Nafasi Ya Matangazo

December 08, 2012

 Rais wa Jamhuri yaKidemokrasia ya Congo( DRC) Joseph Kabila (kushoto) akipokelewa na Waziri wa Uvuvi Dkt. David Mathayo Dec,7,2012 katika uwanja wa ndege  wa kimataifa wa Jk . Nyerere jijini Dar es salaam
 Rais Yoweri Museveni wa Uganda (kulia) akisalimiana na  Makamu wa Rais wa Tanzania Dr. Gharib Bilal  (kushoto)  Dec,7,2012 alipowasili katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK ,Nyerere jijini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa dharura  wa Jumuiya  ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
 Rais wa Mozambique Armando Guebuza (kushoto) akipokelewa na Waziri wa Mambo ya nchi za nnje na ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe (kulia) kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK , Nyerere jjijini Dar es Salaa- Dec,7,2012 kuhudhuria mkutano wa SADC
 Makamu wa Rais wa  Zambia Dkt.Guy Scott (kulia) akifurahia jambo na Waziri wa Uchukuzi Dkt, Harison Mwakyembe (dec,7,2012) wakati wa mapokezi katika uwanja wa ndege wa  kimataifa wa JK Nyerere jijini DSM kwaajili ya kuhudhuria mkutano wa dharura wa SADC.
 Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji Shamim Nyanduga (kulia) akibadilishna mawazo na baadhi ya Mabalozi wenzake na maafisa wanaohudhuria mkutano wa dharura wa SADC,walipokutana katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK, Nyerere Dec, 7, 2012.
 Kikundi cha sanaa ya matarumbeta kinachoongozwa na gwiji wake Mzee Hoza,kikitoa burudani katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JK, Nyerere Dec,7,2012 wakati wa mapogezi ya Marais na wajumbe mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa SADC jijini Dar Es Salaam. (Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO).

Posted by MROKI On Saturday, December 08, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo