarehe 19/12/2018, itafunga kwa
muda barabara ya Morogoro sehemu ya Kimara Stop Over hadi Temboni Wilayani
Ubungo jijini Dar es Salaam kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana.
Taarifa iliyotolewa kwa umma
na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi),
Joseph Nyamhanga inasema Kufungwa kwa muda barabara hii kunatokana na kuwepo
kwa sherehe ya uwekaji wa jiwe la msingi la upanuzi wa barabara hiyo yenye
urefu wa kilometa 19.2 kutoka Kimara hadi Kibaha kuwa njia nane (8)
itakayofanyika eneo la Kimara Stop Over.
“Wizara inashauri watumiaji wa
barabara hiyo kutumia barabara mbadala kwa muda wote ambao barabara hiyo
itakuwa imefungwa kwa muda” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha, Wizara inawaomba radhi
watumiaji wote wa barabara hiyo kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
0 comments:
Post a Comment