Nafasi Ya Matangazo

November 08, 2016

Na Bety Alex, FK Blog -Arusha
VILIO na majonzi  vimetawala katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha baada ya Mbunge wa jimbo la Arusha mjini  Godbles Lema kulazimika kwenda mahabusu katika gereza kuu la Kisongo kutokana na kuwekewa pingamizi la dhamana.

Hatua hiyo imekuja  baada ya wanasheria wa serikali wakiongozwa na Maternus Marandu na Paulo  Kadushi kupinga dhamana ya Mbunge huyo kutokana na kile walichodai akipewa dhamana ataendelea kufanya mikutano ya uchochezi.

Pia waliieleza Mahakama hiyo mbele ya hakimu Desderi Kamugisha kuwa uchunguzi wa kesi zingine za uchochezi zinazomkabili alipatiwa dhamana kwa lengo la kujikerebisha lakini ameendela kukiuka utaratibu wa dhamana ambapo alipaswa asifanye tena makosa yanayofanana kila mara

Kwa upande wa mawakili wa upande wa mhishatakiwa wakiongozwa na John Mallya na Ahmed hamisi ,sheck mfinanga  pamoja na charles adieli walisema kuwa mshtakiwa ana haki ya kupata dhamana kwa sababu ni haki ya msingi na kisheria na kesi zinazomkabili bado hazijafanyiwa hukumu hivyo ana haki ya kupata dhamana bila kukiuka taratibu nq sheria za nchi. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

Walisema kuwa mshitakiwa ni mbunge wa kuchaguliwa ndani ya jamhuri ya tanzania mbapo ana2akilisha wananchi hivyo ni vema mahakama ikampatia dhamana kwa ajili ya kuendelea na majukumu aliyochaguliwa nayo.

Mawakili hao walidai pamoja na mbunge huyo kukabiliwa na kesi mbili za uchochezi  namba 440 na 441 za mwaka 2016  ya kutowa  maneno   ya lugha ya uchochezi yanayodai nchi hii haitatawalika  na itaingia kwenye machafuko kama rais hatafuata katiba na sheria bado wanaamini makosa hayo yanastahili kupata dhamana kama sheria ya makosa ya mwenendo ya jjnai.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili hakimu kamugisha alihairisha shauri hilo hadi november 11 itakapokuja kutolewa uamuzi mdogo huku mshitakiwa lema akirejeshwa rumande katika gereza la kisongo kusubiri hatma ya dhamana yake 

Wakati mbunge huyo akiondoshwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi alionekana kujiamini na kushika biblia takatifu akiwa kwenye gari la polisi ambapo ndipo wafuasi hao walianza kuangua kilio wakimlialia mbunge huyo huku wengine wakizimia.

Kufuatia tukio hilo mwenyekiti wa chama cha demokrasi na maendeleo mkoani hapa Amani Golugwa aliwaomba wananchi wa arusha kuwa wavumilivu katika kipindi hiki wakati shauri hilo likiwa mahakamani na kujitokeza kwa wingi kufuatilia kesi hiho.

Awali kabla ya kusikilizwa kwa kesi hiyo mahakama kuu kanda ya arusha  chini ya jaji Salma magimbi alimuamuru mwanasheria wa serikali awe amemleta mshitakiwa ndani ya nusu saa mahakamini hapo baada ya kukaa mahabusu ya polisi kwa zaidi ya masaa 175 kinyume cha sheria ya mwenendo ya makosa  jinai.

Hata hivyo kabla ya amri ya mahakama hiyo polisi walimleta mshitakiwa katika mahakama hiyo majira ya saa mbili asubui na hivyo kurahisisha amri ya mahakama hiyo
Posted by MROKI On Tuesday, November 08, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo