Nafasi Ya Matangazo

November 09, 2015

Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa Kampuni ya Total Tanzania,Marsha Kilewo, akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kutangaza kuzinduliwa kwa shindano la “Startupper of the year  by Total” ambalo litashirikisha vijana wenye mawazo ya kibiashara na kuweza kushinda hadi sh milioni 35.

KAMPUNI ya Total ya Tanzania, yazindua  Shindano la Total  «Startupper of the year  by Total», lililobuniwa na kundi la Makampuni ya Total litakaloshirikisha nchi 34 za Afrika kwa wakati  mmoja. Shindano hilo  linalenga katika kutambua, kuzawadia na kuwezesha utekelezaji wa miradi bora ya biashara ya ujasiliamali inayoanza au iliyobuniwa chini ya miaka miwili kwa ajili ya maendeleo ya jamii na taifa.

Washindi wa miradi bora watapewa tuzo ya « Startupper of the year 2016 by Total » itakayoambatana na  fedha taslimu itakayotumika kama mtaji wa kuendeleza, na kusimamia uendeshaji wa miradi hiyo.

Shidano hili ni bure kwa  raia wote wa Watanzania wenye umri kati ya miaka kumi na nane( (18) hadi miaka thelathini na tano (35).

Fomu za maombi zimeanza kutolewa kuanzia tarehe 1 Novemba 2015 saa 2:00 asubuhi kwenye tovuti: http://startupper.total.com/.  Shindano litakuwa wazi hadi Januari 31, 2016 saa 5:00 asubuhi ambapo ndio mwisho wa kurejesha fomu.

Jopo la Majaji linalohusisha  wataalamu wa biashara, litachagua miradi kumi  bora nchini Tanzania itakayoingia fainali kwa kuzingatia vigezo vya ubunifu, uhalisia na uwezo wa mradi katika kuleta maendeleo na kuboresha hali ya maisha ya jamii kubwa ya Watanzania.

Orodha ya washindi watakaoingia fainali itachapishwa tarehe 28, Februari, 2016 katika tovuti ile ile walipochukulia fomu za kugombea.

Kuanzia tarehe 15 Machi, 2016, Washindi hao kumi, wataingia katika mchuano wa fainali  kutafuta tatu bora ambapo washindi watawajibika kuitetea miradi yao  mbele ya jopo la majaji ili kupata miradi mitatu bora  ambapo mshindi wa jumla atatangazwa na kupewa zawadi katika hafla maalum ya utoaji wa tuzo.

 Sheria, taratibu, kanuni na vigezo vya shindano  hili zinapatikana bure kwenye tovuti ya (http://startupper.total.com/).

Shindano la « Startupper of the year by Total » ni juhudi za Kampuni ya kimataifa ya Total katika kuhamasisha  maendeleo ya kiuchumi na kijamii ili  kusaidia nchi zote  duniani ambako kampuni ya Total ipo. Shindano hili ni hatua madhubuti yenye lengo la kuvumbua ubunifu wa  miradi mbalimbali ya maendeleo yenye lengo la kuchangia uanzishwaji wa viwanda vidogo vitakavyotoa ajira na kuchangia maendeleo ya jamii na ya nchi za bara la Afrika kwa ujumla.

Shindano hili linalenga kuibua miradi mipya, iliyotokana na wananchi wenyewe ambayo inaendana na malengo ya jumla ya uwepo wa kampuni ya Total.
Posted by MROKI On Monday, November 09, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo