Nafasi Ya Matangazo

May 14, 2014


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
CLABU ya Ako Labamba ya jijini Dar es Salaam imejitosa kudhamini shindano la Miss Ubungo litakalofanyika mwezi ujao.
Baadhi ya washiriki wa Miss Ubungo 2014 wakiwa katika pozi. 
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja Miradi wa Kampuni ya AKO Group Ltd, Honesty Minde, alisema wameamua kudhami ni shindano hilo ili kusaidia kulifanikisha.

Alisema wameamua kuwasaidia waandaaji wa shindano hilo ili kukuza sanaa ya urembo, wakiamini kuwa ndio dira ya maendeleo kwa Watanzania wote.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika pozi kwenye clabu ya Ako Labamba.
“Tuliamua kuwapa maeneo ya kufanya mazoezi pamoja na huduma nyingine muhimu kwa waandaaji na warembo wao. “Naamini kwa pamoja tutafanikisha kwa vitendo mafanikio makubwa ya Miss Ubungo mwaka huu, ukizingatia kuwa ndio lengo letu,” alisema.

Wadhamini wengine katika shindano hilo ni Sigmark Tanzania, Prima Hair, Smart Bol, Handeni Kwetu Blog, MG Hostel, City Park Hotel, Milladayo.com, Dartalk na Nelson Fashion.

Posted by MROKI On Wednesday, May 14, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo