Nafasi Ya Matangazo

August 30, 2018

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kulia) na Kamishna Jerenali wa Zimamoto, Thobias Andengenye wakisikiliza maelezo kutoka kwa ofisa Mwamdamizi wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mabel Masasi juu ya huduma za anuani za makazi zinavyoweza kusaidia utoaji haraka wa huduma za zima moto na uokoaji nchuni. Waziri Lugola alikuwa akitembelea mabanda ya maonesho ya wiki ya Zimamoto Nchini, iliyozinduliwa Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni miongoni mwa taasisi za serikali zilizoshiriki katika maonesho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji kitaifa ambayo inafanyika jijini Dodoma kwa mara ya kwanza nchini.

Lengo kuu la maadhimisho hayo ni kutoa elimu juu ya namna bora ya kuepuka majanga ya moto na kuwawezesha wananchi kuzifahamu vyema shughuli nyiongi zinazofanywa na jeshi hilo ambazo si tu kuzima moto kama inavyofahamika na wananchi wengi lakini ni pamoja na kusaidia katika majanga mbalimbali na ajali.

TCRA kama mdau mkubwa wa zimamoto mbali na kusaidia katika mawasiliano baina ya wananchi na Jeshi la Zimamoto kuwa rahisi na ya bure kwa mujibu wa sheria lakini pia kupitia mradi wao wa anuani za makazi unasaidia Jeshi hilo na wananchi kuweza kufikiwa kirahisi.

Ofisa Mwandamizi Mkuu wa Mawasiliano, Mabekl Masasi alimwambia Waziri Kangi lugola kuwa kupitia anuania za makazi zimeweza kurahisisha jeshi hilo kufika katika maeneo mengi kirahisi kwa kutaja jina la mtaa na namba ya nyumba la eneo husika. 
 Waziri wa Mambi ya Ndani, Kangi Lugola akiuliza jambo katika banda hilo la TCRA 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kulia) na Kamishna Jerenali wa Zimamoto, Thobias Ndengenye wakisikiliza maelezo kutoka kwa maofisa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) juu ya huduma za anuani za makazi zinavyoweza kusaidia utoaji haraka wa huduma za zima moto na uokoaji nchuni. Waziri Lugola alikuwa akitembelea mabanda ya maonesho ya Siku ya Zimamoto Nchini, Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma jana.
Wananchi na maofisa mbalimbali wa Jeshi la Zimamoto wakiwa katika Banda la TCRA kupata vipeperushi na maelezo mbalimbali ya kazi za taasisi hiyo.
Posted by MROKI On Thursday, August 30, 2018 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo