Nafasi Ya Matangazo

January 06, 2014

Mume wa marehemu Dullah na mdogo wa marehemu Ngalu Buzohera wakiwa kwenye harambee ya kuchangisha fedha za kusaidia kusafirisha mwili wa mpendwa wetu marehemu Zainab Buzohera aliyefariki Jumamosi Jan 4, 2014 saa 2 usiku (8pm ET) WanaDMV walijumuika katika harambee iliyofanyika Bladensburg, Maryland na kuchangisha $22,938 kiasi kilichokuwa kinatakiwa ni $15,000 hii inamaanisha wanaDMV wanapoamua hufanya kweli shukurani kwa wote walioshiriki harambee hii kwa njia moja au nyingine lengo ni kufanikisha na Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema tunashukuru kwa kutuwezesha kufanikiwa harambee hii ya mpendwa wetu Zainab Buzohera. WanaDMV tunawashukuru wenzetu wa New York waliofika kwenye harambee hii kuja kusaidia kutimiza malengo.
Shangazi wa marehemu Jasmine Bernett akiongea kwa niaba ya familia ya Buzohera huku akiwa amejawa na uso wa huzuni aliwashukuru  wote waliofika kwani lengo ni kusaidia kuchangia ili mwili wa marehemu Zainab uweze kusafirishwa nyumbani Tanzania kwa mazishi na matarajio ni kusafirisha siku ya Jumatano na kisomo kinatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne jioni mahali patatangazwa baadae.
Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV Bwn Idd Sandaly akielezea utaratibu wa harambee.
Umati wa Watanzania waliokuja kwenye harambee.
Dada Tuma akielezea utaratibu wa mnada utakavyokuwa.
washika mahesabu wakijiweka sawa kabla ya harambee kuanza.
Watanzania waliofiika kwenye harambee wakitoa michango yao kabla ya harambee haijaanza/
Michango ikiendelea kabla ya harambee.
Timu ya New York ikitoa mchango wake.
Dada Tuma akiendesha mnada.
Watanzania kutoka New York katika picha ya pamoja.
Kutoka kushoto ni Yunus, Bob Miano, Mmiliki wa Vizion One Abdallah Kitwara na Albert Mateso wakiwa kwenye harambee.
Posted by MROKI On Monday, January 06, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo