Nafasi Ya Matangazo

December 07, 2012

Waziri wa Jinsia wa Rwanda, Aloysia Inyumba amefariki, jana baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akiwa bado kijana aliyehitimu kutoka Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, Inyumba alishiriki kikamilifu katika kuasisi chama cha Rwanda Patriotic Front (RPF) mnamo mwaka 1987.

Katika Harakati hizo akawa Kamishna wa Fedha wakati wa mapinduzi ya RPF ambapo alipata uwezo wa kuweza kukusanya na kutunza fedha kwaajili ya Mfuko huo wa Mageuzi.

Inyumba alijizolea umaarufu mkubwa wakati wa kufanya manunuzi ya sare mpya za jeshi la RPF kutoka Ujerumani Mshariki maarufu kama Mukotanyi .

Inyumba alishika wadhifa huo wa Waziri wa Jinsia tangu baada ya vita 1994, na baade kuwa mbunge kwa miaka 8 na kurudi tena katika baraza la Mawaziri.
Wakati wa kuzanzishwa kwa RPF akiwa pamoja na marehemu Meja Peter Bayingana , alifanya kazi kubwa ya kumshawishi Kanali Alex Kanyarengwe kujiunga nao.

Marehemu Inyumba atakumbukwa kuwa alisafiri hadi Tanzania kufuta Kanyarengwe ambaye baade alikuja kuwa Mwenyekiti wa RPF, kufutia kifo cha Generali Fred Rwigyema.

Hadi mauti yanamfika , Inyumba alikuwa ni mtu muhimu sana kwa Rais Paul Kagame kwani alikuwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa katika siasa.

Kifo cha Inyumba si pigo tu kwa RPF lakini pia ni pigo kwa wana Rwanda wote.

Inyumba alikuwa akiheshimiwa sana  katika uwanja wa siasa hata kwa wale walio poteza imani zao kwa Kagame kama vile Generali Faustin Kayumba Nyamwasa.
Posted by MROKI On Friday, December 07, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo