Nafasi Ya Matangazo

September 11, 2014

Mbunge wa Nzega ambaye pia ni Mchezaji wa timu ya wabunge wa Simba, Dk. Hamis Kingwangala (kushoto) akiwa uwanjani akilisakata kabumbu.
 *******
 Wakati nafanya tafakuri ya kama nigombee Urais mwakani ama la, haikunitokea hata siku moja kutamani kuutumia ujana wangu kama silaha ya kutafuta comparative advantage over wazee ukizingatia zaidi ya asilimia 60 ya population yetu ni vijana. 

Sababu kubwa iliyoniijia haraka haraka ni kuwa ujana pekee haitoshi kuwa kigezo cha mtu kuchagulika kuwa Rais ama haitoshi kuwa sifa ya kumnyima mtu fursa ya kuwa Rais; kwangu mimi Urais ni nafasi anayopaswa kupewa ama kunyimwa mtu kwa uwezo wake, sifa zake, rekodi yake n.k. Pia nimekuwa nikijiuliza kama ukipiga jalamba leo kuwa Rais wa sasa ni lazima awe kijana, hivi usipochaguliwa mpaka ukazeeka ndiyo kusema utaacha kugombea sasa? 

Nimepata fursa ya kusoma habari kwenye gazeti la Nipashe kuwa 'Urais si lelemama.' Humo amenukuliwa Dkt. Hassy Kitine, akisema wanaotaka Urais na wakatangaza nia ndiyo kwanza wamepoteza sifa ya kuwa Rais na watazamwe, kauli iliyokuja baada ya mimi kutangaza nia majuzi; 

Dr. Kitine anasema kuwa Urais ni nafasi ambayo unapaswa kuambiwa na wengine kuwa unauweza na hivyo kushawishiwa ugombee. 

Hapa nikaona kumbe ile hoja ya baadhi ya vijana wenzangu kuwa 'wanaona ni kitu kigumu kukubali kuongozwa na watu wa kizazi kingine ambao hawatakuwepo miaka 30 ijayo' inapaswa kufanyiwa tafakuri sana. Maana Dr. Kitine anatoa mfano namna Rais Mwinyi na Rais Mkapa walivyopatikana, na anaona kama hiyo ndiyo 'gold standard' ya kupata Rais bora kabisa. 

Ninachokiona hapa ni mwendelezo wa kuamini mambo mazuri ni yale ya kizazi chako tu, mapya yote ni mabaya na hayafai! Mimi na wenzangu tunaoamini katika mapinduzi ya kifikra tunadhani tunahitaji kufanya mambo kwa utofauti ili tutoe matokeo tofauti. Haijalishi matokeo yatakuwaje, mazuri ama mabaya. Tofauti tu. Thats the key word. 

Maana miongoni mwetu wanamabadiliko ya kifikra tunaamini kwamba kama unataka nafasi ya Urais usijifiche, we sema ili tukupime. Na kwamba kumwambia mtu ana uwezo na Urais ni kumkurupusha tu. Anaweza akawa hana vision wala agenda yoyote kwa nchi. 
 
Ni vema akasema anataka Urais na tukamhoji ana vision gani. Ili tushindanishe agenda za kila anayetamani.
Posted by MROKI On Thursday, September 11, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo