Nafasi Ya Matangazo

July 26, 2025

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.



******************
Na. Mwandishi Wetu
Tarehe 29 Oktoba, 2025 ndio siku ya Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Madiwani kwa Tanzania Bara. Jumla ya Wapiga Kura 37,655,559 wamejiandikisha.
 
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele leo tarehe 26 Julai, 2025 kwenye hafla ya uzinduzi wa ratiba ya uchaguzi iliyofanyika kwenye makao makuu ya Tume, Njedengwa jijini Dodoma.
 
“Tarehe 09 Agosti, 2025 hadi tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais. Tarehe 14 Agosti, 2025 hadi tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani na tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais, uteuzi wa wagombea ubunge na uteuzi wa wagombea udiwani,” amesema Jaji Mwambegele na kuongeza…..
 
“Tarehe 28 Agosti, 2025 hadi tarehe 28 Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za uchaguzi kwa Tanzania Bara. Tarehe 28 Agosti, 2025 hadi 27 Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za Uchaguzi kwa Tanzania Zanzibar ili kupisha kura ya mapema na Tarehe 29 Oktoba, 2025 siku ya Jumatano itakuwa ndiyo Siku ya Kupiga Kura”.
 
Akazingumza kuhusu idadi ya wapiga kura waliojiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi huo, Jaji Mwambegele amesema jumla ya wapiga kura 37,655,559 wamejiandikisha na kuongeza kuwa idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 26.55 kutoka idadi ya wapiga kura 29,754,699 waliokuwa kwenye daftari, mwaka 2020.
 
Ameongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar, Wapiga Kura 725,876 wapo katika Daftari la Wapiga Kura la Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na wapiga kura 278,751 wameandikishwa na INEC kwa kuwa hawakuwa na sifa za kuandikishwa na ZEC.
 
“Katika idadi ya wapiga kura 37,655,559 waliopo katika daftari, wapiga kura 36,650,932 wapo Tanzania Bara na wapiga kura 1,004,627 wapo Tanzania Zanzibar,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Ameongeza kuwa kati ya wapiga kura hao, 18,943,455 ni wanawake sawa na asilimia 50.31 na wapiga kura 18,712,104 ni wanaume sawa na asilimia 49.69 na wapiga kura 49,174 ni watu wenye ulemavu.
 
Amesema jumla ya vituo 99,911 vitatumika kupigia kura ambapo vituo 97,349 vitatumika kwa ajili ya kupigia kura kwa Tanzania Bara na vituo 2,562 vitatumika kwa ajili ya kupigia kura kwa Tanzania Zanzibar.
 
“Idadi hii ya vituo 99,911 ni sawa na ongezeko la asilimia 22.49 ya vituo vya kupigia kura 81,567 vilivyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020,” amesema.
 
Jaji Mwambegele ametoa wito kwa wadau wote ikiwa ni pamoja na wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maelekezo yatakayotolewa na Tume.

Posted by MROKI On Saturday, July 26, 2025 No comments

July 25, 2025











WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku mbili nchini Belarus na ametumia ziara hiyo kuwaalika wenye viwanda, makampuni na wafanyabiashara waje kuwekeza nchini.

Waziri Mkuu aliwaeleza wakuu wa taasisi aliokutana nao baadhi ya maeneo ya kimkakati kwenye uwekezaji ambayo ni elimu ya juu, afya, kilimo, TEHAMA, uendelezaji viwanda, madini na kukuza utalii. Alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kukuza uchumi wa Tanzania kwa kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini.

Kwa kuzingatia azma ya Rais Samia, Waziri Mkuu amewahakikishia wenye viwanda na wamiliki wa kampuni zinazotaka kuwekeza nchini, utayari wa Serikali ya Tanzania kushirikiana nazo kwa kuzipatia misaada stahiki zitakapokuja kuwekeza nchini. Amewasihi wenye viwanda vya matreka na mitambo ya kilimo wafungue matawi nchini Tanzania ikiwemo na vituo vya kuhudumuia matrekta (mechanization centres) ili huduma za matrekta ziweze kuwa karibu na wakulima.

Vilevile, jana jioni (Jumatano, Julai 23, 2025) Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kutengeneza mitambo inayotumika kuchimba madini na magari ya migodini; na pia alitembelea kiwanda cha kutengeneza vifaa vya uokoaji na kuzima moto na kusisitiza umuhimu wa kushirikiana na viwanda hivyo ili kuondoa tatizo la uhaba wa vifaa hivyo nchini.

Kampuni na taasisi alizotembelea Waziri Mkuu ni pamoja na kampuni ya kuzalisha na kusambaza dawa na vifaa tiba ya Belmedepreparaty (Republican Unitary Production Enterprises); Kiwanda cha kuzalisha matrekta na mitambo ya kilimo (Minsk Tractor Plant – OJSC); Chuo Kikuu cha Kilimo cha Belarus (BSATU), Kiwanda cha kuzalisha na kusambaza vifaa vya kielektoniki (BelOMO); kiwanda cha uzalishaji na usambazaji wa mitambo na magari makubwa ya kwenye migodi (BELAZ JSC) na kampuni ya kutengeneza na kusambaza vifaa vya uokoaji na zimamoto (POZHSNAB LLC).

Aidha, katika ziara hiyo Waziri Mkuu Majaliwa alikutana na mwenyeji wake, Bw. Alexander Turchin ambapo kwa pamoja walishuhudia utiaji saini wa hati tatu za makubaliano zilizohusu mashauriano ya kisiasa na makubaliano ya kuendeleza sekta za kilimo na elimu.

Vilevile, walishuhudia utiaji saini wa mkataba baina ya Chama cha Wafabiashara, Viwanda na Kilimo ya Tanzania (TCCIA) na Chama cha Wafabiashara wa Belarus unaolenga kukuza ushirikiano wa kibiashara baina ya nchi hizo mbili.

Waziri Mkuu Majaliwa pia alikutana na Wawakilishi wa Muungano wa Kampuni za Belarus zinazofanya biashara na mataifa ya Afrika (AFTRADE); na aliweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya mashujaa.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliambatana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji wa SMZ, Bw. Shariff Ali Sharriff, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika wa Afrika Mashariki, Cosato Chumi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Khatibu Kazungu, Naibu Katibu Mkuu Kilimo, Dkt. Stephen Nindi na Balozi wa Tanzania nchini Urusi na Belarus, Balozi Fredrick Kibuta na watendaji wengine wa Serikali.
Posted by MROKI On Friday, July 25, 2025 No comments

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Julai 25,2025 ametembelea ubalozi wa Tanzania, Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) uliopo Abudhabi.
Alipokelewa na Balozi wa Tanzania UAE  Luteni Jenerali Mstaafu,Yacub Mohmed na watumishi wa ubalozi huo.




 

Posted by MROKI On Friday, July 25, 2025 No comments

July 24, 2025

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amemkabidhi rasmi Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Michuzi Media Group, Bw. Muhidin Issa Michuzi, kwa niaba ya waandishi wa habari wengine waliokidhi vigezo vya kisheria vya kupatiwa vitambulisho hivyo.

Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za JAB jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa jukumu la bodi hiyo kuhakikisha waandishi wote nchini wanatambulika kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari Na. 12 ya mwaka 2016.

Akizungumza baada ya kukabidhi kitambulisho hicho, Wakili Kipangula amempongeza Bw. Michuzi na waandishi wengine waliokwishakamilisha taratibu za kupata vitambulisho vyao, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa ustawi na weledi wa tasnia ya habari nchini.

Ameeleza kuwa bado kuna waandishi wengi ambao maombi yao yamesalia katika hatua ya uhakiki kutokana na changamoto mbalimbali, hususan mapungufu katika viambatisho walivyowasilisha kwenye mfumo wa maombi.

“Mfumo wetu unakagua nyaraka zote kwa uangalifu. Tumebaini maombi mengi yameambatanishwa na nyaraka zisizosoma, nyingine zimejirudia, nyingine zina viambatisho visivyotambulika kisheria kama vile vyeti bandia, na baadhi hawajaambatanisha hata barua za utambulisho kutoka kwa waajiri wao,” alisema Kipangula.

Aidha, amewataka waandishi wa habari ambao bado hawajapata vitambulisho vyao kuhakikisha wanaingia tena kwenye akaunti zao za mtandaoni kupitia mfumo wa JAB, na kuhakiki nyaraka walizoweka, kama zinafunguka na kusomeka ipasavyo kabla ya kupiga simu kuhoji hali ya maombi yao.

Kwa mujibu wa Kipangula, Bodi itaendelea kupitia maombi kwa makundi kadri yanavyowasilishwa, huku ikiweka msisitizo kwa waandishi kuhakikisha wanatimiza vigezo vyote vilivyoainishwa katika mwongozo wa kisheria uliotolewa.

Makabidhiano hayo yanakuja wakati ambapo serikali imeendelea kuhimiza weledi, uwajibikaji, na utii wa sheria miongoni mwa wanahabari nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kulinda uhuru wa vyombo vya habari sambamba na kuhakikisha maadili ya taaluma hiyo yanazingatiwa.
Posted by MROKI On Thursday, July 24, 2025 No comments

July 23, 2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Viongozi na Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa.

Wananchi wakisikiliza hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa Ibada maalaum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (watatu kutoka kulia) akifuatilia Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara. Wengine ni viongozi mbalimbali walioshiriki Ibada hiyo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (watatu kutoka kulia) akielekea kushiriki Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara. Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene na kulia kwake ni mjane wa Hayati Benjamin Mkapa ambaye ni Bi. Anna Mkapa.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiwasili nyumbani kwa aliyekuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa kijijini Lupaso wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais huyo iliyofanyika kijijini hapo. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Juma Mkomi. 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene akiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa wakati wa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais huyo iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.

 

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akitoa utambulisho wa viongozi na wageni walioshiriki Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.


Wananchi wakiwa katika Ibada maalaum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.

 

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Nicholas Mkapa (kulia kwake) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu wa ofisi hiyo, Bi. Salome Kessy (wa kwanza kulia) kabla ya kuanza kwa Ibada maalaum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.

Sehemu ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora wakiwa katika Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.


Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhadhama Kardinali Pengo akiongoza Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.


Viongozi mbalimbali wakiwa katika Ibada maalum ya kumbukizi ya miaka mitano (5) ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara.


Posted by MROKI On Wednesday, July 23, 2025 No comments
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,na Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK,wakibadilishana Mkataba mara baada ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki hafla iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini jijini Dar es Salaam.

Na.Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Tanzania imeweka malengo makubwa ya kibiashara kwa kushirikiana na Uturuki, ikilenga kufikia thamani ya biashara ya Dola za Kimarekani bilioni 1. Hii ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uchumi wa nchi kupitia diplomasia ya kiuchumi na kuongezeka kwa mauzo ya bidhaa za Tanzania katika soko la Uturuki.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,amesema kuwa ushirikiano huo unalenga kuzalisha bidhaa bora na kukuza sekta ya viwanda, kilimo na madini kwa masoko ya kimataifa.

“Kupitia timu ya wataalamu na ushirikishwaji wa sekta binafsi, tutashirikiana katika biashara kama lango kuu la fursa,” amesema Dkt. Jafo.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2024, biashara kati ya Tanzania na Uturuki ilikuwa Dola milioni 284, ambapo Uturuki iliuza bidhaa zenye thamani ya Dola milioni 217 kwa Tanzania, ikionesha fursa kubwa bado hazijatumika kikamilifu.

Waziri Jafo ameeleza kuwa mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Uturuki yameimarika kwa kasi, hasa baada ya kufunguliwa kwa balozi za nchi hizo mwaka 2009 na 2017 mtawalia.

Amesema kuwa ziara za viongozi wakuu wa mataifa haya, ikiwemo ile ya Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan nchini Tanzania na ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Uturuki mwaka 2024, zimekuwa kichocheo kikubwa cha ushirikiano huu.

Vilevile,amesema kuwa makampuni ya Kituruki yamekuwa sehemu ya miradi mikubwa ya maendeleo nchini, kama vile ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ambayo imeleta ajira na fursa mpya kwa Watanzania.

“Makampuni ya Uturuki, hasa kwenye SGR, yameweza kufanya biashara ambayo italeta fursa nyingi kwa wananchi wetu,” amesema Waziri Jafo.

Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK, ameeleza kuwa JTC ni jukwaa muhimu litakalosaidia kuondoa vikwazo vya kibiashara, kurahisisha michakato ya biashara na kuvutia uwekezaji mpya.

“Kamati ya Pamoja ya Biashara itakuwa jukwaa lenye nguvu la kuondoa vikwazo, kukuza uwekezaji, na kufungua fursa mpya kwa mataifa yote mawili,” ameeleza Balozi Goktug.

Ameongeza kuwa Uturuki imejipanga kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu, kilimo, nishati na teknolojia, huku akisisitiza dhamira ya kuimarisha maendeleo ya pamoja chini ya uongozi wa Rais Erdoğan na Rais Samia.

Kwa ujumla, Tanzania ina matumaini makubwa kuwa ushirikiano huu utafungua ukurasa mpya wa maendeleo ya kiuchumi, ajira na mafanikio kwa wananchi wake.
 
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini Dar es Salaam.

Kaimu Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Bw. Ali Goktug IPEK,wakati wa hafla ya kusaini Azimio la Kamati ya Pamoja ya Biashara (JTC) kati ya Tanzania na Uturuki iliyofanyika leo Julai 23,2025 jijini Dar es Salaam.

    

 
Posted by MROKI On Wednesday, July 23, 2025 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo