Nafasi Ya Matangazo

February 12, 2014



Tamasha la mwanamke na akiba, ni tamasha la kwanza na la kipekee kabisa kuwahi kufanyika hapa nchini Tanzania. Tamasha hili lina nia n a dhamira ya kutengenzeza ujuzi na kumuelimisha mwanamke kuhusu kuweka akiba na kujitengenezea fursa mbalimbali.

Tamasha litawaelimisha wanawake namna tofauti za kuweka akiba, na mbinu mbalimbali za kujikimu. Tamasha hili linakusudia kuwaelimisha wanawake umuhimu wa kuweka akiba, mbinu tofauti za kuweka akiba na jinsi ya kukabiliana na changamoto mbalimbali katika kujiwekea akiba.

Akiongea na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo, Mkurugenzi wa Angels Moment, Bi Pamela Mathayo, alisema tamasha hili litahusisha maonesho mbalimbali ya bidhaa za akina mama, na litahusisha mihadhara minne kutoka kwa wataalamu wa masuala ya kibiashara na wajasiriamali. Ni fursa mojawapo kwa watakaohudhuria kujipatia utaalamu na kupanua wigo wao kibiashara, aliongezea. Tamasha hili litafanyika siku ya tarehe 19 mpaka 21 ya mwezi wa pili, katika ukumbi wa Dar live-Mbagala, Dar es salaam.

“Mgeni wa heshima anatrajiwa kuwa mke wa makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Mama Aisha Bilal. Tamasha hili litahudhuriwa na waonesha bidhaa wapatoa 50, na zaidi ya watu 5000 wanatarajiwa kuhudhuria tamasha hili, aliongezea Bi Pamela Mathayo.

 Naye Meneja mawasiliano wa Angel Moments, waandaji wa tamasha hilo alisema nia ya tamasha hilo ni Kuboresha kasumba ya kujiwekea akiba, hususan ikwa akina mama, na mbinu mbalimbali za kujiongezea kipatoKuongeza idadi ya wanawake katika mifuko mbalimbali ya akiba Kuwafunza wanawake namna ya kujinufaisha na akiba zao, ama kwa muda mfupi , wa kati na muda mrefu Kuwatoa wanawake katika utegemezi na umaskini kwa kuongeza kipato chao Kujifunza kutoka kwa wanawake wengine ambao wamefanikiwa kutokana na kuweka akiba Kungamua na kutengeneza midahalo ambayo itakua ni chachu ya kuboresha uwekaji na uelimishaji wa kuweka akiba kwa mwanamke Kuwaleta pamoja wadau mbalimmbali ili kusaidia kumkomboa mwanamke, hususani katika suala la kuweka akiba Kutoa fursa kwa wafadhili kujitangaza, kutangaza bidhaa zao, na pia kuwafikia watanzania wengi zaidi.

Tamasha hili limedhaminiwa na Said Salim Bakhressa, NSSF, PPF, SSRA, UTT, National Housing Corporporation (NHC), Montage Limited, CRDB,  Ashton Media
Posted by MROKI On Wednesday, February 12, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo