Kuna taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya
kijamii ikisema "Ndugu zangu mimi ni Aisha Madoga tumezingilwa na watu
wenye Bunduki hapa UDOM......"
Taarifa sahihi ni kwamba walinzi wanaolinda eneo la
Chuo hicho waliwazuia watu walioingia usiku chuoni hapo wasiendelee kuzunguka
eneo la chuo huku wakiwahamasisha
Wanafunzi wawaunge mkono na washiriki katika maandamano wanayoyaandaa Jijini
Dodoma.
Aidha, Mkuu wa Kituo cha Polisi cha eneo hilo
aliwasiliana na mmoja wa kiongozi wa watu hao na kilichoonekana ni kuzuiwa
kuendelea kuzunguka ndani ya chuo isivyo halali nyakati za usiku.
Hivyo
waliowazuia ni askari kwa kuzingatia sheria kwa sababu walichokuwa wanafanya
chuoni hapo hawakuwa na uhalali wa kufanya hivyo tena nyakati za usiku.
Jeshi la Polisi lingependa kuwaonya watu wa aina
hii wanaofanya vitendo vya kihalifu kama hivyo na kama haitoshi wanatunga
ujumbe wa uwongo na kuusambaza kwenye mitandao kwa lengo la kuwadanganya na
kupata huruma ya wananchi ili kuhalalisha vitendo ambavyo havina Baraka za
kisheria.
Watambue kuwa hatua za
kisheria lazima zitachukuliwa dhidi yao endapo wataendelea na tabia hizo.
0 comments:
Post a Comment