October 21, 2024
Aidha, ametoa wito kwa Wananchi hao na kutoa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa Viongozi wa Wilaya au Mkoa husika mara wanapoona watu wachache wenye lengo nia ovu yala kuharibu na kudhoofisha Mfumo huo ili kuuimarisha na kuuwezesha kufanya kazi kikamilifu.ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
Hayo yamesemwa Oktoba 20, 2024 na Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Deodatus Mwanyika ( Mb) wakati wa ziara ya Kamati hiyo katika Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuona maendeleo katika zao la Kakao na jinsi Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unavyowanufaisha wakulima Mkoani Morogoro
Aidha amefafanua kuwa nia ya Serikali na Kamati hiyo ni kuhakikisha kuwa Mkulima anapata bei halisi na faida kutokana na Mazao yao kama vile zao la Kakao ambalo lililoongezeka bei kutoka Tsh 4,200 mwaka 2021 hadi Tsh 29,595 mwaka 2024
Vilevile, Mwenyekiti huyo imeielekeza Bodi ya Stakabadhi za Ghala (WRRB) kueneza Mfumo huo katika mikoa yote Nchini pamoja na kuongeza aina idadi ya nyingi za mazao yatakayohifadhiwamazao yanatotumia mfumo huo katika maghala kama vile Karafuu na mengineyo ili kuendelea kuwanufaisha Wakulima.
"Nawapongeza WRRB kwa kufanya kazi vizuri na nawataka muendelee kufanya kazi kwa bidii na ubunifu ili kuwawezesha Wakulima kupata thamani ya Mazao yao. Bodi hii ndio tegemeo katika kumnyanyua Mkulima"
Naye Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe akijibu hoja mbalimbali za Wananchi wa Mvomero amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuwakomboa Wakulima kwa kuhakikisha kuwa wanaongeza tija kwenye uzalishaji kwenye eneo dogo, kuongeza thamani na kuwatafutia masoko ya mazao hayo.
Aidha, alitoa wito kwa Wakulima hao kuendelee kujituma, kufanya kazi kwa bidii na kitumia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa manufaa yao huku akiwaasa wasidanganyike kwa Madali wanaonunua mazao kwa bei ya chini bali wawe wavumilivu kwa muda wa siku tatu hadi tano wakisubiri fedha zao baada ya kuuza mazao kupitia Mfumo huo
Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amewashauri wakulima kuutumia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa kuwa Mkoa wake unalima mazao mengi kujipanga kuongeza uzalishaji wa mazao mengi ya kibiashara hususani zao la Karafuu ambapo umepanga kugawa kila kaya kuwa na miche 40 ya karafuu ikiwa ni mpango wa kuongeza uzalishaji wa zao hilo Mkoani humo
Naye Naye Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB Bw. Asangye Bangu amesema Bodi hiyo imepokea maelekezo wajumbe na ameahidi kuwa Bodi hiyo itaendelea kuusimamia Mfumo huo ili kuhakikisha kuwa unawanufaisha wakulima wa mazao yanayopita katika mfumo.
Nao Wananchi wa Mvomero kata ya Turiani wakiongea na Kamati hiyo wamekiri kuwa Mfumo huo ni mzuri na wamefanikiwa kuuza Kakao kwa bei ya tsh 29,000 na 17,000 kwa kilo mwaka 2024 wakati kabla ya kutumia Mfumo huo waliuza Kakao hiyo kwa Tsh 2500 na wameiomba Serikali kuwachukulia hatua wale wote wanaodhoofisha Mfumo huo ili uendelee kuwawezesha kunufaika na bei za ushindani zilizoko sokoni.
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Frank Chonya ahakikishe mkandarasi anayejenga mabweni, madarasa na vyoo katika shule ya sekondari Mandawa awe ameanza kazi ifikapo Oktoba 24, mwaka huu.
Kongamano la 10 la Jotoardhi Afrika (ARGeo-C10) limeanza kwa mafanikio jijini Dar es Salaam ambapo Wataalam takriban 800 kutoka 21 duniani wameshiriki.
Dkt. Biteko amesema hayo leo Oktoba 21, 2023 nchini Singapore wakati akishiriki mjadala kuhusu nishati akiwa pamoja na Waziri wa Madini na Nishati kutoka nchini Cambodia, Mhe. Keo Rottanak na Waziri wa Maliasili kutoka nchini New Zeland Mhe. Shane Jones wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Kimataifa ya Nishati ya nchini Singapore.
“ Serikali haziwezi kufanya kila kitu zenyewe hivyo ni muhimu kushirikiana na sekta binafsi. Sisi Tanzania tunawaalika sekta binafsi ije kuwekeza katika sekta ya nishati kwa ajili ya kuimarisha uzalishaji, upatikanaji na usambazaji nishati na kuboresha maisha ya watu kwa ujumla,” amesema Dkt. Biteko.
Akizungunzia, ajenda ya nishati safi ya kupikia nchini amesema kuwa ni matokeo ya utafiti uliofanywa na kubaini kuwa idadi kubwa ya Watanzania wanatumia kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia hali inayosababisha magonjwa ya mfumo wa upumuaji na uharibifu wa mazingira.
Ili kupunguza athari hizo, Dkt. Biteko amesema kuwa Serikali imeandaa mkakati unaolenga kuhakikisha Watanzania asilimia 80 wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
“ Serikali imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuhakikisha nishati safi inapatikana kwa urahisi na bei nafuu na hivyo tunawakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika hili kwa sababu soko lipo,” amesema Dkt. Biteko.
Kuhusu jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya nishati nchini, Dkt. Biteko ametaja miradi mbalimbali inayofanywa na Serikali ikiwemo mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2115.
“ Serikali inaendeleza vyanzo vipya vya nishati mfano umeme wa jua, upepo na gesi, aidha kwa sasa asilimia 51 ya umeme unazalishwa kwa maji. Tanzania tumeendelea na maandalizi ya kuziuzia umeme nchi za Kenya, Rwanda, Burundi na sasa tunaendelea na mradi kwa ajili ya kuunganisha na nchi ya Zambia, kupitia Umoja wa Mauzio ya Umeme wa pamoja katika nchi za Afrika Mashiriki na Jumuiya za Kusini mwa Afrika (SADC) tuna soko la uhakika na hivyo tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi,” amesisitiza Dkt. Biteko.
Naye, Waziri wa Madini na Nishati kutoka nchini Cambodia, Mhe. Keo Rottanak amesema kuwa mwaka 1998 nchi yake ilifanya mageuzi makubwa katika sekta ya nishati na kuwa sasa asilimia 99 ya vijiji ina umeme.
“ Tutahakikisha tunafikisha umeme katika nyumba za watu na malengo yetu ni ifikapo mwaka 2030 umeme unaozalishwa kwa jua kuwa mbadala wa umeme unaozalishwa na maji, amesema Mhe. Rottanak.
Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na kutoka nchini New Zeland, Mhe. Shane Jones amesema kuwa nchi yake imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya kusambaza umeme na kuwa inajikita katika kuwekeza katika vyanzo mbadala vya kuzalisha nishati.
Awali akifungua mkutano huo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Viwanda na Biashara wa Singapore Mhe. Gan Kim Yong amesema kuwa mahitaji ya nishati duniani yanazidi kuongezeka siku hadi siku hivyo nchi zinapaswa kubuni vyanzo mbadala na kupunguza madhara yatokanayo na gesi ya ukaa ifikapo mwaka 2050.
Akitoa uzoefu wa nchi yake kwenye kuongeza vyanzo mbadala vya nishati amesema “ Kwa sasa tuko kwenye mkakati wa kuzalisha umeme kwa kutumia haidrojeni na nyuklia ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuongezeka kwa ushiriki wa Kampuni za Google na Amazon ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza kwenye miradi ya nishati jadidifu.” Amesema Mhe. Kim Yong.
Aidha,katika mkutano huo pia umefanyika uzinduzi wa tawi la ofisi ya kanda ya Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA) nchini Singapore.
October 20, 2024
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa mwishoni mwa wiki hii, ameshuhudia madiwani wawili na Katibu Kata kutoka vyama vya CUF na ACT-Wazalendo wakirejea Chama cha Mapinduzi.
October 19, 2024
Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameeleza kuhusu umuhimu wa Madini Bonanza na kueleza kuwa limelenga kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano baina ya Watumishi wa Wizara na Taasisi zake ili kuifanya Wizara kuwa familia moja.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani amejiandikisha kwenye daftari la wakazi katika mtaa wa Chimuli II kwenye kituo cha Shule ya Msingi Chadulu jijini Dodoma leo Oktoba 19, 2024.