Nafasi Ya Matangazo

July 18, 2013

 Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga, akionyesha ufunguo wa Bajaji kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji wa Fair Deal auto-dealers, Bw. Anil Dewan kama ishara ya uzinduzi ya promosheni mpya ya “Miliki Biashara Yako” ambayo itawawezesha wateja wake kiuchumi kupitia Bajaji 60 zitakazoshindaniwa kwa muda wa miezi miwili, ambapo kila siku mteja atashinda Bajaji moja.
Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga akionyesha alama ya dole ndani ya Bajaji moja kati ya 60 zitakazoshindaniwa kwa kuongeza salio ya Tsh 1000 tu kwa siku. Mteja wa Tigo anaweza kuongeza salio mara nyingi awezavyo ili kujiongezea nafasi zaidi ya kushinda.

 Meneja Mbunifu wa Ofa za Tigo Suleiman Bushagama (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu promosheni mpya ya “Miliki Biashara Yako.” Pembeni yake ni Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga, Meneja Mauzo Bw. Israel Gadiel  na Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji Bw. Anil Dewan wote kutoka Fair Deal auto dealers wasambazaji wa Bajaj nchini Tanzania.   
Kutoka kulia Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga, katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji, Anil Dewan na Meneja Bidhaa Khalid Saifullah kutoka Fair Deal auto-dealers, wasambazaji wa Bajaj nchini Tanzania.
Moja kati ya Bajaji 60 ambazo zimeanza kushindaniwa leo katika promosheni ya “Miliki Biashara Yako” kutoka Tigo kwa kuongeza salio ya Tsh 1000 tu kwa siku. Mteja wa Tigo anaweza kuongeza salio mara nyingi awezavyo ili kujiongezea nafasi zaidi ya kushinda. Kila Bajaji ina thamani ya Tsh 6,700,000 na Tigo imechukua jukumu la kulipia leseni ya barabara (road license) na bima ya Bajaji tayari kwa mteja atakayeshinda kuja kuichukua na kuanzisha biashara yake mara moja.
Posted by MROKI On Thursday, July 18, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo