Nafasi Ya Matangazo

August 01, 2012

 Jiji la Arusha ni miongoni mwa majiji makumbwa hapa nchini ambayo yanakabiliwa na foleni kwa nyakati za asubuhi na jioni jambo ambalo limekuwa likisababisha kero kubwa kwa watumiaji mbalimbali wa barabara hizo.Miongoni mwa barabara ambayo inaathirika zaidi ni ile ya Old Moshi.
 Aidha barabara ambayo inaongoza kwa kuwa na foleni kubwa ni ile ya Dodoma ambayo huwa na magari mengi wakati wa kwenda na kurudi majira ya asubuhi na jioni.
lakini tatizo kubwa linaloelezwa na watumiaji wa baraba hizo kuwa ni miundombinu hafufu na barabara zinazoingia na kutoka katikati ya mji kuwa ni chache. Wadau mbalimbali wamependekeza kuanza mapema mchakato wa kluzifanyia upanuzi barabara muhimu jijini humo hasa ukizangatia mji huo unavyo panuka huku shughuli nyingi za utalii zikiongezeka sambamba na maofisi ya kimataifa hivyo idadi ya watu pamoja na watumiaji wa magari kuongezeka siku hadi siku.
Posted by MROKI On Wednesday, August 01, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo