Nafasi Ya Matangazo

August 11, 2016

Mawakala wa Kanda ya Nyanda juu Kusini waliohudhuria uzinduzi wa kampeni mkoani wakifuatilia matukio na kutoa mawazo ambapo pia walipata fursa ya kutoa maoni yao kibiashara

 Mawakala wa Kanda ya Nyanda juu Kusini waliohudhuria uzinduzi wa kampeni mkoani wakifuatilia matukio na kutoa mawazo ambapo pia walipata fursa ya kutoa maoni yao kibiashara



KAMPENI ya kuwania kujishindia malori ya usambazaji iliyolenga kuwanufaisha mawakala wa kampuni ya Tanzania Distilleries   kupitia kampeni inayojulikana kama “Nunua,Uza,Shinda na Konyagi inazidi kushika kasi kadri muda wake wa kumalizika unavyosogea ambapo mawakala wanaendelea kuchuana kuuza bidhaa za kampuni kwa ajili ya kufikia lengo lililowekwa ili waweze kushiriki kwenye droo ya kupata washindi itakayofanyika mapema mwezi Oktoba.

Kampeni hiyo ambayo imewalenga wasambazaji katika mikoa  yote nchini itawawezesha washindi  2 kujishindia kila mmoja lori aina ya Eicher  yenye uzito wa tani 3 na pia  katika kipindi hiki cha kampeni wanaendelea kujipatia zawadi mbalimbali.

Akiongelea maendeleo ya kampeni hii baada ya kukamilika zoezi la uzinduzi wake kwenye kanda za mikoa mbalimbali,Meneja Masoko na Udhamini wa TBL Group,George Kavishe,alisema kuwa mwitikio wa mawakala katika kushiriki ni mzuri  kinachosubiriwa ni washindi wawili kujinyakulia malori ya kuwarahisishia  zoezi la usambazaji na biashara zao kwa ujumla. SOMA ZAIDI HAPA

“Natoa wito kwa mawakala wetu kuendelea kushiriki katika kampeni hii na kufikisha malengo ya kuingia kwenye droo kwa kuwa imeandaliwa kwa ajili yao kwa ajili ya kuwawezesha na tunachosubiri ni kuona magari haya yatachukuliwa na wasambazaji kutoka kanda gani.

Kavishe alisema lengo kubwa la kampeni hii ambayo imesifiwa na wasambazaji wa vinywaji vya kampuni hiyo kutokana na kuwa na zawadi kubwa ni kuwainua kibiashara wasambazaji wa bidhaa za kampuni ikiwemo kuwapatia motisha kutokana na kushirikiana na kampuni kibiashara.

“TBL Group tunazo Programu mbalimbali za kuwezesha wateja wetu na ndio maana tumekuwa tukiandaa promosheni mbalimbali zenye lengo la kuwainua kimaisha ikiwemo kuwapatia mafunzo mbalimbali ya mbinu za kufanya biashara kwa mafanikio”.Alisema

Alisema kampeni itadumu kwa kipindi cha wiki 12 na wasambazaji wanaoshiriki wamewekewa viwango vya mauzo; na washiriki wote watakaofikia vigezo wataingia kwenye droo kubwa ya kupata mshindi mwezi Oktoba mwaka huu . “Tunaamini kabisa kampeni hii itaongeza ufanisi kwa wasambazaji wetu nao watoongezea chachu ya manunuzi ya bidhaa zetu”.Alisema.

Baadhi ya mawakala wamepongeza jitihada za kampuni kutenga zawadi kubwa za promosheni ambazo zitawawezesha washindi kurahisisha biashara zao badala ya zawadi ndogondogo  zisizoweza kumwinua kimaisha mshiriki.

Mmoja wa wauzaji wa bidhaa ya Konyagi kanda ya Kusini aliyejitambulisha kama Saimon Haule amesema kuwa japo sio mawakala wote watapata malori lakini watakaobahatika kushinda watakuwa wamepata zawadi ya uhakika na inayofanikisha biashara kukua. “Kampeni hii ya Konyagi ni kubwa cha muhimu ni kukidhi vigezo vya kuingia kwenye droo ya kumpata mshindi “.Alisema
Posted by MROKI On Thursday, August 11, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo