Nafasi Ya Matangazo

September 09, 2016


Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Aggrey  Mwanri, akitoa soma la fursa kwa baadhi ya Wananchi wake waliyojitokeza ndani ya Ukumi wa Chuo cha Uwaziri mjini Tabora mapema leo.



Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Nikki wa Pili akiwafungua wakazi wa Tabora kwa kuwaonyesha fursa wanazopaswa kuzitumia ili waweze kusukuma mbele maendeleo ya mkoa huo.



Msanii wa Muziki wa Kughani Mashairi, Mrisho Mpoto akiwa amenyanyua mikono juu wakati akiwapa mbinu za mafanikio wakazi wa Tabora.



Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh.  Aggrey Mwanri (wa nne kutoka kushoto), akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na wanasemina hiyo.

 Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Ruge Mtahaba (katikati), akiongea jambo mbele ya Mkuu wa Mkoa huo wakati akitoa somo la Fursa.


Afisa Masoko wa kanda ya kati wa NMB, Josephine Kulwa akiwapatia fursa wakazi wa Tabora namna wanavyoweza kufaidika na fursa mbalimbali kwa kujiunga na baadhi ya huduma zitolewazo na benki hiyo. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.


MKUU wa Mkoa wa Tabora MH. Aggrey D.J Mwanri mapema leo alijikuta akitoa ya moyoni kwa kuisifia kamati na uongozi mzima uliyoandaa tamasha la Fiesta 2016 kwa kuwapelekea Darasa la Fursa.

Akizungumza ndani ya Ukumbi wa chuo cha Uwaziri mjini Tabora wakati wa semina hiyo Mkuu wa Mkoa huo Mh. Aggery Mwanri alisema kuwa, amefurahishwa sana na uongozi mzima wa Fiesta kwa kuwawezesha wakazi wa mji huo kuwaonyesha namna ya kupambana kimaisha kwa kutumia rasilimali zilizopo mkoa hapo.

“Napenda kutumia muda huu kutoa pongezi zangu za dhati kwa waandaaji wa Tamasha la Fiesta hasa kupitia darasa hili la Fursa ambalo naamini wazi kabisa kila mmoja wetu aliyehudhulia hapa ataweza kujifunza na kuvuna mbinu mbadala za kujikwamua kimaisha na kuufanya Mkoa wetu wa Tabora kuongeza uajibikaji,”

Pia Mh. Mwanra aliwaomba wananchi wa mkoa huo kutumia fursa ya buruda zitakazo endelea usiku wa leo katika Uwanja wa Ali Hassani Mwinyi kwa kusitarehe na kuangalia vitu vya msingi vye kuwaongezea kipato zaidi.

Semini hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba ilionekana kuchangamka vilivyo na kuwafanya baadhi ya wahudhuliaji wakiwemo wanafunzi wa Chuo hicho kuomba darasa hilo liwe linawafikia mara kwa mara mjini hapo.
Posted by MROKI On Friday, September 09, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo