Nafasi Ya Matangazo

February 09, 2015

Bweni lililowaka moto.
Wananchi na  wanafunzi  wa shule ya  sekondari  Idodi  Iringa   wakishiriki  kuzima  moto katika  bweni la  wanafunzi  wa  kike  shuleni  hapo amnbalo lilikuwa  likiwaka  moto  leo  asubuhi.
 *********
MOTO  mkubwa  ambao  chanzo chake  kinatajwa  kuwa  ni  hitirafu  ya  umeme  umeteketeza bweni  la  wasichana  katika  shule  ya  Sekondari  Idodi  wilaya  ya  Iringa  mkoani Iringa .

Tukio hilo  limetokea  muda  wa saa 4  asubuhi  leo wakati  wanafunzi  wakiwa  madarasani  wakiendelea na masomo.

Katika mahojiano na m,tandao wa matukio daima, Kamanda wa jeshi la Zimamoto Mkoani Iringa, Inspekta Kennedy Komba alisema kuwa bweni hilo limeteketea lote na kuunguza mali zilizoko katika bweni hilo na chache kuokolewa na wananchi waliowahi kufika eneo la tukio kusaidia  kuzima moto  huo.

Alisema kuwa chanzo cha moto huo imesababishwa na hitalafu ya umeme na hakuna mwanafunzi yoyote aliyejeruhiwa na moto huo.

“Endapo tungepata taarifa mapema nina amini tungeweza kuokoa vitu vingi zaidi na kuwataka wananchi wasitegemee mtendaji au kiongozi apige simu katika kikosi cha kuzima moto kwani kila mtu ana haki ya kupiga simu 111 katika kitengo cha mawasiliano cha jeshi hilo kuweza kutoa taarifa ya majanga, tumetumia muda mdogo kufika eneo la tukio kutokana  ubora wa gari hivyo nawashukuru sana wananchi kwa taarifa na kuweza kuonyesha ushirikiano katika uzimaji wa moto huo usilete madhara zaidi “ alisema

Akizungumzia hasara iliyosababishwa ni kiasi gani Komba alisema hadi sasa hawajapata tathmini kamili ya mali zilizoteketea ila baada ya kazi kukamilika itafahamika ni thamani ya vitu vilivyoungua na kuwekwa wazi kwa wanachi.
 Agosti 25/ 2009  jumla  ya  wanafunzi 13  walipoteza maisha baada ya  bweni hilo kuteketea kwa  moto na  baadhi  yao  kujeruhiwa kwa ajali  kama  hiyo ya  moto ambayo kwa  kipindi hicho moto  huo ulisababishwa na mshumaa.
Posted by MROKI On Monday, February 09, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo