Nafasi Ya Matangazo

January 24, 2025






Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Jamhuri ya Korea katika kutekeleza mkakati wake wa kuendeleza madini mkakati na muhimu nchini.

Hayo yamesemwa leo tarehe 24 Januari, 2025 na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Korea nchini Tanzania, Mhe. Eunju Ahn katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

"Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitupa maelekezo mahsusi ya kuhakikisha rasilimali hii ya madini mkakati tunaiwekea mfumo thabiti ili Nchi yetu ipate manufaa zaidi. 

Mkakati wa uvunaji madini ambao upo katika hatua za mwisho kukamilika umelenga kutimiza adhma hiyo ya Mhe. Rais wetu.

"Mojawapo ya nguzo mbili muhimu katika Mkakati huo ni kufanya utafiti wa kina ili kutambua aina na kiasi cha madini mkakati kilichopo, pamoja na kuweka mazingira rafiki ya  ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani madini hayo hapa nchini.

Tanzania ni moja ya Nchi chache duniani ambazo zimebarikiwa na uwepo wa madini ya aina zote na kutoa wito kwa wawekezaji kutoka nchini Korea kuchangamkia fursa ya kuwekeza katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini nchini“, alisema Waziri Mavunde

Awali, akieleza lengo la kuomba miadi hiyo, Mhe Balozi Ahn alieleza lengo hasa ni kujitambulisha kutokana na mahusiano ya siku nyingi ya Korea na Tanzania, hususani katika sekta ya madini, na kusisitiza kwamba yupo tayari kuhakikisha mashirikiano hayo yanakuwa na tija kwa nchi zote mbili katika kuendeleza sekta ya madini hususan madini mkakati na kwakuwa tayari kampuni ya POSCO kutoka Korea imeonesha utayari wa kushiriki kwenye mradi wa madini kinywe wa Mahenge,Mkoani Morogoro.
Posted by MROKI On Friday, January 24, 2025 No comments

Bunge Bonanza la mashabiki wa Simba na Yanga wa Mjengoni (Bunge) kufanyika Februari Mosi 2025, viwanja vya John Merlin Sekondari Jijini Dodoma

Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Bunge Bonanza, Mheshimiwa Festo Sanga wakati Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya Bunge iliyopo Jijini Dar es salaam leo tarehe 24 Januari 2025

Alisema Maandalizi ya Bonanza hili linalodhaminiwa na Azania Bank lishakamilika kwa asilimia Mia moja

"Bonanza hilo linahusisha michezo yote ikiwemo Mpira wa Miguu, mpira wa pete, kuvuta kamba na michezo mingine tu" Alisema

Mhe. Festo alisema kwamba Mgeni Rasmi ambaye amependekezwa na Mheshimiwa Spika ni Ndugu Wallace Karia ambaye ni Rais wa TFF ambapo atakuwa na viongozi wengine wa bunge akiwemo Spika wa bunge Mhe. Tulia Ackson, Waziri mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, mawaziri, manaibu mawaziri na viongozi wengine wengi 

Mhe. Festo Sanga amesema lengo la Mhe. Spika kuleta bonanza hili linalohusisha mashabiki wa timu kubwa wa Yanga na Simba ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika juhudi za kupambania maendeleo ya michezo Tanzania, Malengo mengine ni kuendeleza mahusiano yaliyopo kati ya bunge na taasisi nyingine za kiserikali na taasisi nyingine binafsi lakini pia kujenga afya za kimwili ili kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza ambayo kila siku yanaibuka,

Nae Rais wa TFF ndugu Wallace Karia amesema amefurahishwa na mualiko huo na kwamba atashiriki kwa kiwango cha juu sana kuanzia kwenye maandalizi mpaka mwisho wa bonanza hilo, "Wito wangu kwa wana habari ni kuhakikisha mnasambaza hii taarifa ya bunge bonanza ambapo itashirikisha timu zetu pendwa ili kuwafikia wananchi wengi wapate kuhudhuria" Wallace Karia







Posted by MROKI On Friday, January 24, 2025 No comments
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt, Selemani Jafo,akizungumza na wananchi wakati wa zoezi la uzinduzi wa ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.

Na.Mwandishi Wetu
SERIKALI imeagiza kuwa zoezi la ulipaji fidia ya sh, bilioni 6.2 kati ya sh, bilioni 14.48 kwa Wananchi 595 kutoka vijiji vinne vya Engaruka Chini, Mbaash, Idonyonado na Irerendeni. Kata ya Engaruka Wilayani Monduli kwa ajili ya kupisha Mradi wa Magadi Soda likamilike ifikapo Februari 15, 2025.

Akizungumza na Wananchi wa Eneo hilo Januari 2023 kwa niaba ya Rais Samia Hassan Suluhu wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo la ulipaji fidia , Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt, Selemani Jafo alisema fedha hizo za fidia zimetolewa ikiwa ni Mkakati wa kutekeleza Miradi huo wa Kielekezo wenye manufaa makubwa katika kuendeleza sekta ya viwanda, kuongeza ajira, kukuza Pato la Taifa na uchumi kwa ujumla.

Aidha, ameliagiza Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC ) kuhakikisha ulipaji huo unatetendeka kwa haki na kufuatilia malalamiko yote ya wananchi yakayojitokeza kushughulikiwa ipasavyo, kuandaliwa kwa mipango miji itakayoruhusu ujenzi wa hoteli na huduma nyingine za jamii huku akiwataka Wananchi kuchangamkia fursa zitakazojitokeza kupata ajira na na kuendeleza biashara.

Vilevile, alilisisitiza Shirika hilo kusimamia upatikanaji wa Wawekezaji wenye sifa na uwezo na si makanjanja ili Mradi huo ulete manufaa kwa Taifa na Wananchi kwa kurahisisha upatikanaji wa malighafi hiyo nchini na kuokoa fedha nyingi za kigeni zilizokuwa zinatumika kuagiza malighafi hiyo nje ya nchi.

Aidha amewasisitiza Wananchi kupuuza Taarifa potofu ambazo zimekuwa zikienezwa na watu ambao hawaitakii mema nchi yetu kwa kuwa NDC ambao ndio watekelezaji wa mradi huu wamekabidhiwa Cheti cha Ithibati za mazingira kutoka Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC) kinachothibitisha kuwa uchimbaji wa magadi soda katika Eneo la Engaruka hauna athari zozote za kimazingira kwa ndege ain flamingo ambao hawapo eneo hilo.

Dkt Jafo pia amebainisha kuwa Serikali imeweka mpango wa kukahakisha eneo la Engaruka barabara zake zinapitika pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa umeme mkubwa KV 33 kwa ajili ya kuendesha viwanda sanjari na upatikanaji wa huduma za kijamii katika sekta za elimu, afya na maji safi na salama.

Aidha, Viongozi mbalimbali walioshiriki Hafla hiyo wamesema kuwa Mradi hiyo uliosubiriwa kwa miak takribani 20 utakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo katika eneo hilo la Engaruka, Arusha na Taifa kwa ujumla.

Naye Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Geofrey Pinda amesisitiza kuwa Wizara yake itashirikiana na Wananchi wa Wilaya za Longido na Monduli kuweka mipaka na kuwa na mipango bora ya matumizi ya Ardhi katika vijiji vya Engaruka ili kuepuka migogoro kwa kushirikiana na kamati za vijiji.

"Wananchi wasigombanishwe na migogoro ya mipaka kati ya Wilaya za Longido na Monduli wekeni mipaka ili maendeleo yapatikane na wizara hii itatoa ushirikiano saa zote na RC Makonda pale unapoona panakero tuwasiliane ili kutatua migogoro ili wananchi waishi kwa amani "

Vilevile, amewaelekeza Maafisa Ardhi katika Wilaya ya Monduli na Longido kushiriki kikamilifu katika zoezi la kurejesha mawe ya mpaka ya wilaya hizo mbili yaliyong'olewa na kupoteza utambuzi wa mpaka huo.

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge , Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile aliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kufanikisha jambo hilo lililokuwa na historia na fidia hiyo ilipwe kwa kuzingatia usawa na haki ili zoezi hilo lisiingie dosari kwa wananchi katika ulipwaji wa fidia.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda, amesema Arusha ni miongoni mwa mikoa yenye bahati na kadri siku zinavyosonga, Mkoa huu utatoa fursa mbalimbali za maendeleo kwenye sekta za Kilimo, Madini na Michezo, zitakazosaidia wananchi kujikwamua na umaskini akihimiza kuendelea kupewa kipaumbele cha ajira kwa wazawa wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Mkoa wa Arusha.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa Mradi huo wa Kimkakati, Mkurugenzi Mwendeshaji wa NDC Dkt.Nicolaus Shombe amesema Mradi huo wa Magadi Soda umechukua zaidi ya miaka 20 tangu mchakato wake ulipoanza baada ya NDC kufanya utafiti wake na kubaini uwepo wa magadisoda yenye kufikia mita za ujazo Bilioni 3.8 sawa na tani Milioni 787 ambapo kupitia utekelezaji wake, viwanda viwili vikubwa vitakavyogharimu Trilioni 1.6 vitajengwa katika eneo hilo lenye jumla ya ekari 60, 884.

Alisema viwanda mbalimbali zinatumia magadi soda hayo na Tanzania ni waagizaji wakubwa sana wa magadi soda hayo kutoka nchi za Boswana na maeneo mengine huku ikitumia fedha nyingi za kigeni kuagiza hivyo mradi huo unaenda kuhamisha fedha hizo badala ya kununua nje magadi hayo yatatokea Eneo la Engaruka.

Vilevile, alifafanua kuwa Elimu ya fedha imetolewa kwa wananchi waliopo eneo hilo huku wananchi waliolipwa fidia wanapashwa kuondoka katika eneo hilo ndani ya siku 90 zijazo.

Naye Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mhe.Fredrick Lowassa alisema kuwa Wananchi wananyuso za furaha kutokana na fidia hii nakuiomba Seriiali kushughulikia changamoto za miundombinu zilizopo.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt, Selemani Jafo,akizungumza na wananchi wakati wa zoezi la uzinduzi wa ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Geofrey Pinda,akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda,akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
 
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge , Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile,akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah ,akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
 
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt, Selemani Jafo (hayupo pichani) ,akizungumza na wananchi wakati wa zoezi la uzinduzi wa ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo la Kata ya Engaruka Wilayani Monduli ili kupisha Mradi wa Magadi Soda.
Posted by MROKI On Friday, January 24, 2025 No comments

January 23, 2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa, akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Wakili Patrick Kipangula, alipozitembelea ofisi za Bodi hiyo leo tarehe 23 Januari, 2025, Mtaa wa Jamhuri Posta, Jijini Dar es Salaam.
Bw. Msigwa amefanya ziara hiyo ili kufahamiana na watumishi wapya wa Bodi, kukagua ofisi na kujionea maendeleo ya uandaaji wa nyaraka mbalimbali za Bodi kabla haijazinduliwa rasmi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa pamoja na Watumishi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari wakifuatilia wasilisho la utekelezaji wa uandaaji wa nyaraka mbalimbali za uanzishwaji wa Bodi kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Wakili Patrick Kipangula, wakati wa ziara ya kwenye ofisi za Bodi leo tarehe 23 Januari, 2025 zilizopo Mtaa wa Jamhuri Posta jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa, amemuagiza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Wakili Patrick Kipangula, kuhakikisha nyaraka zote muhimu zinazohitajika kwa ajili ya uanzishwaji rasmi wa Bodi hiyo zinakamilishwa mapema ili iweze kuanza kufanya kazi yake.

Bw. Msigwa ametoa agizo hilo leo wakati alipozitembelea ofisi za Bodi hiyo leo tarehe 23 Januari, 2024, Mtaa wa Jamhuri Posta, Jijini Dar es Salaam ili kufahamiana na watumishi wa Bodi, kukagua ofisi na kujionea maendeleo ya uandaaji wa nyaraka hizo kabla uzinduzi rasmi haujafanyika.

“Kwanza mimi niwapongeze sana kwa hatua mliyofikia, lakini Kaimu Mkurugenzi hakikisha unasimamia hizi nyaraka zote mlizozitaja zifanyiwe kazi kwa haraka sana na kukamilika, umuhimu wa kuanza kazi kwa bodi hii unaujua na bahati nzuri wewe ni mtu wa Sheria, ulishiriki tangu mchakato wa uandaaji wa Sheria na kanuni zake, hivyo unayafahamu majukumu yake na unafahamu kwa nini tunahitaji Bodi ya Ithibati,” amesema Bw. Msigwa na kusisitiza;

“Serikali ya Awamu ya Sita tunaona umuhimu wa kuwepo kwa hii Bodi, hivyo ni muhimu sana haya yote yaliyopangwa kufanyika yafanyike na yalete tija na manufaa kwa Tasnia ya Habari, ni muhimu sana”.

Bw. Msigwa amesema baadhi ya nyaraka zinazotakiwa kufanyiwa kazi haraka ni pamoja na Muundo Bodi, Mpango Mkakati wa Bodi wa Miaka Miwili (Strategic Plan), Mkakati wa Mawasiliano wa Bodi (Communication Strategy) na Kanuni za Maadili ya Waandishi wa Habari.

Amesisitiza kuwa Mpango Mkakati wa Bodi ndiyo nyaraka na mwongozo muhimu unaoelezea malengo ya Bodi, majukumu yake, umuhimu wake, vyanzo vya mapato na namna gani taasisi itaendeshwa.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari ilitangazwa tarehe 18 Septemba, 2024 baada ya aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Jerry Silaa kuteua Mwenyekiti wa Bodi Bw. Tido Mhando na wajumbe wake sita pamoja na sekretarieti yenye watumishi 6.

Bw. Msigwa amekuwa kiongozi mkubwa wa kwanza kuitembelea Bodi hiyo tangu ilipohamishiwa chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo baada ya mabadiliko ya Wizara yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mwishoni mwa mwaka jana.
Posted by MROKI On Thursday, January 23, 2025 No comments
Posted by MROKI On Thursday, January 23, 2025 No comments

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Januari 22,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa FCC jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yameongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt.Hashil Abdallah ambapo amesema kuwa mazungumzo hayo ni maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kukaa,kukutana na kujadili mambo yote yayorahisisha shughuli za ufanyaji biashara nchini.

Aidha Dkt.Abdallah amesema katika majadiliano hayo wamepanga kufanya vikao endelevu na kuadhimia kufanyika kwa mkutano mkubwa wa kiseta MPPD ambapo utakuja kufanya majumuisho yaliojadili katika Mkutano huo.

Vilevile ametoa pongezi kwa Shirikisho hilo kwa kuboresha Sera zao na Muundo unaoendana na falsafa za awamu ya sita na kwa kufanya hivyo Serikali itakuwa bega kwa bega na Shirikisho hilo kwani wamedhihirisha kuwa sekta hiyo inabadilika kulingana na mazingira ya Mifumo ya Biashara.

Naye Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bi.Angelina Ngalula amesema kuna mabadiliko wameyafanya kwenye uendeshaji wa taasisi ili kuweza kutoa mchango mkubwa kwa Serikali katika kuimariaha uchumi wa nchi.

Amesema mabadiliko hayo yamefanywa kwenye nyanja za Teknolojia, masuala ya kidigitali ,wafanyabiashara wadogo,vijana ,afya,elimu na mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na kujumuisha taasisi na Mabaraza ya Wilaya ili kutatua kero na kujenga uelewa wa mipango ya Shirikisho na mifumo.

Vilevile ameishukuru Wizara na Taasisi zake kwa ushirikiano kati yao ambao umeboresha utendaji kazi wa Shirikisho kuliko miaka 4 iliyopita ambayo ilikuwa na malalamiko makubwa hasa kwenye tozo pamoja na kuanza mapema maandalizi ya Maonesho ya OSAKA-EXPO nchini Japani.

 
Posted by MROKI On Thursday, January 23, 2025 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo