Nafasi Ya Matangazo

October 13, 2017

Habari njema zinatoka kwa nguli wa mavazi Afrika, Mustafa Hassanali, amekuwa mmoja kati ya wabunifu 21 kutoka Afrika, ambao wameonesha vipaji vyao vya kipekee katika jukwaa la mitindo lenye hadhi ya kipekee Afrika, linalofanyika kila mwaka nchini Ethiopia lijulikanalo kama “HUB OF AFRICA FASHION WEEK 2017”.

Wiki  hii  Mustafa alizindua mavazi yake mapya yaliyobeba jina la “tengeneza Tanzania “ au “Make in Tanzania”.

Mavazi hayo vyenye nia ya kutoa mchango katika kutimiza juhudi za Rais wetu, John Magufuli, katika kutimiza sera uchumi wa  viwanda na uwekezaji, na si hivyo tu bali, kutoka kipindi hicho hadi leo, yamekuwamatamanio makubwa ya Mustafa kuanzisha na kutangaza viwanda vya nguo vilivyopo  Tanzania, na kufanya nchii yetu kuwa soko pekee kwa nchi zingine za Afrika. Na hiyo ndo siri pekee ya mavazi yake.

Mavazi haya yamekuwa na utofauti kubwa na mavazi mengine ya Mustafa, “Make in Tanzania Collection” ni nguo zenye mikato ya kipekee, na michoro ya kupendeza iliyopo katika kitambaa hicho cha pamba.

Mavazi hayo yamepambwa na mkusanyiko wa rangi nzuri na nguo hizi zinapendeza kuvaliwa katika mitoko ya mchana au msimu wa kiaangazi na hufaa kwa wote wanaume na wanawake.

 Kama Rais wa Marekani marehemu John F Kennedy alivyowai kusema “usiulize nchi yako inaweza kukufanyia nini, uulize unachoweza kufanya kwa nchi yako”, hivyo basi Mustafa haja tangaza jina lake tu pia amekuza na amepata nafasi ya kujulisha wadau wa viwanda na wahamasishaji mitindo duniani, uwepo wa Viwanda vya nguo na sekta ya Mitindo ya Tanzania kupitia ubunifu wake wa mitindo.


 Mbunifu Mustafa Hassanali katika maonesho hayo.
Wanamitindo waki[pita kuonesha mavazi ya Mbunifu Mustafa Hassanali
Posted by MROKI On Friday, October 13, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo