Nafasi Ya Matangazo

March 07, 2012

SBL YASITISHA UDHAMINI TAIFA STARS


KAMPUNI ya Bia ya Serengeti   SBL), mesitisha udhamini wake kwa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ulioanza mwaka 2006 kufuatia kupandishiwa dau la kuidhamini timu hiyo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Habari za kiuchunguzi, ambazo bongostaz imezipata zimesema kwamba SBL iliyoanza kuidhamini Taifa Stars kwa dau la Sh. Milioni 700, imetakiwa na TFF kutoa Sh. Bilioni 3.6 kwa mwaka kuidhamini timu hiyo.

Ofisa mmoja wa TFF, ambaye hakutaka kutajwa jina aliiambia bongostaz jana kwamba pamoja na hayo mazungumzo bado yanaendelea baina ya SBL na shirikisho hilo. 

Hata hivyo, Ofisa huyo wa TFF alisema shirikisho limeahidiwa udhamini mnono kutoka kampuni nyingine kubwa ya bia nchini.

"Lakini kwa kuzingatia pale ambapo SBL wameitoa Taifa Stars, waliichukua haina mdhamini na hakuna mtu au kampuni iliyokuwa tayari kuidhamini, wamefanya mambo mengi kwa manufaa ya soka hii, kwa kweli hata mimi ningependa SBL iendelee kudhamini timu hii,"alisema Ofisa huyo.

TFF iliipandishia dau la udhamini SBL kutoka Milioni 700 hadi 800, baadaye 900 na mwaka jana ilikuwa n Sh Bilioni 1.2. TFF sasa inataka Sh Bilioni 3.6 kwa mwaka na kwa sababu mkataba wa udhamin baina ya pande hizo mbili uliisha tangu Desemba, Taifa Stars haina mdhamini kwa sasa.


Teddy Mapunda, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mahusiano wa SBL alipoulizwa na bongostaz kuhusu mustakabali wa suala hilo, alikiri bayana kuwa sasa mambo yote yamesimama kwa sababu mazungumzo yanaendelea kati yao na TFF. Source HAPA

WAZIRI MAGUFULI AMTAHADHARISHA MKANDARASI ANAYEJENGA BARABARA YA MSATA - BAGAMOYO

Na Mwandishi wetu-Ujenzi
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amefanya ziara ya kushtukiza kutembelea mradi wa ujenzi wa barabara ya Bagamoyo hadi Msata ambayo inajengwa kwa kiwango cha lami na mkandarasi Estim Construction Company Ltd.
Katika ziara hiyo Mhe. Magufuli aliandamana na wataalamu mbali mbali kutoka Wizara ya Ujenzi Makao Makuu na Tanroads. Msafara huo hata hivyo ulilazimika kufanya kikao cha dharura eneo la Kiwangwa ambako ndipo sehemu ya lami kuanzia Msata ilipoishia ikiwa na urefu wa kilometa 25 tu kati ya kilometa 64 zinazokusudiwa kujengwa kwa mradi wote..
Mhe. Magufuli alielezea kuridhishwa na kiwango cha ujenzi alichokiona na kumtaka mkandarasi huyo kuendelea kuzingatia viwango hivyo alivyowekewa kimkataba. Hata hivyo wakati akipokea taarifa ya mradi alishtushwa kubaini kuwa hadi sasa mkandarasi huyo ametekeleza asilimia 46 tu ya kazi zilizopangwa wakati ambapo amekwishatumia asilimia 73 ya muda wa mradi wote.
Akitoa ufafanuzi Mwakilishi wa Kampuni ya JBG Gauff Ingenieure GMBH & CO ambayo ndiyo inayomsimamia mkandarasi wa mradi huu Injinia Kini Kiyoniza, alielezea kuwepo kwa ongezeko kubwa la viwango vya kazi kwamba ndiyo sababu ya kuchelewa kwa utekelezaji. Maelezo haya hayakumridhisha Waziri Magufuli na akamuagiza Mtendaji Mkuu wa Tanroads kuhakikisha anausimamia kwa karibu mradi huu na kuhakikisha kuwa hakuna visingizio vitakavyotolewa na kusababisha ongezeko la muda au gharama za mradi huu.
Ilielezwa kuwa Mkandarasi huyo anatakiwa kuwa amekamilisha mradi huu ifikapo mwezi Septemba mwaka huu wa 2012, za zipo kila dalili kuwa hataweza kumaliza kwa muda uliobaki kitu kilicho mlazimu Waziri Magufuli kuhoji ni kwanini mkandarasi huyo asijigawe katika makundi mawili kwani anavyo vifaa na kwamba hata madai yake yote yamelipwa kwa asilimia 100 hivyo kutokuwa na visingizio vyovyote vya ucheleweshaji.
Akimalizia Waziri wa Ujenzi alimtahadharisha Mkandarasi Estim kwamba Serikali haitakuwa tayari kuendelea kutoa kazi nyingine kwa makandarasi ambao wanashindwa kukamilisha kazi walizo nazo hadi wazikamilishe.
Alifafanua kuwa lengo ni kuwakuza makandarasi wazalendo lakini nao ni lazima waonyeshe kuwa wanauwezo wa kutekeleza kazi wanazopewa kwa ufanisi kwani miradi hii hutumia fedha nyingi za walipa kodi na hivyo ni budi zisimamiwe ipasavyo.Mradi wa ujenzi wa barabara kati ya Bagamoyo na Msata utagharimu kiasi cha Shilingi bilioni 88.6 hadi utakapo kamilika

Mkuu wa Gereza la Mahabusu mjini Songea awapandisha vyeo askari wa nne wa jeshi hilo leo

 
Mkuu wa Gereza la Mahabusu mjini Songea,SP Sylvester Shija (kushoto) kwa niaba ya Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama nchini Rais Jakaya Kikwete,akimvalisha cheo staff sajent Anna Alexander wakati wa hafla ya kuwapandisha vyeo askari wa nne wa Jeshi hilo Mjini Songea leo.
Mkuu wa Gereza la Mahabusu Mjini Songea,SP Silvester Shija akizungumza na askari pamoja na maofisa wa jeshi hilo mkoani Ruvuma mara baada ya kuwapandisha vyeo askari wa nne kutoka koplo hadi sajent na wengine kutoka sajent hadi staff sajent, kwa niaba ya Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini Rais Jakaya Kikwete.hafla hiyo imefanyika leo mjini humo.
Baadhi ya asakari magereza kutoka gereza la mahabusu mjini Songea wakiwapongeza askari wenzao wanne walipandishwa vyeo kwa ngazi mbalimbali mjini songea leo. PICHA NA MUHIDIN AMRI

Serikali yakataa masharti ya madaktari


Waziri Mkuu,Mh. Mizengo Pinda.

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema masharti ya madaktari ya kutaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk . Hadji Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya waondolewe nyadhifa zao ndipo majadiliano mengine yaendelee, hayakubaliki.

Pia amewasihi madaktari hao kutoendelea na mgomo leo na badala yake waiachie Serikali iendelee kushughulikia madai yao, likiwamo suala la kubadili uongozi wa wizara hiyo na iwapo wataendelea na mgomo, watambue kuwa maisha ya Watanzania yako mikononi mwao.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Pinda alieleza kushangazwa na kitendo cha madaktari hao kung’ang’ania hoja ya kufukuzwa kwa Dk Mponda na Dk Nkya, wakati waliwasilisha mbele ya Serikali madai mengi na yanayoendelea kushughulikiwa na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike.


Alisema alipokutana na madaktari hao aliunda Kamati iliyojumuisha sekta mbalimbali wakiwamo wajumbe wawili wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), wauguzi na wafamasia, kwa ajili ya kushughulikia madai ya madaktari hao na kamati hiyo ilishakamilisha kazi yake.

Hata hivyo, alisema katika mkutano wao wa mwisho na Serikali ulioongozwa kwa upande wa Serikali na Katibu Mkuu wa Wizara ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi, madaktari hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa MAT, Dk Namala Mkopi, waligoma kuendelea na mazungumzo wakitaka viongozi hao wasimamishwe.

“Niliambiwa kuwa wakati kikao hicho kinaanza, madaktari waliweka masharti ya kutaka viongozi hawa wasimamishwe ndipo majadiliano mengine yaendelee, nikajiuliza kwa nini wang’ang’anie masharti haya wakati tayari Serikali ilishasema yanashughulikiwa?” Alihoji. Alisema anachofahamu ni kwamba viongozi hao wawili nafasi zao ni za kisiasa na mwenye mamlaka ya kuwateua ni Rais.

“Hivyo kitendo cha Mkuu wa Nchi kupewa saa 72 awe amewasimamisha kazi, kwanza mimi sikubaliani nacho na ninajua hata Rais mwenyewe hatakubaliana nacho,” alisema.

Alisema inafahamika wazi kuwa madai waliyotoa madaktari hao kwake yanafanyiwa kazi na mengi kama vile nyongeza ya posho, posho za mazingira hatarishi, mishahara, posho za usafiri na bima, yanazungumzika na kwamba utaratibu wa kuyafanyia kazi ulikuwa unaendelea.

Alitoa mfano kuwa madaktari hao walitaka posho ya sasa kwa kima cha juu kwa madaktari ya Sh 25,000 kwa siku iongezwe na kufikia Sh 50,000 huku wengine wakitaka ifikie Sh 80,000, jambo ambalo linaweza kushughulikiwa ingawa kwa kupitia kwanza bajeti na hali ya uchumi wa nchi.

“Ndiyo maana nashangaa wenzetu hawa kulileta suala hili leo, wakati tulishatoka nao mbali hadi kufikia kusimamisha kwanza Katibu Mkuu (Blandina Nyoni) na Mganga Mkuu (Deo Mtasiwa), ili kupisha uchunguzi huku madai mengine yakishughulikiwa, kwa masharti haya mapya labda kama wenzetu wana jambo lingine,” alisema.

Aliwaomba madaktari hao waiachie Serikali kazi ya kushughulikia madai yao na kuendelea na kazi leo, lakini wakiendelea na mgomo huo kwa kisingizio cha kuwasimamisha Dk Mponda na Dk Nkya haitaleta picha nzuri kwa Watanzania, kwa kuwa wao ndio waathirika wakuu.

“Kwanza jamani huyu Dk Mponda ndiyo kwanza ana mwaka mmoja na miezi kadhaa tangu awe Waziri wa Afya na mengi ya madai ya madaktari hawa yanaonekana wazi ni matatizo ya muda mrefu, hali ambayo kweli Serikali imeona na kuamua kuijenga sekta hiyo ya afya ili iwe na meno,” alisema.

Alisema amesikia na kupokea ujumbe mwingi kuwa madaktari hao wamepanga kugoma leo huku wakidai kuwa wataikomesha Serikali.

“Naomba watambue kuwa wanachofanya si kuikomesha Serikali, bali kuwakomesha wagonjwa, kwani wao ndio waathirika wakuu, naomba watumie busara na hekima na kurejea kazini, ili kuwalinda Watanzania wasio na hatia.” Alisema ni jambo linalosikitisha kuona madaktari hao ambao wanatambua umuhimu wao kwa Taifa hasa suala la afya, kutumia fursa hiyo ya maisha ya Watanzania kuibana Serikali, kwa kuwa wanafahamu wanaweza kufanya lolote wanalotaka.

Alisema kimsingi, zipo sheria za nchi ambazo zinaweka bayana masharti kwa sekta zinazogusa watu, ikiwamo ya afya wafanyakazi wake kutogoma, kwa kuwa waathirika zaidi wa migomo hiyo ni wananchi ambao hawana hatia. Aliwataka madaktari kutambua kuwa sheria katika eneo hilo iko makini na kuwasihi iwapo wanataka kugoma basi wagome kwa misingi ya kisheria.

“Ila jamani ninawaomba sana madaktari wasigome na kuacha watu wakifa kwa kisingizio cha watu wawili, watambue kuwa huwezi kumpa Rais masharti, hili halikubaliki si hapa tu hata nchi zingine.” Kuhusu Serikali imejipangaje iwapo madaktari hao watagoma leo, Pinda alisema haijajiandaa na lolote kwa kuwa inaamini wataalamu hao watatumia hekima na kuiachia Serikali ishughulikie madai yao na wao kuendelea na kazi.

“Lakini jamani tujipange kwa lipi, kwa kuwa Mponda hajaondoka? Basi kama ni hivyo kuna tatizo kubwa kuliko inavyodhaniwa.” Aidha Pinda alisema mpaka sasa hajafahamu athari za mgomo wa madaktari uliopita na kutaka swali hilo, waulizwe wahusika wenyewe wa sekta ya afya, kwa kuwa wao ndio wanaofahamu jinsi Watanzania walivyoumia.

Zawadi za Tabora Marathon kuwekwa hadharani leo

Rais wa Riadha Tanzania (RT), Francis John (kati) akizungumza wakati wa utambulisho wa mbio za Tabora Marathon. Wengine ni waratibu wa mbio hizo ambazo zimekuwa gumzo kubwa mjini Tabora

KAMATI ya mbio za Tabora Marathon 2012, leo inatarajiwa kuanika zawadi za washindi wa mbio hizo za kwanza kihistoria kufanyika mkoani humo.
Mbio za Tabora Marathon 2012 zinatarajiwa kurindima mjini Tabora Machi 10 na kushirikisha wakimbiaji kutoka mikoa mbalimbali ya Kanda ya Magharibi.
Kwa mujibu wa Mshauri wa Ufundi wa Tabora Marathon, Tullo Chambo, leo watafanya jukumu hilo baada ya kufanikiwa kukamilisha maandalizi mbalimbali, ikiwamo wadhamini.
Chambo alisema, licha ya ugumu wa upatikanaji wa wadhamini, lakini wanawashukuru waliojitokeza kufanikisha mbio hizo, ambazo ni chachu ya kuhamasisha mchezo huo na kuibua vipaji.
“Kimsingi hadi kufikia hatua hii, tumehangaika usiku na mchana na ninawashukuru wapenda michezo wote walionyesha mapenzi mema na mchezo huu na Mkoa wa Tabora kwa ujumla, kwa kuweza kufanikisha kufanyika kwa mashindano haya ya kipekee katika historia ya mchezo wa riadha mkoani Tabora na Kanda ya Magharibi kwa ujumla,” alisema Chambo na kuongeza kuwa;
Leo tutawaanika wote waliofanikisha mbio hizi katika mazingira magumu, pamoja na zawadi ambazo washindi watazawadiwa katika mbio hizo.
Pia aliwapongeza viongozi wa serikali mkoani Tabora, chini ya RC, Fatma Mwasa, na viongozi wa Chama cha Riadha Mkoa wa Tabora, kwa ushirikiano wao uliofanikisha kufikia hatua hii.

Serengeti Premium Lager wins DLG’s gold medal for quality


Serengeti Premium Lager has been awarded yet another gold medal for 2012 from DLG, an international leading testing organisation, for its high quality standards.

DLG is Germany-based highly respected organisation which shares knowledge and expertise worldwide with leading international practitioners, experts and other specialist organisations.
The DLG gold medal is awarded for a duration of 24 months.

The award winning news was gladly received by senior officials at Serengeti Breweries Limited (SBL), who expressed their confidence in the great brand, which has now won its third gold medal from DLG, in addition to several others from Monde Selection. 

“Great result for Serengeti!,” remarked Colman Hanna, SBL plant Manager for Dar es Salaam. “Congratulations!!” said Frank Mrazek, SBL Plant Manager for Mwanza.

“I would like to congratulate Master Brewer Colman Hanna, Donani Ritte of our Dar Brewery, and Supply Chain Director Mark Taylor, for this delightful recognition as I do know that consistent quality results are always a matter of great team effort”, said Ephraim Mafuru, the Director of Marketing at SBL.

Teddy Mapunda, SBL Corporate Relations Director had this to say: “This is a big moment for our company. I would like to recognize the production staff at SBL today for their brewing excellence and unwavering attention to quality performance.” 

Allan Chonjo, Brand Manager for Serengeti Premium Lager expressed his gratitude for the brand’s achievements: “Consumers of Serengeti Premium Lager can be confident that the brand is one of the best tasting and highest quality beers not only locally, but also internationally.”

The brand has been consistently winning awards in global competitions, a testimony to its outstanding quality, taste and refreshment. 

East African Breweries Ltd (EABL), a subsidiary of multinational brewing company, Diageo, acquired majority stake in SBL in 2010. Since the acquisition, SBL products have been winning consumers’ confidence and are placed among the top brands in the market.

March 06, 2012

Maelfu wamuga marehemu Jane Mponzi Dar es Salaam

 Maelfu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam leo wameungana na Familia ya Mhandisi Mponzi wa Oysterbay jijini Dar es Salaam akatika misa maalum ya kumuaga binti yao kipenzi Jane G. Mponzi aliyefariki juzi Machi 4,2012 saa 4 asubuhi baada ya kuugua ghafla. Jane Mponzi aliyekuwa Mfanyakazi wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom na shabiki mkubwa wa Timu ya Simba ya Dar es Salaam pamoja na Man U aliagwa kwa awamu mbili ambazo zote zilifurika watu isivyotarajiwa.
 Baadhi ya waombolezaji wakiwa nyumbani kwao na marehem,u jijini Dar es Salaam.
 Ben Mponzi mdogo wa marehemu akisoma wasifu wa marehemu dada yake.
 Waombolezaji wakiwa nyumbani katika msiba.
 Familia ya Mzee Mponzi ikiwa Kanisani
 Waombolezaji waliofika katika Misa maalum ya kumuombea Marehemu Jane wakiwa Kanisani St Peter Dar es Salaamkabla ya mwili kusafishwa kwenda Tosamaganga Iringa kwa maziko kesho mchana.
 Kiukweli watu walikuwa wengi sana na magari yalikuwa mengi hadi Shule ya Msingi Oysterbay.
 Athumani Hamisi alikuwa ndiye mtu wa kwanza kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Jane.
 Watu kutoka Vodacom nao walityoa heshima
 Viongozi wa Dini na wanasiasa nao walifika kutoa heshima za Mwisho kwa marehemu Jane Mponzi.
 baba wa Marehemu akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Jane Mponzi.
 Wanafamilia
 Mwili ukitolewa nyumbani
 Padri akiunyunyizia maji ya baraka
Padri akiendesha misa maalum ya kumuombea marehemu.

RAIS KIKWETE AFUNGua MKUTANO MKUU WA MWAKA WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI LEO MJINI MOSHI


Rais Jakaya Kikwete akizindua mojawapo ya vitabu vya muongozi wa Jeshi la Polisi  wakati wa  ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi  Chuo cha Polisi mjini Moshi leo Machi 6, 2012  Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Shamsi Vuai Nahodha wa kulia Rais ni Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh Leonidas Gama
Sehemu ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi  Chuo cha Polisi uliofunguliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete mjini Moshi leo Machi 6, 2012 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa  ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi  Chuo cha Polisi mjini Moshi leo Machi 6, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili Chuo cha Polisi mjini Moshi leo Machi 6, 2012 tayari kwa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Shamsi Vuai Nahodha na kushoto kwake ni Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema.

SBL yazindua tuzo za Diageo za Waandishi wa habari za Biashara Afrika

Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bi. Teddy Mapunda akifafanua kwa msisitizo namna ya kushiriki, kwenye uzinduzi wa tuzo za Diageo za Waandishi wa habari za Biasharara Afrika ((Diageo Africa Business Reporting Awards 2012)
Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bi. Teddy Mapunda (pichani kati) akifafanua jambo mbele ya Wanahabari kuhusiana na tuzo hizo,Kulia ni Meneja Mahusiano ya Jamii,Nandi Mwiyombela na kulia ni Meneja Mahusiano ya ndani (SBL) Imani Lwinga.


TUZO ZA DIAGEO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA BIASHARA AFRIKA 2012-(Diageo Africa Business Reporting Awards 2012) ZAZINDULIWA RASMI.

TUZO HIZI ZINAENZI UANDISHI WA HABARI ZA BIASHARA AFRIKA.

Usajili  wa tuzo sasa uko wazi kufanyika kwenye tovuti. 

Kampuni ya Biaya Serengeti (SBL), ambayo ni kampuni tanzu ya Diageo, inayoongoza duniani katika biashara ya vinywaji vyenye kileo,  leo wamezindua rasmi tuzo za habari za kibiashara kwa mwaka huu 2012. 

Tuzo hizi zilianzishwa na Diageo mwaka 2004, kwa ajili ya kuwatambua waandishi wa habari na wahariri ambao wameweza kutoa taarifa zilizojitosheleza na za hali ya juu katika mazingira ya biashara Afrika. 

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Bi. Teddy Mapunda alisema“ Kampuni ya Diageo   inaamini kwamba taarifa nzuri na zina mchango mkubwa wa kuinua mtazamo wa  maendeleo na uchumi wa Afrika na changamoto zake.”  

Habari hizo kwa kiasi kikubwa zinahamasisha nia ya kufanya biashara na zinaangaza mazingira mazuri na  ya uhakika juu ya utajiri wa bara hili,”alisema Bi Mapunda. 

Bw. Nick Blazquez, Raiswa Diageo Afrika, naye alitoa vielelezo kuhusu tuzo hizi na alikuwa na haya ya kusema: “Ni dhahiri kabisa sasa kwamba hamasa ya biashara Afrika imepanuka na dunia nzima sasa imeridhika na kiwango cha ukuaji wa uchumi barani Afrika. 

Kama kampuni inayoendesha shughuli za kibiashara Afrika, tunaelewa umuhimu wa kuongezeka kwa taaluma ya uandishi wa habari za kiabishara na jinsi inavyounda mazingira mazuri na kuvutia kwa uwekezaji wa muda mrefu,” aliongeza. 

“Nikiangalia miaka ya nyuma n amaendeleo ya tuzohizi, nimetambua uamsho wa hali ya juu na viwango vilivyomo katika uandishi wa habari za kibiashara na kuongezeka kwa juhudi za vyo mbo ya habari ndani na njeya Afrika ili kuhamasisha biashara na ujasiria mali barani humu. 

Ninajivuniakwamba Diageo inatambua mafanikio haya na tunategemea kuona mchango wa hali ya juu kwa siku za usoni.” 

Wakati tuzo hizi za waandishi wa habari za biashara Afrika kutoka Diageo zinakaribia kutimiza miaka kumi tangu kuanzishwa kwake, Diageo inaendelea kufikiria jinsi watakavyobadilisha uhalisia, matokeo na namna ya kuwafikia zaidi walengwa wa tuzo hizi. 

Diageo inategemea kuboresha zaidi utoaji wa tuzo hizi kupitia mafanikio ya mwaka uliopita, kukaribisha usajili kutoka vyombo vyote vya habari na kutoka bara zima la Afrika na nje yaAfrika. 

Mwaka huu, kundi la mfumo mpya wa utoaji wa habari limeondolewa na kuwa kundi linalojitegemea ili kuonyesha upana wa vyombo vinavyotumia mfumo huu wa utoaji habari. 

Waandishi wa habari wanahamasishwa kutuma maombi yao. Habari ziwe zimetolewa kupitia mfumo wa vyombo vyote vya habari, ikiwa ni pamoja na gazetimtandazo (blogs) na habari zilizochapishwa kupitia tovuti mbalimbali pia wanaruhusiwa katika makundi yote, yaani 'categories'. 

Sherehe yaTuzo hizi zitafanyika mjini London, Uingereza tarehe 28 mwezi Juni.Tarehe ya mwisho wa kupokelewa kwa maombi haya ni siku ya Ijumaa tarehe 23 mwezi Machi mwaka huu. Maombi yote yatumwe kupitia tovuti yetu: www.diageoafricabusinessreportingawards.com.  Hakuna kiingilio.

Wanahabari Iringa waandamana

Hatimaye waandishi wa habari wa Iringa waandamana leo wakiwa na madai mengi, ikiwamo kunyimwa posho na kutotendewa haki na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa hasa wakati wa ziara za viongozi. Tembelea www.simonmkina.com kwa picha zaidi. Hii iliwahi kufanyika miaka kadha iliyopita jijini Dar es Salaam.

NHIF YAWEKA KAMBI YA UPIMAJI AFYA STENDI KUU MKOANI SINGIDA NA KUTOA MSAADA KATIKA HOSPITALI ZA MKOA HUO


DR. KUBONYA WA NHIF AKIMPA USHAURI WA NAMNA YA KULINDA AFYA YAKE KUTOKANA NA UZITO ULIOONGEZEKA,BW. ALLY JUMANNE AKIWA NI MMOJA WA WAKAZI WALIOJITOKEZA KUPIMA NA KUJUA HALI ZA AFYA ZAO LEO MKOANI SINGIDA,NHIF IMEWEKA KAMBI HIYO MAHUSUSI IKIWA NI KUWAHAMASISHA WANANCHI KUWA NA UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA MARA KWA MARA.
MJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI WA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA BW. ALEX MAGESA AKITOA ZAWADI YA MASHUKA 700 KWA HOSPITALI,ZAHANATI NA VITUO VYA AFYA MKOANI SINGIDA KUPITIA KWA MUUGUZI MKUU WA MKOA HUO BI.ELLETRUDE MAKOWI.
BW. DEUS KUNUWA AKIMPIMA UWIANO WA UREFU NA UZITO WA MWILI KITAALAMU (BMI) BW. JOSEPH SANGAU,UHAMASISHAJI WA UPIMAJI WA AFYA KWA WANANCHI WA SINGIDA UNAKWENDA SANJARI NA SIKU YA WADAU INAYOFANYIKA MKOANI HUMU AMBAPO WANANCHI WANAIMIZWA KUJIUNGA NA MIFUKO YA AFYA YA JAMII KWANI NDIYO MKOMBOZI WA HUDUMA ZA AFYA KWENYE HALMASHAURI ZAO HUSUSANI VIJIJINI.
MGANGA MKUU MFAWIDHI WA HOPSITALI YA MKOA WA SINGIDA DKT. SULEMANI MTTANI AKIMWELEZA MJUMBE WA BODI YA NHIF BWN ALEX MAGESE MAANDALIZI YA AWALI YA UKARABATI WA JENGO(ALIPO PICHANI) LITAKALOTUMIKA KUWAHUDUMIA WANACHAMA WA NHIF NA CHF HIVI KARIBUNI.

March 05, 2012

TBL YASAIDIA UCHIMBAJI VISIMA VYA MAJI MOROGORO


Ofisa Ustawi Jamii Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro, Tabitha Majiku  (kulia) akitoa neneo la shukrani baada ya kupokea msaada wa fedha za kusaidia miradi ya maji mkoani humo  kutoka Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro. Kutoka kushoto ni  Mkurugenzi wa Uhusiano na   Sheria wa TBL, Steve Kilindo  na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk. Ntobi Mwakibete (wa pili kulia).
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo  (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni 24.9 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk. Ntobi Mwakibete za kusaidia kuchimba kisima cha maji.  Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amiri Nondo akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. milioni 26.7, Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Uchimbaji Visima vya Maji ya Jae-Hi-Tech Dry Cleaning, Maximillian Makota zilizotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa ajili ya uchimbaji wa visima vya maji mkoani humo. Kulia ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa TBL, Steve Kilindo. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Morogoro.

Leah Samike anawakaribisha hapa sasa

Napenda kuwafahamisha kuwa nimefungua studio ya kusafisha picha, nawakaribisha kuleta kazi zenu Ofisi ipo Mtaa wa Jamhuri na Upanga hapa Azam Take Away.
karibuni sana.
siku  njema.

Jane Mponzi kuagwa Kesho Dar na kuzikwa Jtano Tosamaganga Iringa

Familia ya Bwana Gabriel Mponzi wa Oysterbay,Jijini Dar-es-salaam.Wanasikitika kutangaza kifo cha
mpendwa mtoto wao Jane Mponzi “Mama Melanie” pichani kilichotokea siku ya jumapili tarehe 4/3/
2012 katika Hospitali ya Agha Khan Dar-es-salaam.

Ibada ya kumuaga marehemu itafanyika Jumanne tarehe 6/3/2012 nyumbani kwa marehemu
Oysterbay, Dar-es-salaam kuanzia saa 6 mchana na marehemu atazikwa Ipamba-Tosamaganga, Iringa
siku ya Jumatano tarehe 7/3/ 2012.

Kwa maelezo zaidi kuhusu ratiba ya mazishi, wasiliana na mwenyekiti wa kamati ya maandalizi
Dr. Ponziano Mponzi kupitia namba 0767 600 604.

Ndugu, jamaa na marafiki waliopo mbali, wanaweza kutuma michango yao ya kufanikisha safari ya
mwisho ya kwenda kumlaza mpendwa wetu Iringa kupitia:

M-PESA- 0756 -999-900
TIGO PESA- 0713 -123- 617
AIRTEL MONEY- 0784- 615-566

Bwana ametoa na Bwana ametwaa,Jina la Bwana lihimidiwe.
Amina.

March 04, 2012

Acheni Simba aitwe Simba; yaibanhua Kiyovu 2-1 Taifa.


Dakika ya 19 na 32 za mchezo,Mshambuliaji wa timu ya Simba,Felix Sunzu akipachika mabao 2 katika kipindi cha kwanza,baada ya kupata pasi safi kabisa kutoka kwa mchezaji Emmanuel Okwi (Balloteli),hivi sasa ni kipindi cha pili na mpira unaendelea, Kiyovu mnamo dk ya 76 wanaweka goli la  kwanza kimiani.

Felix Sunzu akikimbia kwa furaha mara baada ya kuitikisa nyavu za Kiyovu goli la pili.
  Kikosi cha Kiyovu Rwanda.
 Kikosi cha Simba SC
 Shangwe kutoka kwa mashabiki wa simba.
Sunzu akihangaika kumtoka mchezaji wa Kiyovu.
Washabiki wa Simba full buruuudani baada ya timu yao kuibuka na goli 2 kipindi cha kwanza.Mpira unaendelea kipindi cha pili ambapo timu ya Kiyovu inajipatia goli la 1.

Watangazaji wa Clouds FM/TV Eprahim Kibonde na Shaffii Dauda wakienda hewani live hivi sasa .
 Clouds TV wakiwa live 
 Mashabiki wa simba kibao.
 Shabiki wa Simba akipuliza Vuvuzela.
 Burudani za hapa na pale zilikuwepo Uwanjani.
 Shabiki wa Simba kwa Mbwembwe balaa.
 Mashabiki wa timu ya Simba ya Jijini Dar es Salaam,wakiwa wamefurika kwa wingi ndani ya uwanja wa Taifa kwa ajili ya kuishangilia timu yao inayoingia dimbani muda mfupi ujao kumenyana na timu ya Kiyovu ya nchini Rwanda katika mashindano ya Kombe la Shirikisho ikiwa ni mchezo wa pili mara baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa awali huko nchini Rwanda.
Baadhi ya Wanahabari wakiwapiga picha watu waliokuwa wamevalia kinyago cha mfano wa mnyama Simba.

Wachezaji wa Simba wakipiga jalamba kabla ya mchezo kuanza.
Wachezaji wa Kiyovu ya nchini Rwanda wakiomba dua kabla ya kuanza kwa mchezo.
 Picha na Jiachie blog.

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More