Nafasi Ya Matangazo

March 20, 2023

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange (watatu kulia) akipokea sehemu ya msaada wa vitanda 10 kwa ajili ya kituo cha afya cha Levolosi, kutoka kwa Kaimu Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Emmanuel Kafui (watatu kushoto) uliotolewa na Benki ya CRDB kwa uratibu wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mrisho Gambo (wanne kulia). Msaada huo unaelekezwa moja kwa moja katika Wadi ya Wanawake katika kituo hicho cha Levolosi kilichopo jijini Arusha ili kupunbuza adha iliyokuwepo hapo awali ya kulala wawili katika  kitanda kimoja. Msaada huo unathamani ya shilingi Milioni sita.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Hargeney Chitukuro.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada wa vitanda 10 kwa ajili ya kituo cha afya cha Levolosi, kilichopo jijini Arusha, uliotolewa na Benki ya CRDB, Vitanda hivyo vinathamani ya shilingi milioni sita.

Posted by MROKI On Monday, March 20, 2023 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo