Nafasi Ya Matangazo

March 27, 2010

Timu ya Tifa Taifa Stars leo imeutumia vyema uwanja wake wa nyumbani wa Uhuru Dar es Salaam kwa kuwacharaza makombora 6-0 timu ya Tifa ya Simalia katika mchezo wa kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Magoli ya Stars yalifungwa na John Bocko, Kigi Makasi, NMrisho Ngasa, Erasto Nyoni, Mussa Hassan "Mgosi" na Nadir Haroub "Canavaro".

Kwamotoke hayo sasa Stars itakutana na Rwanda katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam mvhezo utakaopigwa Mei Mosi mwaka huu.
Pichani ni Erasto Nyoni akiwania mpira dhidi ya Anwar Sadat Ibrahimi (chini) wa somalia.


Kikosi cha Stars Kilikuwa kama Ifuatavyo.
1.Shaban Hassan Kado
2.Shadrack Nsajigwa
3.Stephano Mwasika
4.Nadir haroub
5.Kevin Yondan
6.Erasto Nyoni
7.Mrisho Ngasa
8.Andulhalim Muhoud
9.John Bocco
10.Abdi Kassim
11.Kigi Makasi

WALIOINGIA BADAE
1.Nurdin Bakar
2.Uhuru Suleiman
3.Mussa Hassan "Mgosi"

Kocha ni Marcio Maximo
Mwamuzi wa kati-Kirwa Sylvesta toka KENYA.
Akisaidiwa na Ngururi John na Range marwa Aden wote toka Kenya.
Kamisaa wa mchezo ni Israel Mujuni Nkongo toka Tanzania.
Msimamizi wa mchezo. Hussein Fadoul-Toka Djibouti.
Mlinzi alikuwa ni ASP Jonas Mahanga
Posted by MROKI On Saturday, March 27, 2010 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo