Nafasi Ya Matangazo

September 14, 2016

WANASAYANSI wanasema kuwa majaribio ya awali yanaonyesha kuwa siku za usoni itawezekana kuwatengeneza watoto bila ya kutumia mayai ya mama.

Wanasayansi hao wamefaulu kutengeneza watoto wa panya kwa kutumia mbegu za kiume na kuziunganisha na seli za kawaida kwa kuzidanganya kudhani kwamba zitatungisha mayai ya kawaida ya uzazi wa panya hao.

Uchunguzi huu unamaanisha kuwa siku za usoni huenda wanawake wasishirikishwe katika utengenezaji wa watoto kabisa, watafiti wanasema kwenye matokeo ya utafiti huo ambayo yamechapishwa kwenye jarida la kimatibabu la Nature Communications.

Wanasayansi hao kutoka Chuo Kikuu cha Bath walianza majaribio hayo kwa kutumia mayai ya uzazi ambayo hayajatungishwa mbegu za kiume.

Walitumia kemikali kufanya ujanja fulani ambao ulielekeza mayai hayo ya uzazi kuwa makamilifu.

Mayai haya ya bandia yanafanana au yana sifa nyingi zilizo sawa sana seli za kawaida kama vile seli za ngozi, katika njia ambayo zinajigawanya na pia kudhibiti chembe zinazoamua maumbile ya viumbe au DNA.

Watafiti wanasema kuwa iwapo kwa kutungisha mbegu za kiume kwenye mayai bandia kunaweza kuzalisha watoto wenye afya kwa panya, basi inamaanisha kuwa siku za usoni mpango huo unaweza ukatumiwa kwa mwanadamu na kwa kutumia seli ambazo ambazo hazitoki kwenye mayai ya uzazi.

Katika majaribio ya panya, uwezekano wa upachikaji mimba uliweza kufaulu mara moja kwa kila mara nne. Hii ni sawa na asilimia 25.

Dkt Tony Perry, mmoja wa watafiti hao aliambia BBC kuwa: "Hi ni mara ya kwanza kwa mtu yeyote kuweza kuthibitisha kwamba kitu kingine chochote, isipokuwa mayai ya uzazi, kinaweza kuungana na mbegu za kiume ili kuzalisha mtoto. Hali hii inafutilia mbali dhana ambayo imekuwepo kwa zaidi ya miaka 200." ISOME ZAIDI HAPA BBC
Posted by MROKI On Wednesday, September 14, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo