Nafasi Ya Matangazo

March 11, 2016

Golikipa mahili wa Mbeya City Fc, Juma K Juma  amerejea kikosini kutoa mapumziko ya majuma mawili aliyopewa na kocha  Kinnah Phiri kufuatia  mkewe Bi Nasra Nassor kujifungua watoto mapacha hivi karibuni.

Akizungumza na mbeyacityfc.com  muda mfupi uliopita Kaseja amesema kuwa amefurahi kusafiri na hatimaye kurudi salama kwenye timu yake huku pia akitoa shukurani zake za dhati wa wale wote ambao wamekuwa karibu nae yeye kama mchezaji na pia familia yake tangu alipojiunga na City.

“Nashukuru mungu nimefika hapa salama baada ya safari yangu, pia namshukuru kwa kile alichonijaalia, nimerudi kikosini nikiwa na ari kubwa zaidi  ili kuituikia timu yangu kwa nguvu zote  katika kutafuta mafanikio hasa kwenye kipindi hiki  ambacho ligi inaelekea mwishoni, hakika tunapita kwenye kipindi kigumu lakini  umoja wetu utatufanya kuvuka hapa” alisema.


Akiendelea zaidi Kaseja  aliyewahi kucheza kwa mafanikio kwenye timu za Moro United, Simba, na Yanga aliweka wazi kuwa anaimani kuwa na kocha Kinnah Phiri kuwa ataijenga upya City na kuifanya kuwa timu itakayotisha zaidi kwenye msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Posted by MROKI On Friday, March 11, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo