Nafasi Ya Matangazo

April 21, 2024



Na Mwandishi Wetu, Arusha
WACHEZAJI Omary Mmbaga na Scholastica Kaizer wa timu ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (Ulinzi Sports Club) wameibuka mabingwa wa mchezo wa vishale (darts) wa michuano ya Kombe la Mei Mosi Taifa 2024, uliofanyika Jijini Arusha.

Wachezaji hao wazoefu wamekuwa mabingwa wa kwanza katika mashindano hayo baada ya mchezo huo kuingizwa rasmi na kuchezwa kwa mara ya kwanza katika michuano hii,

Aidha, Mmbaga ni mzoefu wa mchezo huo ambapo amekuwa na mwendeleza mzuri wa kushinda katika michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) kwa miaka mitatu mfululizo, Michezo ya Mashirika ya Umma na Binafsi (SHIMMUTA) pamoja na masndano mengine.

Nafasi ya pili kwa wanaume imechukuliwa na Thomas Lemunge kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na nafasi ya tatu kwenda kwa Jerome Ndibalema kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kwa upande wa wanawake nafasi ya pili imechukuliwa na Rehema Abdallah kutoka Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilfu Tanzania (TPHPA) na nafasi ya tatu imekwenda kwa Elizaberth Luwanda kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).

Aidha, mchezo wa Netiboli umezikutanisha timu za Shirika⁰
Posted by MROKI On Sunday, April 21, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo