Nafasi Ya Matangazo

March 30, 2023

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja akigawa mitungi ya gesi 100 kwa wanawake wajasiriamali.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja amegawa vifaa vya Michezo mashuleni Mkoani Mwanza.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja amegawa vifaa vya Michezo mashuleni Mkoani Mwanza.
Picha ya pamoja.


Vifaa hivyo vya michezo vilivyokabidhiwa kwa shule za Sekondari za Nansio, Bukongo na Namagondo ni pamoja na mipira na jezi vyenye thamani ya shilingi milioni 3,350,000.

Pia katika ziara hiyo, Mhe. Masanja amekabidhi fedha taslimu kiasi cha shilingi milioni 3,000,000 kwa ajili ya kuwasaidia wajasiriamali hao kuendelea kujinunulia nishati gesi kwa ajili ya biashara zao.

Awali akizungumza na wanafunzi hao, Mhe. Masanja aliwaasa kusoma kwa bidii,kuwa na hofu ya Mungu , nidhamu na kuwaonya kutojihusisha na mambo ambayo sio utamaduni wa Mtanzania.

Aidha aliwataka wajasiriamali  kutumia nishati mbadala na kuachana na matumizi ya nishati chafu ambayo ina athari kwa afya ya binadamu na mazingira kwa ujumla.
Posted by MROKI On Thursday, March 30, 2023 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo