Nafasi Ya Matangazo

September 09, 2015

Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kati – Magharibi, Humphrey Mmbando akitoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala muhimu yaliyojitokeza wakati wa semina kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji wa leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa nchi nzima kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini. Wengine pichani (mstari wa mbele) ni baadhi ya Maofisa kutoka Ofisi ya Madini – Shinyanga.

Baadhi ya akina mama ambao ni wachimbaji wadogo wa madini mkoani Shinyanga wakiwa katika semina kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Kutoka Kushoto ni Amina Mtoro, Hafsa Issa, Halima Mohamed, Khadija Salum na Nusura Juma. Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchi nzima.



Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akitoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao wakati akiwasilisha mada kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP) kwa wachimbaji madini wadogo, wakati wa Semina maalumu iliyofanyika leo Septemba 9, 2015 mjini Shinyanga.

Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni, Wizara ya Nishati na Madini, Juma Masoud akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa wakati wa Semina kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo imefanyika leo Septemba 9, 2015 mjini Shinyanga ikiwa ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa na Wizara husika kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini kote.



Baadhi ya Vijana ambao ni wamiliki wa leseni za madini mkoani Shinyanga wakiwa katika Semina kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining cadaster Transactional Portal – OMCTP) yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini nchi nzima. Kutoka Kushoto ni Juma Swalehe, Steven Ngonyani, Salum Abdillah na Meshack Daniel. Mafunzo hayo kwa mkoa wa Shinyanga, yamefanyika leo Septemba 9, 2015.



Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Erick Mkoma, akisaini Kitabu cha Wageni katika Ofisi ya Madini Kanda ya kati Magharibi iliyoko mjini Shinyanga. Wengine pichani ni Juma Masoud (katikati) na Mhandisi Nuru Shabani (Kulia). Wataalam hawa leo Septemba 9, 2015 wametoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini mkoani Shinyanga kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandano (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP).
Posted by MROKI On Wednesday, September 09, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo