Nafasi Ya Matangazo

November 08, 2016



 MKUU wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Luice Bura (wapili kulia) akiangalia moja ya mashimo ya vyoo ambayo hayajamaliziwa ujenzi wake.
 MKUU wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Luice Bura (katikati) akizungumza wakati wa ukaguzi.
Na FK Blog-Kigoma
MKUU wa Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma Luice Bura amemtaka Kurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kibondo kuwasimamisha kazi watumishi watatu katika kitengo cha ujenzi kwa tuhumaa za  ubadhirifu wa fedha kiasi cha Sh Milioni 109. 

Fedha hizo ni sehemu ya Sh milioni 264 zilizotakiwa kumaliza mradi wa vyumba vitatu vya madarasa na nyumba ya walimu yenye uwezo wa kuishi familia za watu sita na matundu  matano ya vyoo katika Sekondari ya Itaba katani humo. BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Maagizo hayo aliyatoa jana katika kikao cha ulinzi Na usalama ambacho yeye ndiye Mwenyekiti wa kamati hiyo baada ya kufika eneo la  Ujenzi wa vyumba vya madarasa Na vyoo katika shule  za Sekondari Tank na Nyumba za walimu Na kukuta vyoo havija sakafiwa Na vyumba vingine havijajengwa.

Bura aliwataja watumishi watakao simamishwa ni pamoja na Salehe Mbogoye, Felix Ngomano na Haruni Mbapaye kutoka idara ya ujenzi , ambao ndio waliokuwa wakisimamia ujenzi wa majengo hayo na kuchangia upotevu wa sh.milioni 109, ilihali  kiasi cha sh.milioni 46 zimelipwa bila kufanyiwa kazi na ujenzi uliofanyika upo chini ya kiwango huku ujenzi upo  chini ya asilimia 50% na  kuidhinisha  malipo hewa.

" baada ya kupokea  malalamiko  kutoka kwa wananchi kutokana na mradi huo niliamua kuituma Kamati ya ulinzi na usalama ,walifika katika eneo la ujenzi na kukuta ujenzi haujakamilika ambapo matundu ya choo ni mashimo tu, madirisha hayapo sakafu haijawekwa na ninakuomba Mkurugenzi uwasimamishe kwa muda watumishi hao hadI uchunguzi utakapo kamilika kutokana Na tuhuma hizo",alisema Bura.

Hata hivyo Bura alisema cha kushangaza Madiwani wa kamati ya ujenzi  waliomba posho ya kufanya ukaguzi wa ujenzi   na wakapewa posho ya siku tano ,kumbe  hata kwenye eneo la ujenzi hawajafika hali iliyowapelekea watumishi wengine kuangukiwa na barua za maadili ni pamoja na  Ofisa Elimu Sekondari Wilaya Honolata Kabundugulu, Fedy Eliasafu Ofisa Maliasili na Ofisa kilimo wilaya Said Shemahonge ambao wataitajika kujibu tuhuma hizo.      

Akitoa ufafanuzi juu ya mradi huo Mjumbe wa kamati ya maendeleo ya kata husika Bosco Ngomagi alisema serikali ihakikishe inashirikisha wananchi wa eneno husika,ili kuondoa uhujumu uchumi wa jamii ambapo kamati husika watasimamia mradi husika Na wannchi wtafuatilia kwa ukaribu ilikujua no kiasi gani kimetengwa ilikuweza kukamilisha mradi Na mradi ukamilike kwa wakati.

Nao baadhi ya Vibarua kutoka kampuni iliyochukua zabuni ya ujenzi ya Mangalazi Engenearing ya Kigoma Mjini  Paschal Leonardi walimuomba mkuu huyo awasaidie  malipo yao kwa kuwa fedha nyingi zimeshatumika Na wao hawajapata malipomyao mpakasasa wanaendelea Na kazi lakini mpakaka sasa kunabaadhi wamechukua fedha hizo bado hawajawalipa.
Posted by MROKI On Tuesday, November 08, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo