Nafasi Ya Matangazo

July 14, 2015

 Mkurugezi Mkuu wa Kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary (mwenye kanzu) akimwonesha Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Mha. Happiness Mgalula sindano iliyochambuliwa na mashine ya kuchambua uchafu kwenye alizeti inayoletwa kiwandani hapo. Anayetazama ni Mha. Omari Athumani, Mchambuzi Sera Mkuu, Tume ya Mipango 

Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary akiwaonesha wajumbe wa timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango machine ya kukamua mafuta ya alizeti (haionekani pichani)
Baadhi ya wafanyakazi wa kitengo cha kupakia mafuta kwenye madumu wakiendelea kupakia mafuta ya ujazo wa lita tano kiwandani hapo

Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha kukamua mafuta cha Singida Fresh Oil Mills Khalid Omary akionesha dumu la mafuta yanayozalishwa na kiwanda chake tofauti na yale ambayo ni feki ambapo watu wasio waaminifu wanatumia nembo ya kiwanda hicho 

Baadhi ya wakulima wanaoleta alizeti kiwandani hapo wakisubiri huduma ya kukamua mafuta kiwandani hapo. Takribani asilimia 80 ya wakulima wanaoleta alizeti kiwandani hapo wanataka kukamua mafuta ambapo kiwanda kinawalipisha gharama ya kukamua lakini wao wanaondoka na mafuta yao. Jumla ya wakulima 500 wanaleta alizeti kiwandani hapo.
Posted by MROKI On Tuesday, July 14, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo