Nafasi Ya Matangazo

January 25, 2017

Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF)Dk. Reginald Mengi akizungumza jijini Dar es salaam jana wakati akitolea ufafanuzi juu ya baraza la kibiasha baina ya Uturuki na Tanzania lililoundwa juzi baaina ya taasisi hiyo na Bpodi ya mahusiano ya kigeni kwenye masuala ya kiuchumi nchini Utururuki (DIeK). Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji  wa TPSF, Godfrey Simbeye.
Mkurugenzi Mtendaji  wa TPSF, Godfrey Simbeye (kushoto) akizungumzia uundwaji huo wa baraza la kibiashara baina ya Tanzania na Uturuki. Kulia ni Mwenyekiti wa TPSF ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk Reginald Mengi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF)Dk. Reginald Mengi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana juu ya baraza la kibiasha baina ya Uturuki na Tanzania lililoundwa juzi baaina ya taasisi hiyo na Bpodi ya mahusiano ya kigeni kwenye masuala ya kiuchumi nchini Utururuki (DIeK).
Mkurugenzi Mtendaji  wa TPSF, Godfrey Simbeye akifafanua jambo.
*************
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) ni chombo kilichoundwa mwaka 1998 kwa lengo la kuunganisha asasi za sekta binafsi nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara wa taifa kupitia sekta binafsi.

Bodi ya mahusiano ya kigeni kwenye masuala kiuchumi nchini Uturuki (DIeK) na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) wameingia makubaliano kuanzisha Baraza la Kibiashara baina ya nchi hizo mbili. makubaliano haya yalifikiwa tarehe 23 Januari 2017, Dar es Salaam.

Baraza litakuwa na majukumu na shughuli zifuatazo:
· Kusaidia kukuza biashara kati ya nchi hizo mbili
·Kutoa mchango katika kuanzisha na kukuza viwanda, kupitia ushirikiano wa teknolojia wa mashirika na taasisi za kiuchumi za nchini uturuki.
·Kuratibu juhudi za pamoja kukusanya, kuunganisha, kuchambua, kutathmini na kueneza taarifa zinazohusu biashara, viwanda na masuala ya ushiriakiano kwenye teknolojia na uwekezaji; kwa nia ya manufaa ya nchi zote mbili.
·Kutambua changamoto za kibiashara baina ya nchi hizo mbili na kwenye ushirikiano kiuchumi na kuleta mapendekezo ya jinsi gani serikali husika zitakavyo zitatua.
·Kuwasilisha misaada katika kuandaa maonyesho ya kibiashara na kuhamasisha wanachama wa baraza la kibiashara kushiriki kikamilifu katika shughuli za namna hizo.
·Kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati(SMEs) pamoja kuwapa ujuzi na maarifa.
·Kukusnya takwimu na taarifa juu ya fursa katika biashara, uwekezaji na masuala mengine katika ushirikiano kiuchumi, na kusambaza taarifa hii kwa wanachama.

Baraza la kibiashara baina ya Uturuki na Tanzania litagawa katika kamati za kitaifa mbili. Kila kundi litakuwa na wanachama wake na taasisi za kiuchumi au za kibiashara. DEiK itaunda sekretariat ya upande wa Uturuki, na TPSF itaunda sekretariat kwa upande wa Tanzania.

Baraza kuu la biashara litahushisha sekta mbalimbali za nchi hizo mbili na kuendelea kuangalia uwezekano wa ushirikiano zaidi kwa manufaa ya nchi zetu mbili.

Kamati hizi ndogo za Baraza zinatarajiwa kukutana angalau mara moja kwa mwaka, kutazama na kujadili mafanikio ya Baraza kwenye masuala ya kibiashara, uwekezaji,teknolojia baina ya Utruki na Tanzania.
Posted by MROKI On Wednesday, January 25, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo