Nafasi Ya Matangazo

December 12, 2017


Mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka umetoa  washindi wa wawili wa sh. Milioni  10  katika droo maalumu ya mwisho wa mwaka ili kuwapa wachezaji wa droo hiyo kufurahia sikukuu za mwisho wa mwaka .

Akizungumza na waandishi habari wakati wa kukabidhi hundi hizo  kwa washindi hao , Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba amesema droo hiyo inachezwa majira ya saa tatu na nusu usiku ambayo inakwenda hadi mwishoni wa mwaka.

Kemi amesema  kuwa washindi wote waliopewa hundi ni kutokana na kushinda mchezo huo kwa kufuata taratibu zilizowekwa za  mchezo,Amesema Watanzania waendelee kuchangamkia fursa ya mchezo huo na kuibuka washindi na kufurahi  msimu wa sikukuuu na ziku zinazoendelea.

Kemi amesema kuwa droo ya walioshinda ni maalumu na wakiona umuhimu wataweza kuitumia na droo zingine zikiendelea.Mshindi wa Tatu Mzuka wa Sh.milioni 10, Samson Mwamwenda amesema  hakuamini kama ameshinda kutokana na kusikia watu wanashinda.

Amesema kuwa amecheza kwa wiki mbili akipata sh.2000  na mara ya mwisho akapata sh.10,000 lakini ameweza kushinda milioni 10.
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Samson Mwamwenda,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Godfrey Madeje,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .

Posted by MROKI On Tuesday, December 12, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo