Nafasi Ya Matangazo

August 03, 2016

 Warembo wanaoshiriki shindano la miss kanda ya kaskazini kutoka katika mikoa ya Arusha,Manyara,Tanga na Kilimanjaro wakiwa nje ya hotel ya Clous view sehemu ambayo wanafanyia mazoezi kwa ajili ya shindano hilo linalofanyika july 6 katika viwanja vya ukumbi wa Triple A FM.

Warembo wanaoshiriki shindano la miss kanda ya kaskazini kutoka katika mikoa ya Arusha,Manyara,Tanga na Kilimanjaro wakiwa nje ya hotel ya Clous view sehemu ambayo wanafanyia mazoezi kwa ajili ya shindano hilo linalofanyika july 6 katika viwanja vya ukumbi wa Triple A FM.

 

Na Woinde Shizza,Arusha
Jamii imetakiwa kuwapa ushirikiano wa kutosha wasichana wanaoshiriki  mashindano ya urembo kwani mashindano hayo ni kazi kama vile kazi zingine.

Hayo yamebainishwa na baadhi  ya warembo wanaoshiriki shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya Kaskazini (Miss Kanda ya kaskazini 2016)wakati walipokuwa wakiongea kwa nyakati tofauti na mwanandisi wa habari hizi katika kambi yao kujiandaa na shindano litakalo fanyika Jumamosi July 6 katika ukumbi wa Triple A uliopo jijini Arusha

MMoja wa washiriki hao aliyejitambulisha kwa jina la Mariamu Mohmed (18) Mshiriki kutoka mkoa wa Manyara alisema kuwa  wazazi wengi hususa ni   ndugu wamekuwa wakichukulia shindano hili kama ni sehemu ya uhuni kitu ambacho sio cha kweli

Alibainisha kuwa shindano hili ni zuri na linatoa ajira kwa vijana wengi na mbali na ajira pia linasaidia vijana wengi ambao ni wasichana kujiajiri wenyewe na wengine kuajiriwa katika sehemu mbalimbali.

Kwa upande wake mshiriki kutoka mkoani Tanga Rukaiya Hassan (20) alisema kuwa kuingia katika urembo sio uhuni wala umalaya kwani ,mtu kuwa na tabia chafu kama izi ni hulka yake mwenyewe na sio mashindano haya ndio yanasababisha mshiriki au mshindi kuwa muhuni

Aidha mshiriki kutoka mkoani Arusha Maurine Ayubu (20) alisema kuwa baadhi ya ndugu wa karibu wamekua wakiwakatisha tamaa washiriki wengine wakiwatenga kutokana na kile wanachodai kuwa ndugu aliyeshiriki shindano hili ni malaya kitu ambacho sio cha kweli na kinawakatisha tamaa warembo wengi ambao walikuwa na ndoto ya kushiriki mashindano hayo.

"unajua mimi naona kila mtu na tabia yake ambayo anayo lakini swala la kusema kuwa kushiriki shindano hili ni umalaya sio la kweli nanaomba ndugu a ambao wananduguzao wanashiriki mashindano ya umiss wawape ushirikiano wa kutosha kwani hii ni kazi kama kazi zingine"alisema mshiriki kutoka mkoani Kilimanjaro Navia Samwel.

Aidha pia aliongeza kuwa kwa upande wake anaamini kabisa atashinda katika kinyaganyiro hicho kwani anajiamini na aliwasihi wenzake iwapo itatokea mtuakitolewa nje asibaatike kuingia katika hatua yatano bora asikate tamaa kwani anaweza pia kushiriki katika mambo mengine ikiwa ni pamoja na uwana mitindo.

Kwa upande wake muaandaaji wa shindano hilo mkurugenzi wa mwandago ivestiment Faustine Mwandago alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yameshakamilika wanasubiri tu siku ya tukio ifike kwani warembo wamepikwa wakapikia vya kutosha .
Posted by MROKI On Wednesday, August 03, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo