Nafasi Ya Matangazo

September 28, 2023


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Chemba ya Wafanyabiashara, Wenye  Viwanda na Kilimo Tanzania  (TCCIA) jana imewahimiza  wafanyabiashara na  wenye viwanda nchini  kuchangamkia  fursa ndani ya Soko Huru la Afrika (African Continental Free Trade Area (AFCFTA) kwa kuwa sasa TCCIA inatoa vyeti vya uasili ambavyo vinaeleza bidhaa za Tanzania zinakokwenda na kumpunguzia ushuru mfanyabiashara.
 
Akizungumza kwenye mafunzo hayo ya siku moja yaliyoandaliwa na TCCIA, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA, Bi Mwanahamisi Hussein, amewahimiza wafanyabiashara na wenye viwanda wa Tanzania kujinufaisha na fursa zilizomo katika soko huru la Afrika ili Tanzania ipate fedha ya kigeni na kukuza uchumi wa taifa.
 
“ Tunatoa mafunzo haya kuhakikisha wafanyabiashara wa Tanzania wananufaika na fursa kwenye soko huru la aflrika na kufahamu faida zake. Faida moja wapo ya kutumia siko hilo  kuongeza wigo wa masoko ya bidhaa za Tanzania, kukuza viwanda vyetu na kuongeza ajira,” alieleza Bi Mwanahamisi na kuongeza kwamba TCCIA ina wajibu wa kuunga mkono juhudi ya serikali ya awamu ya sita ambayo inatoka kipaumbele kwa shughuli za sekta binafasi.
 
Alisema kwamba  Tanzania ni kati ya nchi ambazo zimeingia katika mikataba mizuri ya masoko mbalimbali duniani ikiwemo soko huru la Afrika, na kufafanua kwamba TCCIA inataendelea kutumia fursa ya mafunzo kama hayo kuwafikishia taarifa  wafanyabiashara na kuhakikisha wanazalisha bidhaa  zennye ushindani katika soko huru la Afrika.  

“Tunataka Tanzania ifanye biashara.  Hatutaki  Tanzania iwe soko la bidhaa za nchi nyingine tu. Tunataka tupeleke bidhaa zetu nchi nyingine hasa kwa kutumia siko hili la Afrika, maana tuna biashara zinazotakiwa nje ya Tanzania,” alieleza Bi Mwanahamisi.
 
Mshiriki wa mafunzo hayo, Bi Maria A. Mtui amesifu  mafunzo kwani yamewawezesha kupata welewa zaidi juu ya fursa katika soko hilo , na kujua aina ya nyaraka zinazohusiana biashara katika soko hilo.
 
Bw. Joshua Zuberi amesema mafunzo hayo yamewafahamisha kwa uwazi zaidi namna wafanyabiashara wa Tanzania watakavyotumia fursa za soko hilo na kwamba wataweza kufanya biashara katika masoko makubwa pasipo kutozwa ushuru.  

“Hata wateja wetu watafurahia kufanyabiashara pasipo kutozwa ushuru.  Hili ni jambo zuri katika kufanya biashara,” alisema.
Posted by MROKI On Thursday, September 28, 2023 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo