Nafasi Ya Matangazo

October 30, 2011

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kulia) akiangalia aina mbalimbali za vito vya madini katika jengo la Perth Council House Perth Australia Okt.29,2011 wakiwa katika ziara ya wake wa viongozi waliohudhuria mkutano mkuu wa nchi wanachama wa jumuia ya madola pamoja na Mwenyeji wake Patner wa waziri mkuu wa Australia Bw, Tim Mathieson (mwenye suti) katika ziara hiyo wamejifunza umuhimu wa sekta ya nishati na madini kwa nchi ya Australia.
Mama Salma Kikwete akionyeshwa vazi la asili-na mhifadhi olman walley- Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kushoto) akiangalia pamoja na kupatiwa historia mbalimbali kuhusu aina ya vazi liliotengenezwa kwa ngozi ya mnyama wa asili ya Kangaroo . kutoka kwa mhifadhi Olman Walley walipotembelea bustani ya mimea ya asili pamoja na wanyama katika eneo maalumu la King's Park Austaralia.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kushoto) akiwa pamoja na baaadhi ya wake wa viongozi wawaliohudhuria mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa jumuia ya madola wakiangalia sanaa ya asili wa watu wa nchi ya Australia oktoba 29. 2011 inayopigwa na Olman Walley walipofanya ziara ya kuangalia aina mbalimbali ya wanyama ,bustani ya hifandi ya miti ya asili kwenye eneo la Caversham Wildlife Park .Pichani wa pili kulia ni Mke wa Rais wa Nigeria Patience Jonathan.
Picha ya Mhifadhi Olman Walley ikiwa ni kielelezo cha kuonyesha jinsi ya utamaduni wa vazi la zamani la asili ya watu wa Australia . Jamani utamaduni tusidharau utamaduni wetu. unamouna alivyopendeza?
Posted by MROKI On Sunday, October 30, 2011 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo