Nafasi Ya Matangazo

February 26, 2015

Ama kweli ukistaajabu ya musa hakika utayaona ya firauni...na kuishi kwingi ni kuona mengi...hali kadhalika wahenga wanasema Tembea uyaone...Misemo hiyo mitatu inaweza kujidhihirisha kwa namna tofauti tofauti kupitia tukio la mkazi wa Jiji la Dar es salaam ambaye ni Mwalimu wa kike katika shule ya Sekondari Kibasila iliyopo hatua kadhaa kutoka Manispaa ya Temeke kubainika ndani kwake alipokua akiishi huko Yombo, Kisiwani Kata ya Sandari kuwa kuna shehena ya kinyesi cha binadamu katika ndoo, mabeseni, chupa za soda, maji pamoja na majagi.

Pichani juu ni  Wafanyakazi wa usafi wa Manispaa ya Temeke wakibeba kinyesi kwenda kukimwaga baada ya kuvunja nyumba aliyokuwa akiishi Mwalimu Gaudencia Albert.
 Ubebabi kinyesi ukiendelea
Shehena ya kinyesi iliyokuwa chumbani kwa mwalimu huyo. 


 ********
Manispaa ya Temeke jana Februari 25, 2015, imeteketeza kinyesi kilichokutwa katika chumba cha mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kibasila Gaudensia Albert baada ya maofisa wa afya wa manispaa hiyo kuchukua hatua hiyo ili kunusuru afya za wakazi wa eneo hilo.

Kazi hiyo ilifanyika majira ya saa tisa alasiri katika eneo la Yombo, Kisiwani Kata ya Sandari jijini Dar es chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi na wakishirikiana na Mwanyekiti wa Mtaa huo, Yahya Bwanga.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini wakati wa zoezi hilo, Ofisa Afya wa Manispaa ya Temeke, Floyd Tembo alisema tukio hilo walilipata juzi juzi jioni, baada ya kulipata waliwatuma Watendaji wa Afya wa Kata hiyo wafanye utafiti wakujua tatizo hilo lilikuwa na ukubwa gani. SOMA ZAIDI KWA KUBOFYA HABARI MSETO BLOG
Posted by MROKI On Thursday, February 26, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo