Nafasi Ya Matangazo

March 19, 2024



Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu,  Utamaduni na Michezo chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Husna Sekiboko (Mb) imeielekeza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo iongeze bajeti ya Mfuko wa Utamaduni na Sanaa ili Mfuko huo uweze kukopesha Wasanii wengi zaidi.
 
Mhe. Husna ametoa maelekezo hayo Machi 18, 2024 Jijini Dar es Salaam baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa Mfuko huo ambapo amesema Mfuko huo unapaswa kuwa na Sheria, hivyo wizara ianze mchakato wa kuhakikisha sheria hiyo inapatikana.
 
"Dhamira ya Mfuko huu ni kuendeleza Wasanii, hakikisheni fedha wanazokopa ni kwa ajili ya kufanya kazi ya sanaa na si vinginevyo, Benki ambazo zinatoa mikopo hii hakikisheni mnatoa masharti yanayofanana na kazi wanazofanya Wasanii na Wizara pia endeleeni kuweka mazingira bora ya upatikanaji wa soko la kazi hizo", amesisitiza Mhe. Husna.
 
Awali Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma amesema wizara imefanikiwa kusimamia mfuko huo ili utekeleze majukumu yake kwa kuendelea kuongeza vyanzo vipya vya mapato tofauti na ruzuku ya Serikali pekee kwa kuwa wahitaji ni wengi.
 
Ameongeza kuwa, tangu kuanza kwa utekekezaji wa kukusanya kodi kwenye vifaa vya kuhifadhia kazi za sanaa ambayo ni asilimia 1.5, hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 465 zimekusanywa ambapo asilimia 10 ya fedha hizo zinaenda kwenye Mfuko huo kwa lengo la kuongeza vifaa vingine ambayo vinatumika kuhifadhia kazi hizo.
Posted by MROKI On Tuesday, March 19, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo