Nafasi Ya Matangazo

August 10, 2011


LOLOTE LAWEZEKANA CHINI YA JUA: NIMEFIKA KILELE CHA MLIMA

Jina langu ni Josephat Torner ni mwafrica niliyezaliwa na ulemavu wa ngozi

Nahisi kama maisha yangu yote nimekuwa nikipanda  mlima mrefu. Nimepanda na nimepambana na unyanyapaa na ubaguzi wa kila siku. Nimepigania kuthaminiwa, nimeanguka lakini kila mara nimeinuka, nimepoteza kaka na dada zangu njiani.

Kwa muda wa siku 8 zilizopita nimetembea kwa ajili ya albino wote Africa  ambao kwa namna fulani maishani mwao wamejisikia kama mimi. Nimetembea kwa ajili ya Ukombozi wetu

Kupanda mlima huu mrefu kuliko yote ni kazi ngumu kulikozote nilizowahi kufanya, vita ambayo nisingekubali kushindwa

Kwangu mimi,Leo nimefika kilele cha mlima, Pengine mimi ni mutu wa kwanza albino  kufika kufika kilele kirefu kuliko vyote Africa , natazama pande zote za Bara letu nawaambia Waafrica wote na watu wote kuwa  Albino ni binadamu  anayejiweza kama wengine . Sote ni Waafrica kamwe si wanyama. Hadi kufikia leo yawezekana mumekuwa munaona mwafrica Albino. Natumaini leo hii munaona mutu

Nawaambia Albino wote Africa,tokeni gizani sasa na musiendelee kamwe kuishi kivulini mwa jua, Nimepambana na Mlima, nimepambana na Juan a sote sasa nafahamu twaweza kuwa huru

Tusimame sote kwa pamoja tupigane hii vita , kwani leo sote tunadai haki yetu ya kuishi.

Posted by MROKI On Wednesday, August 10, 2011 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo