Nafasi Ya Matangazo

July 14, 2015

 BARAZA la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NDC), na Benki ya Posta Tanzania, (TPB), wamesaini makubaliano ya ushirikiano wa kuwawezesha wanachama wa VCOBA nchini. Benki TPB na NDC kutiliana saini makubaliano ya ushirikiano kati ya baraza na benki hiyo, katika kuwawezwesha wana VICOBA kiuchumi. Hafla hiyo ilifanyika leo Julai 14, 2015. kwenye ukumbi wa wizara ya fedha jijin I Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEC), Beng’ Issa, (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Benjki ya Posta, Sabasaba Moshingi, (wapilia kulia), Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota Likokola, (wapili kushoto), Mwanasheria wa Benki ya Posta Tanzania, Mystica Mapunda Ngongi, (wakwanza kulia), wakiwa wameshikana mikono baada ya benki hiyo kutiliana saini makubaliano ya ushirikiano kati ya baraza na benki hiyo, katika kuwawezwesha wana VICOBA kiuchumi. Hafla hiyo ilifanyika leo Julai 14, 2015. kwenye ukumbi wa wizara ya fedha jijin I Dar es Salaam.
************
Akizungumza wakati wa hafla ya kutiliana saini makubaliano nhayo kwenye ukumbi wa wizara ya fedha jijini Dar es Salaam leo Julai 14, 2015, Katib u Mtendaji wa baraza hilo, Beng’ Issa, alisema, Katika juhudi za kuwawezesha watanzania kiuchumi kupitia upatikanaji wa mitaji na kuendeleza ujasirimali nchini, Serikali kupitia Sheria ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004, ibara ya IV, sehemu ya 16  iliagiza  uanzishwaji wa Mfuko wa Taifa wa Uwezeshaji Mwanachi yaani ‘’Mwananchi Empowerment Fund,”.
“Katika kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa mitaji yenye gharama nafuu kwa wajasiriamali nchini, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi limesaini hati za makubaliano na Benki ya Posta Tanzania katika kusimamia udhamini wa mikopo  yenye masharti nafuu kwa makundi  mbali mbali  ya wajasiriamali nchini yanayokidhi masharti husika.” Alisema Beng’i.
Mfuko huu utakao simamiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ni pamoja na kutoa fursa kwa wananchi katika makundi au mtu mmoja mmoja kupata mitaji ya kuwekeza kwenye miradi ya kiuchumi kupitia mikopo ya moja kwa moja au udhamini (direct lending   or guarantee system).
Ili kutimiza azama hiyo baraza limeamua kushirikiana na benki ya ;posta Tanzania ambayo ina mtandao mpana, kutekeleza azma hiyo ambapo wananchama wa VICOBA, watapata mikopo na mafunzo kutoka benki ya posata. Soma zaidi hapa
Posted by MROKI On Tuesday, July 14, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo