Nafasi Ya Matangazo

January 14, 2026





WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yoichi Mikami na kujadiliana naye masuala ya uchumi, miradi ya maendeleo na uwekezaji.

Akizungumza na Balozi huyo leo (Jumatano, Januari 14, 2026) ofisini kwake Mlimwa jijini Dodoma, Waziri Mkuu ameishukuru nchi hiyo kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali kama vile barabara ya Arusha hadi Holili, bandari ya Kigoma, miradi ya kilimo na upatikanaji wa vifaa tiba vya huduma za afya ya mama na mtoto.

“Serikali itahakikisha kuwa miradi hii inatekelezwa kwa ufanisi mkubwa na inakamilishwa kama ilivyopangwa,” amesema Dkt. Mwigulu 

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kutuma salamu za pongezi kwa Waziri Mkuu wa Japan, Bibi Sanae Takaichi kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo tangu Oktoba, 2025 na kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo nchini humo. “Tanzania inasisitiza kuendeleza ushirikiano wa karibu na Japan kwa manufaa ya pande zote mbili,” amesema.

Kwa upande wake, Balozi Mikami alimweleza Waziri Mkuu kwamba amefurahishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya kijamii 79 ambayo awali ilikuwa inasuasua na kwamba tangu Septemba, 2024 hadi sasa, imebakia miradi 16 tu.

Alisema nchi yake itaendeleza ushirikiano na Tanzania ambao umedumu kwa miaka zaidi ya 60.
Posted by MROKI On Wednesday, January 14, 2026 No comments


 

Posted by MROKI On Wednesday, January 14, 2026 No comments

January 13, 2026











Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amesema maendeleo ya kweli kwa wananchi huanzia katika mashina ya Chama hicho, akisisitiza kuwa jitihada zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi hupata nguvu kupitia uongozi wa ngazi za chini.

Dkt. Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke tangu chama hicho kianzishwe,  amesema hayo katika mkutano wake na Mabalozi wa Mashina wa CCM katika Wilaya ya Ilala, ikiwa ni hitimisho la ziara yake katika Mkoa wa Dar es Salaam yenye lengo la kuimarisha uhai wa CCM kuanzia kwenye mashina Kwa kauli mbiu ya "Shina lako linakuita".

Akizungumza na Mabalozi hao amesema mashina ndiyo sehemu ya kwanza ya wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo, kwa kuwa ndiko wanakotoka wananchi wenyewe na ndiko changamoto zao halisi zinapojadiliwa.

Ameeleza kuwa mahusiano kati ya maendeleo ya jamii na maendeleo ya kisiasa hayawezi kutenganishwa, kwa kuwa mashina imara huwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji, jambo linaloongeza imani ya wananchi kwa Chama.

Ameongeza kuwa viongozi wa mashina wana wajibu mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, akisema uangalizi wa karibu wa miradi hiyo ndio msingi wa maendeleo yenye tija kwa wananchi.

Aidha, Mwanadiplomasia huyo, amesema Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongeza kazi kubwa inayofanywa na mabalozi hao wa mashina na kwamba chama kitaendelea kuthamini mchango wao mkubwa kwenye mashina.
Posted by MROKI On Tuesday, January 13, 2026 No comments

Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Na Fredy Mgunda, Mufindi.
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.

Shughuli hizo ni sehemu ya mpango endelevu wa upandaji miti unaotekelezwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuendeleza misitu ya kupandwa, kuongeza uzalishaji wa rasilimali za misitu na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msaidizi wa Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Said Singano, alisema uchukuaji wa miche unafanyika kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kitaalamu ili kulinda ubora wa miche.

“Tunasisitiza miche ichukuliwe kwa uangalifu mkubwa ili isiharibu mizizi, kwa sababu ubora wa miche ndiyo msingi wa mafanikio ya upandaji miti mashambani,” alisema Singano.

Shughuli hizo pia zimeongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa Shamba la Miti Sao Hill katika uhifadhi wa mazingira, mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na upatikanaji endelevu wa mazao ya misitu kwa manufaa ya Taifa.

Mmoja wa wananchi walioshiriki zoezi hilo, Bw. Joshua Ng'umbi kutoka Kijiji cha Igowole Wilaya ya Mufindi, alisema ushiriki wake umemsaidia kuongeza kipato na kupata ujuzi mpya katika shughuli za misitu.

“Mbali na kupata ajira, nimejifunza kuchagua miche bora na namna sahihi ya kupanda miti ili iweze kuota vizuri na kukua kwa ubora unaoweza kuleta kipato kizuri wakati wa uvunaji,” alisema Bw. Joshua.

Kwa ujumla, zoezi la uchukuaji miche katika Tarafa za Irundi na Ihalimba limeendelea kuleta manufaa makubwa kwa Shamba la Miti Sao Hill na wananchi kwa kuimarisha juhudi za upandaji miti, kutoa ajira na kukuza uelewa wa masuala ya misitu na uhifadhi wa mazingira.

Posted by MROKI On Tuesday, January 13, 2026 No comments
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akiongea na wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakati wa kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza  katika chuo hicho.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakimaliza Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya wakati akitoa hotuba yake 
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya akikabidhi kiasi cha shilingi milioni mbili kwa uongozi wa chuo kikuu cha Iringa zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao. 
**************
Na Fredy Mgunda, Iringa.
Wanafunzi wa vyuo vikuu wametakiwa kujiepusha na ndoa za rejareja,makundi ya hovyo yenye viashiria vya kuharibu masomo na maisha kwa wanafunzi wenye ndoto ya kuja kulitumikia taifa la Tanzania na nje ya Tanzania.

Akizungumza wakati kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuo kikuu cha Iringa,Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, Dkt Tumaini Msowoya alisema kuwa wanafunzi wanapaswa kuepukana na ndoa za rejareja, makundi ya hovyo na kuwa wazalendo kwa ajili ya maisha yao.


Dkt Msowoya amesema baadhi ya wanafunzi hujikuta wakitumbukia kwenye ndoa za rejareja na kusahau lengo la masomo kutokana na tamaa za kifedha na kuishi maisha mazuri chuo jambo ambalo limekuwa likipoteza dira ya masomo kwa wanafunzi wengi.


"Najua mna miaka zaidi ya 18 hivyo sio watoto Kwa mujibu wa kawaida lakini je, ndoa ndiyo imekuleta chuoni? Wazazi wako wanajua umeoa au kuolewa huku?" amesema na kuongeza, Dkt Msowoya

"Niliwahi kufanya utafiti kuhusu maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu nikagundua wengi wanaishi na wenza ilhali familia zao hazijui. Hii ni hatari,"

Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka makundi yenye viashiria hasi katika masomo na maisha kwa ujumla.

Katika hafla hiyo, alitoa mchango wa shilingi milioni mbili (2,000,000) zilizotolewa na Dikson Mwipopo, Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Iringa, kwa ajili ya kuwaunga mkono wanafunzi hao. 
Posted by MROKI On Tuesday, January 13, 2026 No comments

January 12, 2026







Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi-CCM, Dokta Asha-Rose Migiro, kesho tarehe 13.1.2026 anatarajiwa kuhitimisha ziara yake ya kimkakati katika wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam, kwa kuzungumza na Mabalozi wa mashina.

Ziara ya Dokta Migiro iliyobeba kauli mbiu isemayo ShinaLakoLinakuita, tayari imeshafanyika katika wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na Kinondoni na kesho itafanyika wilayani Ilala kwa kuzungumza pia na Mabalozi wa mashina katika ukumbi wa Diamond Jublee.

Katika ziara yake Katibu Mkuu wa CCM, anazungumzia zaidi nguvu ya wanachama walioko katika mashina, matawi, huku akisisitiza nafasi ya wazee katika kutoa elimu ya itikadi kwa vijana
Siku ya kwanza ya ziara, akizungumza na mabalozi wa mashina wa Wilaya za Temeke na Kigamboni katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa PTA uliopo Sabasaba jijini Dar es Salaam, Dokta Migiro, alisema kuna kila sababu ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinazingatia utaratibu wa kusikiliza maoni na ushauri kuanzia ngazi ya chini badala ya utaratibu wa maelekezo kutoka juu kwenda chini.

Alitumia pia kikao hicho kutoa rai kwa viongozi na wana CCM kuzingatia utaratibu wa kutoa maoni kuanzia ngazi ya chini kwenda juu.

“Nitoe wito kwa viongozi wetu tusifanye utaratibu wa kutoa amri kutoka juu kushuka chini maana uongozi mzuri ni lazima uanzie chini kwenda juu, yale tunayoyapata kutoka kwenye mashina, matawi ndio yatapanda juu kwa lengo la kukiimarisha chama chetu, alisema Dkt.Migiro.

Aidha, siku iliyofuata katika ziara yake, akizungumza na viongozi wa mashina na matawi wa Wilaya za Kinondoni na Ubungo, Katibu Mkuu huyo wa CCM, alisema Chama Cha Mapinduzi hakijengwi katika majukwaa, bali hujengwa kuanzia ngazi ya mashina na matawi, huku akibainisha majukwaa hutumika zaidi kwa ajili ya kutoa hamasa.

“Mashina ndiyo moyo wa CCM kwa kuwa ndiyo yanayokutanisha chama na wananchi moja kwa moja kupitia vikao na shughuli mbalimbali za kijamii na kisiasa, amesisitiza Dk.Migiro, anayeendelea na ziara yake mkolani Dar es salaam yenye kauli mbiu ShinaLakoLinakuita. #ShinaLakoLinakuita
Posted by MROKI On Monday, January 12, 2026 No comments
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), Bw. Moses Mabamba, ametoa ufafanuzi kwa Umma kuhusu hali ya utoaji wa huduma za vivuko katika eneo la Kigamboni, akibainisha hatua madhubuti zinazochukuliwa na Serikali kuhakikisha wanafunzi wanaorejea shuleni kesho wanavushwa kwa kipaumbele maalum.
 
Akizungumza leo tarehe 12 Januari 2026 katika eneo la Kivukoni, jijini Dar es Salaam, Bw. Mabamba alisema kuwa kwa sasa kivuko cha MV. KAZI kipo kwenye ukarabati mdogo ambapo tayari injini mbili mpya zimefungwa pamoja na mifumo mipya ya umeme na mifumo mingine ya uendeshaji. Alibainisha kuwa matengenezo hayo yako katika hatua za mwisho na kivuko kinatarajiwa kuanza kutoa huduma kesho mara baada ya majaribio ya awali kukamilika.
 
Aidha, Bw. Mabamba alieleza kuwa huduma za uvushaji zinaendelea kutolewa kupitia ushirikiano na wadau wa sekta binafsi – Azam Sea Taxi, ambapo wamekubaliana kuwapa wanafunzi kipaumbele katika huduma hiyo ili kuhakikisha wanawahi shule kwa wakati na kwa usalama.
 
“Matarajio yetu ni kwamba Serikali imefanya maandalizi makubwa kuhakikisha wanafunzi wanarejea shuleni bila changamoto. Tumewasiliana na wenzetu wa Azam Sea Taxi na wamekubali kushirikiana nasi kuwavusha wanafunzi kwa kipaumbele wakati tukikamilisha majaribio ya MV. KAZI,” alisema Bw. Mabamba.
 
Aliongeza kuwa ukarabati wa MV. MAGOGONI unaoendelea mjini Mombasa, Kenya, umefikia zaidi ya asilimia 81.3 na kivuko hicho kinatarajiwa kurejea nchini mwezi Aprili 2026. Wakati huo huo, MV. KIGAMBONI kinatarajiwa kumaliza ukarabati mwezi Oktoba 2026. Mara baada ya kurejea kwa vivuko hivyo, TEMESA italipeleka MV. KAZI kwenye ukarabati mkubwa.
 
Alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imejipanga kuhakikisha huduma kwa wananchi, hususan wanafunzi, hazikwami na zinaendelea kama kawaida pia amewaomba radhi wananchi kwa usumbufu wowote unaoweza kujitokeza katika kipindi hiki kifupi cha mpito na kuekeza kuwa Serikali, kupitia TEMESA, inafanya kila jitihada kuhakikisha huduma za vivuko zinaimarishwa kwa ufanisi.
Posted by MROKI On Monday, January 12, 2026 No comments

January 10, 2026





Na Mwandishi wetu, 
Zanzibar
Wananchi wa Zanzibar wameiomba Serikali kupitia Tume ya Madini kuanzisha masoko na minada rasmi ya madini Visiwani humo ili kuwawezesha wafanyabiashara, wachimbaji wadogo na wawekezaji kufanya biashara ya madini kwa uwazi, usalama na bei shindani.

Ombi hilo limetolewa na wananchi waliotembelea Banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara Zanzibar yanayoendelea kufanyika Fumba, ambapo wameeleza kuwa ukosefu wa masoko rasmi na minada ya madini umekuwa kikwazo kwao kushiriki kikamilifu katika biashara ya madini.

Wamesema kuwepo kwa masoko na minada ya madini kutachochea ukuaji wa uchumi wa Zanzibar, kuongeza ajira kwa vijana na wanawake, kuongeza kipato kwa wananchi pamoja na kudhibiti biashara holela ya madini.

Kupitia maonesho hayo, Tume ya Madini inaonesha fursa katika utafutaji wa madini, uchimbaji, uchenjuaji, uongezaji thamani, biashara ya madini pamoja na utoaji wa bidhaa na huduma kwa shughuli za migodini.

Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Mahusiano kwa Umma na Mawasiliano wa Tume ya Madini, Greyson Mwase, amesema sekta ya madini inatoa fursa jumuishi kwa makundi yote ikiwemo wachimbaji wadogo, vijana na wanawake na kuwataka wananchi wa Zanzibar kujiandikisha na kuomba Leseni za Uchimbaji Mdogo wa Madini (PML), kushiriki katika uongezaji thamani wa madini na kutumia mifumo rasmi ya biashara ya madini.

Maonesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara Zanzibar yataendelea hadi Januari 16, 2026, na wananchi wanakaribishwa kutembelea Banda la Tume ya Madini kwa ajili ya kupata elimu, ushauri na kugundua fursa za uwekezaji katika sekta ya madini inayokua kwa kasi nchini.
Posted by MROKI On Saturday, January 10, 2026 No comments

January 09, 2026






Na Calvin Katera - Manyara
Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Maendeleo ya Biashara Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Massana Mwishawa amefunga rasmi mafunzo ya usimamizi wa vihatarishi yaliyofanyika ukumbi wa Mikutano Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara yaliyoanza Januari 5, 2025 na kutamatika rasmi leo Januari 9, 2025.

Akizungumza katika zoezi hilo Kamishna Mwishawa amesema "Usimamizi wa vihatarishi ni nyenzo muhimu katika kuimarisha utawala bora, uwajibikaji na ufanisi wa taasisi. Katika mazingira ya sasa yanayobadilika kwa kasi, Shirika linawajibika na vihatarishi mbalimbali vya kimkakati, kiutendaji, kifedha, kimazingira na kiutawala".

Naye Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Shirika Abdallah Kiwango amesisitiza umuhimu wa Risk Champions kuishi na kutekeleza elimu ya usimamizi wa vihatarishi katika maandalizi ya mipango ya kimkakati, bajeti, utekelezaji wa majukumu ya kila siku, mifumo ya ubora (QMS) pamoja na ukaguzi wa ndani, ili kuongeza tahadhari dhidi ya matukio yajayo. 
 
Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi James Paschal na Mkaguzi wa Ndani (CIA) amesisitiza umuhimu wa mafunzo haya kuwa endelevu katika ngazi zote za usimamizi ili kuongeza uelewa wa pamoja na kuwezesha ugawaji bora wa rasilimali kwa kuzingatia vipaumbele. 

Kadhalika Mwakilishi wa Sehemu ya Mipango, ufuatiliaji na Tathmini  Afisa Uhifadhi Mkuu Bertiller Massawe amewakumbusha Risk Champions umuhimu wa kulisha taarifa katika Mfumo wa Usimamizi wa Vihatarishi wa Shirika (RIMS) ili kuwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi kwaajili ya maamuzi. 

Mafunzo haya yamelenga kukuza ukomavu kwa Maafisa na Askari katika utekelezaji wa majukumu yao na yamejumuisha Maafisa Ishirini na Saba na Askari Watatu kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) pamoja na Mwezeshaji toka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).
Posted by MROKI On Friday, January 09, 2026 No comments







Na: OWM (KAM) - Dar es Salaam
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Rahma Kisuo amehamasisha waajiri nchini kutoa kipaumbele kwa vijana wanaojitolea katika maeneo ya kazi ili kuimarisha mahusiano mazuri pamoja na morali ya kazi kwa vijana hao.

Amesema hayo leo Januari 9, 2026 katika ufunguzi wa kikao kazi cha mafunzo na uboreshwaji mwongozo wa watarajali wa Mwaka 2017 uliowakutinisha Waajiri wote nchini Jijini Dar es salaam.

Aidha, Naibu Waziri kisuo amewataka waajiri kuondoa urasimu katika kuwapokea vijana kwa ajili ya mafunzo ya kazi. Pia amesema kuwa vijana wanahitaji sana fursa hizo ili waweze kupata ujuzi wa vitendo, kujiamini na kujiandaa na ushindani uliopo katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

“Mafunzo ya Uzoefu katika kazi ni nyenzo muhmu katika kujenga taifa lenye nguvu ya uchumi na kijamii.
Imani yangu mshikamano huu mliokuwa nao tutafanikisha kuandaa vijana wenye ujuzi, nidhamu na maadili ya kazi kwa manufaa ya taifa letu,” amesema

Vilevile, ametoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa zilizopo kwa waajiri na wasisite kuomba nafasi zinazotangazwa na wajitokeze ili kuonesha uwezo wao.  Ameongeza kuwa, Mafunzo hayo ni daraja la mafanikio yao ya baadae 

Akizungumza Awali, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus amewashukuru wadau wote kwa kuitikia wito wa serikali na kushiriki kikamilifu katika kikao kazi hicho kwa kuwa watakuwa sehemu ya suluhisho la changamoto ya ajira nchini.

Kikao kazi hicho kimelenga kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa waajiri waliofanya vizuri katika utekelezaji wa programu ya mafunzo Tarajali (Internship); kupata jukwaa la pamoja ili kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuimarisha utekelezaji wa Programu hiyo ili iwe na tija na kukidhi mahitaji ya soko la ajira.
Posted by MROKI On Friday, January 09, 2026 No comments













Na Joyce Ndunguru, Arusha
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), ameizindua rasmi Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) leo Januari 9, 2026, jijini Arusha.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Dkt. Kijaji amewapongeza wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA kwa kuteuliwa kwao, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis Semfuko.

“Kwa namna ya kipekee nikupongeza sana Mwenyekiti wa Bodi ya TAWA, Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis Semfuko kwa kuendelea kuaminiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Bodi kwa awamu nyingine tena. Kwa dhati ya moyo wangu, ninawapongeza wote kwa kuteuliwa kuwa wajumbe wa Bodi ya TAWA, hongereni sana”, amesema Waziri Kijaji.

Sambamba na pongezi hizo, Waziri Kijaji ametoa rai kwa Bodi ya TAWA kuendelea kushirikiana na sekta binafsi katika uboreshaji wa miundombinu kwenye maeneo ya hifadhi, kwa lengo la kuyaongezea thamani, kuvutia wawekezaji na kuongeza idadi ya watalii.

“Ninaielekeza Bodi hii ninayoizindua leo kuwaita wawekezaji waje kuwekeza nasi kwenye miundombinu muhimu ili tuweze kunufaika na vivutio hivyo”, amesema Waziri Kijaji.

Aidha, Waziri Kijaji ameisisitiza Bodi ya TAWA kuendelea kuimarisha ulinzi wa maeneo ya hifadhi pamoja na kuongeza bidii katika udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu kwa kutumia teknolojia ya kisasa, kuongeza vituo vya askari, kuboresha vitendea kazi na kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni nane ifikapo mwaka 2030.

Akitoa neno la shukrani, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA, Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis Semfuko, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumteua kwa mara ya pili kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA.

Aidha, Meja Jenerali (Mstaafu) Semfuko amesema kuwa kwa kushirikiana na wajumbe wa Bodi ya TAWA wataendelea kuwa wabunifu na wazalendo katika kuhakikisha TAWA inakuwa kinara katika uhifadhi, utoaji wa huduma bora na kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.

Sambamba na hilo, Semfuko ameahidi kuwa maelekezo yote yaliyotolewa yatatekelezwa ipasavyo, huku Bodi yake ikishirikiana kwa karibu na Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na wadau wa kisekta katika kuhakikisha malengo ya TAWA yanafikiwa.

Katika hafla hiyo ya uzinduzi, Waziri Kijaji aliambatana na Naibu Katibu Mkuu – Utalii, Bw. Nkoba Mabula, pamoja na viongozi wengine kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.
Posted by MROKI On Friday, January 09, 2026 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo