Nafasi Ya Matangazo

November 19, 2019

Shule ya msingi vilima vitatu, ambayo amekarabati madarasa, ujenzi wa nyumba za walimu, vyoo na kuweka madawati na vitatu ukarabati ambao umefanywa na Taasisi ya Chemchem Association na amekabidhi umegharimu zaidi ya sh 54.2 milioni.
 Mkuu wa wilaya Babati Elizabeth Kitundu akiwa na watendaji wa taasisi ya chemchem na viongozi wa kijiji cha vilima vitatu wakiwa wanatembelea shule ya msingi Vilima vitatu.
Mwandishi wetu,Babati. 
Mwekezaji katika sekta ya Utalii, wilayani Babati mkoa wa Manyara,Taasisi ya chemchem association, amekabidhi shule ya msingi vilima vitatu, ambayo amekarabati madarasa, ujenzi wa nyumba za walimu, vyoo na kuweka madawati na vitatu ukarabati ambao umegharimu zaidi ya sh 54.2 milioni.

Shule ya msingi vilima vitatu ilikuwa ikikabiliwa na uhaba wa madarasa, vyoo, nyumba na walimu na madawati na kusababisha wanafunzi kusoma chini.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi shule hiyo, mkuu wa wilaya babati Elizabeth Kitundu ,kukarabatiwa na kujengewa majengo mapya katika shule hiyo, ni mchango wa mwekezaji huyo katika kuunga mkono jitihada za serikali kuboresha elimu.

Kitundu ameipongeza taasisi hiyo kwa kuendelea kushirikiana na serikali katika sekta ya elimu pia amewataka waendelee kushirikiana na wananchi wa Kijiji hicho ambacho kampuni hiyo, imewekeza katika utalii wa picha na hoteli.

" Maendeleo yanakuja kwa kuletwa na elimu hivyo ninaomba muendelee kushirikiana ili kuleta maendeleo katika Kijiji hiki ili kutatua changamoto zilizopo hapa". alisema

Alisema hata hivyo, kampuni hiyo ambayo imewekeza ndani ya hifadhi ya jamii ya Burunge, inahimiza wananchi kutunza wanyamapori na kuacha vitendo vya ujangili lakini pia kutunza na mazingira ili watalii waendelee kufika katika maeneo yao na hivyo kupatikana fedha za misaada.

“kama tukiendelea kutoa ushirikiano kwa mwekezaji huyo, kuacha kuharibu mazingira watalii watakuja zaidi na hivyo wao wanafaidika na sisi wananchi na serikali tutaendelea kunufaika”alisema

Afisa maendeleo ya jamii ya taasisi ya Chemchem ,Walter Pallangyo alisema pallango alisema wataendelea kushirikiana vizuri na wananchi katika kusaidiana elimu Bora pamoja na mahitaji mengine .

Pallango aliwaomba wananchi kuendelea kutunza mazingira na uhifadhi wa wananyama kwani mazingira yanapokuwa mazuri tunapata wageni wengi maana fedha hizo zinatokana hifadhi hiyo ili wazidi kufanya maendeleo

Afisa mtendaji wa Kijiji Husna Shabani amesema kuwa taasisi hiyo inatijitoa kwa hali na Mali katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo , ikiwa marekebisho yaliyofanyika ni vyumba vya madarasa nane ,ofisi za walimu mbili, nyumba za walimu tatu,ujenzi wa vyoo vya matundu manne pamoja na madawati Mia moja 100 vyote hivyo vikiwa na thamani ya sh 54.2 milioni.

Husna aliendelea kusema hata hivyo taasisi hiyo imeweza kuwaletea vitabu vya kufundishia vyenye gharama ya sh 325,700 hivyo shule hiyo imekuwa na mafanikio katika taaluma Kila mwaka mwaka.

“mwaka ,2017 walifanya mtihani 23 na walifaulu wote pia 2019 walifanya mtihani 20 na walifaulu 19 kwa wastani alama ya 150 kupitia maboresho hayo hali ya taaluma itaboreka na utoro unapungua k na matunda ya ukarabati huo umetokana na hifadhi ya jamii burunge”alisema

Akizungumza mkuu wa shule vilima vitatu Denis Mtui alishukuru chemchem kwa kuweza kukarabati shule hiyo maana awali shule hiyo ilikuwa chakavu Sana katika sekta zote tofauti na Sasa shule hiyo inatia hamasa ya kuonekana shule Bora kimuonekano na kielimu pia.

Mtui alisema aliahidi watatunza shule hiyo na kuendelea kukarabati inapopata shida pia anaomba wananchi kuwa naushirikiano mzuri katika kuleta maendeleo yaliyonatija katika jamii ikiwepo kuacha matukio ya kuvamia maeneo ya mwekezaji kuingiza mifugo.
Posted by MROKI On Tuesday, November 19, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo