Nafasi Ya Matangazo

July 08, 2025








Na Mwandishi wetu, Nachingwea,Lindi
Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde (Mb) amebainisha kuwa Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameelekeza kutolewa kwa leseni ya uchimbaji madini ya nikeli kwa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na kwa Wachimbaji wadogo waliokuwepo katika eneo la vilima vya Ntaka- Nachingwea,Mkoani Lindi.

Waziri Mavunde ameyasema hayo leo tarehe 08 Julai, 2025 katika mkutano wa hadhara wa wananchi na wachimbaji katika Kijiji cha Nditi punde tu baada ya kufanya ziara ya kutembelea maeneo na migodi ya wachimbaji wadogo chini ya Umoja wa Vikundi vya Wachimbaji Madini (UVIWAMA).

" Rais Dkt. Samia S. Hassan amesikia kilio chenu cha muda mrefu cha kutaka kupewa maeneo ya uchimbaji katika Leseni inayomilikiwa na Serikali. Na ndiyo maana nimefika hapa kuja kuwaletea habari njema wachimbaji wadogo kwamba, hatutawaondoa katika eneo mnalochimba na tunakwenda kuwarasimisha.

Pamoja na kupewa eneo la uchimbaji, naomba niwasihi wachimbaji wadogo kufuata taratibu kwa mujibu wa Sheria ya Madini Sura ya 123 ambayo inaelekeza mwenye haki madini kuhakikisha anapata ridhaa ya mwenye haki ardhi kabla hajaanza uchimbaji, ili kuepusha migogoro katika shughuli zao za uchimbaji.

Rais Dkt. Samia ameelekeza eneo la leseni hiyo lenye ukubwa wa Kilometa za Mraba 45 ipewe Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kwa ajili ya kuanza uchimbaji mkubwa wa nikeli ndani ya miezi 18 ijayo kama Sheria ya Madini inavyoelekeza.

Kwakuwa kwenye Leseni hii serikali ililipa zaidi ya shilingi bilioni 243 kama fidia, ni lazima sasa  STAMICO na wachimbaji wadogo wafanye uchimbaji wenye tija ili kurejesha fedha hizo katika mfuko mkuu wa Serikali”Alisema Mavunde

Awali, akitoa salam kwa niaba ya wachimbaji wadogo, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo Mkoa wa Lindi (LIREMA), Bw. Mayunga Musa Buyaga amesema wachimbaji wadogo wanamshukuru sana Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa upendo mkubwa na kuwajali na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kufanya uchimbaji wenye tija.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Zainab Telack amempongeza Mh. Rais Dkt Samia kwa kurudisha matumaini na nyuso za furaha kwa wachimbaji wadogo na kuahidi kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati ili shughuli za uchimbaji zifanyike kwa utaratibu uliowekwa pasipo kuzalisha migogoro.
Posted by MROKI On Tuesday, July 08, 2025 No comments






Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Wananchi wametakiwa kuchangamkia fursa za uwekezaji katika uchimbaji wa madini ya bati yanayopatikana kwa wingi katika Mkoa wa Kagera, hususan katika Wilaya ya Kyerwa, kufuatia mahitaji makubwa ya madini hayo ndani na nje ya nchi.

Wito huo umetolewa leo na Mkaguzi Msaidizi wa Madini kutoka Ofisi ya Afisa Mgodi Mkazi – Kyerwa, Gilbert Fumbo, alipokuwa akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Fumbo amesema kuwa Mkoa wa Kagera umejaliwa kuwa na madini mengi ya bati yanayopatikana katika maeneo ya Kyerwa, Sindicate, Kabingo, Murongo, Katera na Kaitambuzi, akibainisha kuwa bado kuna fursa kubwa kwa wananchi na wawekezaji kuchukua hatua za uwekezaji.

“Mahitaji ya madini ya bati katika soko la kimataifa ni makubwa ikilinganishwa na idadi ya wachimbaji waliopo kwa sasa. Tunawahamasisha wananchi kujitokeza kuomba leseni za uchimbaji wa madini na kuanza shughuli rasmi za uchimbaji ili kujiongezea kipato, kuchangia mapato ya Serikali na kukuza uchumi wa nchi,” ameeleza Fumbo.

Ameongeza kuwa azma ya Serikali kupitia kaulimbiu ya “Madini ni Maisha na Utajiri” inalenga kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini. Amebainisha kuwa Ofisi ya Madini Mkoa wa Kagera imejipanga kikamilifu kutangaza fursa za uwekezaji ili kuhakikisha rasilimali hizo zinawanufaisha Watanzania.

Fumbo pia ameeleza kuwa kutokana na jitihada za Tume ya Madini za kuhamasisha uwekezaji, wawekezaji kutoka mataifa ya China, Korea na Urusi wameanza kujitokeza kwa wingi katika shughuli za uchimbaji wa madini ya bati tangu mwaka 2024.

Kuhusu mchango wa madini hayo kwenye makusanyo ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Fumbo amebainisha kuwa madini ya bati yamechangia shilingi bilioni 1.423, sawa na asilimia 94.86 ya lengo la ukusanyaji wa shilingi bilioni 1.5 la madini hayo.

Katika hatua nyingine, Fumbo ameainisha uwepo wa madini mengine muhimu kama tungsten yanayopatikana katika eneo la Kigorogoro, ambayo hutumika kutengeneza vifaa vya kivita na kielektroniki, na kuwahamasisha wananchi kuchangamkia pia fursa za uchimbaji wa madini hayo.

“Kagera siyo tu ina utajiri wa ardhi yenye rutuba, bali pia ina hazina kubwa ya madini ambayo tukiyatumia vyema, yanaweza kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa jamii na taifa kwa ujumla,” amehitimisha Fumbo.
Posted by MROKI On Tuesday, July 08, 2025 No comments
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy akiwasili kwenye Banda la REA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam Julai 7, 2025
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kushoto) akipata maelezo kuhusiana na bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia zinazosambazwa na Kampuni ya Jicho Chanya kutoka kwa Afisa Masoko wa kampuni hiyo, Ibrahim Kikoti kwenye Banda la REA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam Julai 7, 2025.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kushoto) akiwa amebeba bidhaa ya kuni poa inayozalishwa kutokana na mabaki ya  miwa na Kampuni ya Hanny G Investment ya Arusha wakati akipata maelezo kuhusiana na kuni hiyo kutoka kwa Afisa Masoko wa kampuni, Neema Chiva kwenye Banda la REA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam Julai 7, 2025.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kulia) akipata maelezo kuhusiana na bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia zilizoandaliwa kwa teknolojia iliyoboreshwa katika Banda la REA kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam Julai 7, 2025.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mratibu wa Miradi wa Kampuni ya TaTEDO-SESO inayojihusisha na Uendelezaji wa Teknolojia na Huduma za Nishati Endelevu, Shima Sago kuhusiana na bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia zinazozalishwa na kampuni hiyo wakati wa Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam katika Banda la REA Julai 7, 2025


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Amebainisha hayo Julai 07, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

“REA inalo jukumu la kuhakikisha maeneo yote ya vijijini yanapata aina zote za nishati safi zinazotumika nchini ikiwemo; umeme, nishati safi ya kupikia pamoja na bidhaa za mafuta ya petroli na dizeli na hili linafanyika kupitia miradi mbalimbali ambayo baadhi imekamilika na mingine ipo katika hatua tofauti tofauti za utekelezaji,” amebainisha Mha. Saidy.

Alisema Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia umeelekeza ifikapo mwaka 2034; angalau 80% ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia na REA ni miongoni mwa taasisi zilizopewa jukumu la kuhakikisha lengo hilo linafikiwa.

Alibainisha kuwa kwa sasa takriban asilimia 96 ya wananchi maeneo ya vijijini wanatumia kuni na mkaa kupikia na kwamba jukumu lililopo ni kuhakikisha wananchi hao wanaachana na matumizi ya nishati zisizo salama na kuanza kutumia nishati safi na salama.

Alitaja hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na REA ikiwemo uhamasishaji na uelimishaji wananchi kufahamu athari za kutumia nishati isio salama pamoja na kuwafahamisha faida za kutumia nishati safi ya kupikia, kuwarahisishia wananchi upatikanaji wa bidhaa za nishati safi jirani na maeneo yao na kuwezesha teknolojia za nishati yenyewe.

“Kuna dhana imejengeka kwamba nishati safi ya kupikia ni gharama kuliko nishati zingine dhana ambayo haina ukweli kwa 100% kwani kwa sasa kuna teknolojia zilizoboreshwa ambazo zinazuia upotevu wa nishati wakati wa kupika hivyo kuwapunguzia gharama watumiaji," alifafanua Mha. Saidy.

Aliongeza kuwa watu wengi hawaangalii gharama nyingine kama muda wanaotumia kusaka kuni na madhila mengine wanayokutana nayo huko porini wakati wakisaka kuni.

Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha REA kutekeleza jukumu la kusimamia upatikanaji wa nishati safi ya kupikia hasa ikizingitiwa kuwa yeye ni kinara wa nishati safi ya kupikia.

Alibainisha baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana tangu kuanza kutekeleza mkakati huo wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo ni pamoja na kuwezesha wananchi maeneo mbalimbali vijijini kuhama kupitia ruzuku iliyotolewa ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ya kilo 6 na vichomeo vyake.

“Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Samia ilitoa ruzuku ya 50% kwenye mitungi ya gesi ya kupikia ipatayo 452,000 ambayo imeshaanza kusambazwa kwenye mikoa yote Tanzania Bara na zoezi linaendelea; sambamba na mitungi 110,000 ambayo ilisambazwa mwaka juzi kupitia Wabunge kwenye majimbo yao,” alisema Mhandisi Saidy.

Sambamba na hilo, Mha. Saidy alibainisha kuwa REA imewezesha Jeshi la Magereza ambapo kwa sasa magereza zote 129 zimehama kutoka kwenye matumizi ya nishati zisizo salama, na hivi karibuni REA imekuja na mpango wa kuwezesha Maafisa wa Jeshi la Magereza nao kutumia nishati safi ya kupikia katika familia zao.

“Kama mtakumbuka Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza taasisi zinazohudumia zaidi ya watu 100 zianze kutumia nishati safi ya kupikia na hili tunatekeleza na tunatarajia kuzifikia zaidi ya taasisi 400 katika mwaka huu wa fedha. Tulianza na Jeshi la Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na takriban shule 53,” alibainisha Mha. Saidy.

Mhandisi Saidy vilevile alibainisha mradi wa mikopo nafuu wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vya mafuta ya petroli na dizeli ulioanzishwa na REA ambao umelenga kuwasogezea wananchi wa vijijini huduma kwa gharama nafuu na ubora unaokubalika.
Posted by MROKI On Tuesday, July 08, 2025 No comments

July 07, 2025






Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi leo 7 Julai, 2025 ametembelea banda la Wizara ya Nishati  kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa maarufu kama sabasaba jijini Dar es salaam

Akiwa kwenye banda la Wizara ya Nishati Mhe Mwinyi alipokelewa na Mkuu wa kitengo cha  Mawasiliano Serikalini Bi Neema Chalila Mbuja, ambapo alimweleza juu ya hatua za utekelezaji zilizofikiwa kwenye utekelezaji wa mkakati wa Taifa wa nishati safi ya kupikia na kuongeza kuwa ajenda hiyo ni utekelezaji wa azimio la Mhe Rais Samia kama kinara wa nishati safi ya kupikia.

Amesema Wizara ya Nishati kupitia taasisi zilizopo chini ya Wizara zimekuwa zikitekeleza kwa vitendo ajenda hiyo kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambae ni kinara wa nishati safi ya kupikia kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

Wizara ya nishati tayari imezindua mikakati miwili ya nishati safi ya kupikia na ule wa mawasiliano ili kuwezesha utekelezaji wa ajenda ya nishati safi ya kupikia kwa vitendo
Posted by MROKI On Monday, July 07, 2025 No comments

 BOFYA LINK HII KUONA MATOKEO 
Posted by MROKI On Monday, July 07, 2025 No comments





Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Dkt. Venance Mwasse, ameipongeza Tume ya Madini kwa mafanikio makubwa ya kuvuka lengo la makusanyo ya mapato kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo imekusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.071 dhidi ya lengo la shilingi trilioni 1.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika banda la Tume ya Madini kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, Dar es Salaam, Dkt. Mwasse amesema mafanikio hayo ni matokeo ya usimamizi makini, matumizi ya teknolojia, na ubunifu unaoendelea ndani ya Tume.

“Mafanikio haya ni uthibitisho kuwa sekta ya madini ni nguzo imara ya uchumi wa nchi. Kama alivyosema Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, madini siyo nyanya tuziache zioze – yanapaswa kuchimbwa kwa weledi na kwa kutumia wataalamu wa ndani. Tume ya Madini imetekeleza hilo kwa vitendo,” amesisitiza Dkt. Mwasse.

Aidha, ameeleza kuwa utekelezaji wa mabadiliko ya sheria ya madini umechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio haya, hususan kupitia sera ya Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini (Local Content), inayotoa fursa kwa wazawa kushiriki kikamilifu katika huduma, ajira na biashara zinazohusiana na sekta ya madini. 

Amebainisha kuwa STAMICO ni miongoni mwa mashirika yaliyonufaika moja kwa moja na utekelezaji wa sera hiyo.

Kwa upande wake, Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Tume ya Madini, Bw. Damian Kaseko, ameeleza kuwa Tume ilianzishwa rasmi mwaka 2017 chini ya Sheria ya Madini Na. 7, ikiwa na jukumu la kusimamia kikamilifu shughuli zote za madini nchini. Tangu kuanzishwa kwake, Tume imeendelea kuimarika na kuwa chombo madhubuti katika kusimamia rasilimali za madini kwa manufaa ya Taifa.

Makusanyo haya ya kihistoria ni kielelezo cha mafanikio ya kimkakati katika sekta ya madini na mchango wake mkubwa katika kukuza uchumi wa Taifa, huku yakionesha uwezekano mkubwa wa sekta hiyo kuwa chachu ya maendeleo endelevu kwa Watanzania wote.
Posted by MROKI On Monday, July 07, 2025 No comments

July 06, 2025





Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Cyprian Luhemeja, ameipongeza Tume ya Madini kwa hatua yake ya kutoa leseni za uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wadogo huku ikizingatia vigezo vya utunzaji wa mazingira. 

Ameitaka Tume kusimamia kikamilifu utekelezaji wa masharti ya leseni ili kuhakikisha mazingira yanalindwa ipasavyo.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba, jijini Dar es Salaam, Mhandisi Luhemeja amesema hatua hiyo ni muhimu katika kuondoa uchimbaji holela na kupunguza uharibifu wa mazingira.

“Zamani wachimbaji wadogo wa madini walikuwa wanaingia kwa nguvu kwenye maeneo ya uchimbaji bila kufuata utaratibu wowote, na mara nyingi kuchimba bila kuwa na leseni. Hali hii ilisababisha uharibifu mkubwa wa mazingira,” amesema Mhandisi Luhemeja.

Kwa upande wake, Afisa Sheria Mwandamizi wa Tume ya Madini, Bw. Damian Kaseko, amesema Tume inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Madini, ikiwa ni pamoja na kutoa leseni za uchimbaji, kusimamia biashara ya madini nchini, pamoja na kusuluhisha migogoro ya ardhi  katika maeneo ya uchimbaji wa madini.

Bw. Kaseko ameeleza kuwa utoaji wa leseni  za madini kwa wachimbaji wadogo unazingatia taratibu madhubuti, ikiwemo kuwasilisha Mpango wa Utunzaji na Uendelezaji wa Mazingira (Environmental Protection Plan - EPP) kabla ya kuidhinishiwa leseni ya uchimbaji katika eneo husika.
Posted by MROKI On Sunday, July 06, 2025 No comments

July 05, 2025











Wizara ya Madini kwa kushirikiana na taasisi zake inaendelea kutoa elimu ya kina kuhusu shughuli za madini katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Kupitia banda la Wizara hiyo, wananchi, wawekezaji na wanafunzi wanapata fursa adhimu ya kujifunza kwa undani kuhusu sekta ya madini nchini, kuanzia shughuli za uchimbaji, uchenjuaji, usimamizi wa mazingira, hadi masuala ya usafirishaji wa madini na masoko ya madini.

Akizungumza katika maonesho hayo, Mjolojia kutoka Wizara ya Madini, Neema Masinde, amesema kuwa lengo la ushiriki wa Wizara na taasisi zake ni kuhakikisha wananchi wanaelewa mchango mkubwa wa sekta ya madini katika kukuza uchumi wa nchi pamoja na kuwapa maarifa sahihi kuhusu fursa zilizopo ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za sekta hiyo.

“Tunatoa elimu ili kuwahamasisha wananchi washiriki kwa tija katika sekta hii muhimu, kwani ni miongoni mwa sekta zinazochangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa (GDP) pamoja na kutoa ajira kwa Watanzania,” amesema Masinde.

Maonesho ya Sabasaba mwaka huu yamevutia washiriki kutoka zaidi ya nchi 40, huku banda la Wizara ya Madini likitajwa kuwa miongoni mwa mabanda yaliyovutia idadi kubwa ya wageni kutokana na mvuto wa sampuli mbalimbali za madini na elimu ya moja kwa moja inayotolewa na wataalam waliobobea.
Posted by MROKI On Saturday, July 05, 2025 No comments
Posted by MROKI On Saturday, July 05, 2025 No comments






WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Julai 05, 2025 ameshiriki katika mbio za Great Ruaha Marathon (GRUMA 2025) zilizoanzia na kuishia kwenye eneo la Ibuguziwa, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Akizungumza katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa ameto wito kwa waratibu wa mbio hizo kuweka mikakati ya kuzifanya ziwe za kimataifa ili ziweze kukutanisha raia wa mataifa mbalimbali duniani.

Lengo la Mbio hizo ni kuhamasisha uhifadhi wa mazingira  wa Mto Ruaha Mkuu ambao ni uti wa mgongo wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na kuifanya jamii kuona umuhimu wa kulinda vyanzo vya maji na kuhimiza matumizi endelevu ya rasilimali za asili.
Posted by MROKI On Saturday, July 05, 2025 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo