Mkuu
wa Shule ya Sekondari ya Mbeya iliyopo jijini na Mkoa wa Mbeya, Magreth
Haule, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya walimu, wafanyakazi na
wanafunzi wa shule hiyo kwa maofisa wa kampuni ya Simu ya Airtel mara
baada ya kupokea msaada wa vitabu zaidi ya 200 vya masomo tofauti
tofauti kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne jana. (katikati) ni Ofisa
Masoko wa kampuni ya mtandao wa simu ya Airtel Kanda ya Nyanda za Juu
Kusini, Jonas Mmbaga na Ofisa Mauzo wa kampuni hiyo Mbeya Priscus
Kimario.
Mkuu
wa Shule ya Sekondari ya Mbeya iliyopo jijini na Mkoa wa Mbeya, Magreth
Haule (kushoto) akikabidhiwa msaada wa Vitabu vya masomo tofauti
tofauti jana kutoka kwa Ofisa Masoko wa kampuni ya simu ya Airtel Kanda
ya Nyanda za Juu Kusini, Jonas Mmbaga, (katikati) vitabu hivyo
vilivyotolewa msaada na kampuni hiyo.
*******
Kampuni
ya simu ya Airtel chini ya mradi wa shule yetu imetoa msaada wa vitabu
vyenye thamani ya takriban shilingi milioni 2 kwa shule ya sekondari ya
Mbeya.
Makadhiano
ya vitabu yameshuhudiwa na jumuiya nzima ya Shule yenye zaidi ya watu
takribani 1365 wakiwemo wanafunzi, walimu na wafanyakazi wengine
waliokusanyika kwa shauku ya kupokea vitabu hivyo ikichagizwa na kauli
mbiu ya Airtel Baba lao.
Afisa
Masoko wa kampuni hiyo Kanda ya Kusini, Jonas Mmbaga amesema “lengo la
kutoa msaada huo ni kutekeleza azma ya kuendeleza ushirikiano na jamii
katika Nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ili kukuza taaluma mashuleni.
Chini ya mpango wa shule yetu tumeweza kuzifikia shule mbalimbali nchini
na leo tunayofuraha kutoa msaada wa vitabu kwa shule ya sekondari
mbeya.
Mbaga
alisema Vitabu hivi ni vya masomo ya sayansi vikiwemo vya Hisabati,
Kemia, Fizikia, na Biolojia, kwa ajili ya kidato cha kwanza hadi cha
nne. Na tumeichagua shule ya Sekondari Mbeya ili kuwakilisha shule
nyingine zilizopo mkoani Mbeya.
“Tunaahidi
kuendelea kuzifikia shule nyingi zaidi mkoani hapa na mikoa ya jirani
kupitia mpango wetu maalum wa shule yetu ambao ni endelevu uliodumu
zaidi ya miaka 7 mpaka sasa. Tuaamini kwa kujikita kwenye sekta ya
elimu tunaendeleza ushirikaino wetu na serikali chini ya wizara ya elimu
kusaidia kutatua changamoto zilizopo husasani ya vitabu mashuleni na
kuongeza kiwango cha ufaulu nchini”.aliongoza Mmbaga
Kwa
upande wake Mkuu wa shule ya sekondari ya Mbeya Bi Magreth Haule
alisema” Nawashukuru sana Airtel kwa msaada wa vitabu walioutoa shuleni
hapa huu ni uthibitisho kuwa Airtel wapo karibu na jamii hasa katika
kuendeleza sekta ya elimu. Msaada huu ni mchango mkubwa na ni changamoto
kwa wanafunzi na walimu kuongeza juhudi katika kuhakikisha tunakuza
kiwango cha elimu shuleni hapa. Tunaahidi kuvitumia vizuri vitabu hivi
kwa manufaa ya wanafunzi na jamii nzima kwa ujumla
Nao
Wanafunzi Revina Florence, Denis Michael na Happy Mwaisengela kwa
nyakati tofauti na kwa niaba ya wenzao wameipomgeza kampuni ya simu ya
Airtel kwa msaada huo na kwamba vitabu hivyo vitachochea hamasa za
wanafunzi kuongeza bidii katika masomo ili kufikia lengo lililokusudiwa.
Vitabu
hivyo ni mwendelezo wa shughuli za huduma kwa jamii zinazotelewa na
Airtel kupitia mradi maalumu wa Shule yetu unaoziwezesha shule
mbalimbali kutapa vitabu vya ada na kiada, mpaka sasa shule zaidi ya 900
zimeshafaidika na mpango huu
0 comments:
Post a Comment